Monday, March 11, 2013

Wamiliki wa Televisheni waitaka serikali iache kulazimisha watu kutumia Ving'amuzi na badala yake waruhusu kurejea kwa mfumo wa zamano wa analojia

Mwenyekiti wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Dk. Reginald Mengi
Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT) wameitaka serikali kuacha mara moja utaratibu wake wa sasa wa kulazimisha matangazo yote ya televisheni nchini kurushwa kwa digitali kupitia ving'amuzi na badala yake irejeshe utaratibu wa zamani kwani hivi sasa wao wamekuwa wakipata hasara kubwa.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo, mwenyekiti wa MOAT, Dk. Reginald Mengi, ambaye aliambatana na wakurugenzi wa Sahara Communications (Star TV) na wa Clouds Media, alisema kuwa utaratibu wa sasa unaowalazimisha wananchi wote kupata matangazo ya televisheni kupitia ving'amuzi umekuwa ukiwakosha wengi matangazo hayo na matokeo yake, wao huathirika kwa kukosa pesa za kuendeshea shughuli zao kupitia matangazo ya kibiashara kama ilivyokuwa zamani.

Wamiliki hao wameitaka serikali kutoa uhuru kwa wananchi wote kupata matangazo kwa njia wanazotaka wenyewe za digitali na analojia (antena za kawaida) kulingana na utashi wao na pia uwezo wao kiuchumi badala ya ilivyo sasa ambapo wengi wamekuwa wakikosa uwezo wa kununua ving'amuzi na kuvilipia kila mwezi, hivyo kukosa matangazo yao na mwishowe kuwaingizia hasara wamiliki wa vituo vya televisheni.

Mengi ameongeza kuwa hadi sasa bado wanaendelea kufanya taratibu za kuisihi serikalini itekeleze yale wanayoomba na kwamba, wataendelea kufanya subira kwa miezi kati ya miwili hadi mitatu kuanzia sasa na wakiona kuwa bado serikali iko kimya, watakachokifanya ni kufunga vituo vyao vyote vya televisheni kwani ni bora waendelee na biashara nyingine kuliko ilivyo sasa ambapo kila uchao wamekuwa wakipata hasara.

Serikali ililazimisha kuanza urushaji wa matangazo kupitia ving'amuzi kuanzia Januari Mosi, 2013 na kuzima kwa awamu matangazo yote ya televisheni kupitia njia iliyokuwa ikitumika awali ya analojia isiyohitaji ving'amuzi bali antena za kawaida.

Oscar Pisorius anaelekea kukata tamaa

 Oscar Pistorius anakana madai ya kumuua mpenzi wake Reeva

Mwanariadha wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius, anayetuhumiwa kwa mauaji ya mpenzi wake, huenda akajinyonga, rafiki wa karibu wa familia yake ameambia BBC.
Mwanariadha huyo, amejipata pabaya baada ya kulazimika kuuza baadhi ya mali zake ili kugharamia kesi yake, alisema Mike Azzie.
Bwana Azzie alitoa matamshi yake katika kipindi cha BBC, kuhusu kesi inayomkabili Pistorius, ambapo mwanariadha huyo anakanusha madai hayo.
Wakati huouo, mawakili wa mwanariadha huyo , wameomba mahakama kulegeza vikwazo vya dhamana aliyopewa.
Bwana Pistorius, ambaye anakabiliwa na kesi kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp nyumbani kwake mwezi jana, anakanusha madai kuwa alipanga kumuua Reeva akisema hakujua kama ni yeye wakati wa kitendo hicho.
Aliachiliwa kwa dhamana tarehe 22 mwezi Februari na kesi itasikilizwa tena mwezi Juni.
Bwana Azzie, ambaye amekuwa akiwasiliana na Pistorius, alisema kuwa ana wasiwasi kuhusu hali yake ya kiakili
Azzie, ambaye Oscar humuiya mjomba, Mike, alisema kuwa manariadha huyo, amelazimika kuuza farasi wake ili kugharamia kesi yake.
''Hajiamini hata kidogo na ni kama tu ambaye anazunguka zunguka asijue anakokwenda,'' alisema bwana Azzie
"naweza kusema kwa kuongea naye tu, anaonekana kama mtu aliyevunjika moyo sana. Naweza kusema anakaa kama mtu ambaye amekata tamaa na hata anaweza kujinyonga . Na hiyo inatia wasiwasi mkubwa,'' alisema Azzie katika kipindi maalum kuhusu Oscar.

Mshukiwa wa ubakaji ajinyonga India

Maandamano yalifanyuika baada ya ubakaji huo mjini Delhi kulaani kitndo hicho cha unyama

Mshukiwa katika kesi ya ubakaji wa msichana mmoja wa chuo kikuu ambaye baadaye alifariki nchini India, amepatikana amefariki gerezani. Haya yamethibitishwa na wakili wake.
Polisi wanasema kuwa Ram Singh, alijinyonga akiwa ndani ya gereza la Tihar mjini Delhi's Tihar, lakini mawakili wa utetezi wanadai kuwa huenda alinyongwa.

Ram Singh, aliyekua na umri wa miaka 33, alikuwa mmoja wa washukiwa katika kesi ya ubakaji wanaozuiliwa na polisi kwa madai ya mauaji ya msichana waliyembaka.
Wote walikanusha madai hayo.
Shambulizi dhidi ya mwanafunzi huo, lililofanyika Disemba mwaka jana, lilizua mjadala mkali nchini India kuhusu wanawake wanavyodhulumiwa.
Jela la Tahir ambako washukiwa wa ubakaji wanazuiliwa 

Kesi ya mshukiwa wa sita inaendeshwa katika mahakama ya watoto.
Mwandishi wa BBC Sanjoy Majumder,mjini Delhi,anasema kuwa kifo cha bwana Singh kinakuja kama aibu kubwa kwa maafisa ambao wanakabiliwa na shinikizo kubwa kuhusu kesi hiyo.
Msemaji wa jela hiyo Sunil Gupta, aliambia BBC kuwa Ram Singh alijinyonga kwa banketi usiku wa kuamkia leo.

Wanafunzi Wa Chuo Wazichapa Kwaajili ya Kugombania Mabwana

https://fbcdn-sphotos-h-a.akamaihd.net/hphotos-ak-ash4/321251_566650766697301_37412131_n.jpg
Hii sasa ni laana kwa dada zetu kwa kufikia hatua hii ya kupigana na kuzalilishana na kuachana uchi tena mbele za watu kisa wanaume:Tunawaomba wakina dada wajiheshimu jamani:

FIFA yaichimba mkwara Serikali ya Bongo


Taarifa zilizoingia hivi punde ni kwamba shirikisho la kimataifa la soka duniani FIFA limeifungia Tanzania kwenye mashindano yote ya kimataifa yaliyo chini. Kwa taarifa zaidi endelea kufuatilia mtandao huu.
source shaffih dauda

Duuuuh!! mtoto wa miaka 8 afunga ndoa na bibi yake

Eight-Year Old Sanele Masilela walks down the aisle with his 
61-year-old bride Helen Shabangu at their wedding ceremony in Tshwane, 
South Africa
Eight-Year Old Sanele Masilela walks down the aisle with his 61-year-old bride Helen Shabangu at their wedding ceremony in Tshwane, South Africa
Ceremony: The schoolboy kisses his 61-year-old bride, who is 
already married and a mother of five. He said he had been told to tie 
the knot by his ancestors
With this ring: The boy's family say the wedding was simply a 
ritual and not recognised in law
With this ring: The boy's family say the wedding was simply a ritual and not recognised in law


Duniani kuna mambo --- Dogo wa miaka 8 aliyeoa mwanamke wa miaka 61 nchini Afrika Kusini.

WANANCHI WA MOROGORO WAMPONGEZA PADRE RICARDOMARIA

Padre Ricardo Maria ambaye anamiliki shule mbili za sekondari mkoani morogoro nilimnasa juzi kati pande za Mji mpya mkoani hapa akielekea kwenye moja wa shule zake zilipo maeneoe ya Nane Nane akitumia usafiri wake wa baiskeli.

Habari kutoka ndani ya shule hizo za raia huyo wa ltalia zinadai kwamba mtumishi huyo wa mungu asiye vaa viatu kutokana na imani ya dhehebu lake,hupokea watoto yatima na kuwasomesha bure kwenye shule zake. 

Mungu akubariki sana mtumishi wa mungu usiyekuwa na makuu licha ya kujaliwa kuwa na kipato kizuri ikumbukwe pia Padre huyu ni mmoja wa wakurugenzi wa Radio Ukweli inayomilikiwa na kanisa katoriki jimbo la Morogoro.[PICHA NA DUSTAN SHEKIDELE,MOROGORO]

Tigo yampeleka nchini China Mshindi wa Promosheni ya Ascend Y200 Bw.Christian Mkama.


Mshindi wa droo ya Ascend Y200 ya mwaka jana bw. Christian Evarist Mkama akiongea na waandishi wa habari uwanja wa ndege wa kimataifa JK Nyerere kabla ya safari kuelekea nchini China.
Mshindi wa droo ya Ascend Y200 ya mwaka jana bw. Christian Evarist Mkama akiwa na mama mzazi Bi. Eva Christian Amuko na mjomba wake bw. Fortunatus Christian Amuko uwanja wa ndege JK Nyerere kabla ya safari kuelekea nchini China.
Tigo Tanzania imempeleka Bw. Christian Evarist Mkama nchini China ambaye ni mmoja kati ya washindi wawili wa droo ya kwanza ya Ascend Y200 ambayo ilifanyika mwaka jana tarehe 19 Desemba.
 
Kwa kuwa mshindi wa droo hii amejishindia tiketi ya bure ya kwenda na kurudi nchini China pamoja na kulipiwa gharama zote za safari,chakula na dola 200 kwa siku za matumizi.
 
Akiwa nchini china mshindi huyu atakaa siku nne na atatembezwa na kuonyeshwa sehemu mbalimbali za mji wa Guangzhou, na kupelekwa kwenye sehemu za utalii ya mlima Lotus.
 
Promosheni ya AscendY200 ilizinduliwa mwaka jana 2012 mwezi wa kumi(oktoba) kwa jumla kutakuwa na droo tano za Ascend Y200 na kila droo itakuwa na washindi wawili kwa jumla ya washindi kumi watapatikana kwenye droo hizi.
 
Kushiriki kwenye shindano hili mteja wa Tigo inambidi awe amenunua simu ya Ascend Y200 kwenye maduka ya Tigo yaliyosajiliwa na kujisajili kwenye kifurushi cha A-Smart package.

GHASIA ZAIBUKA KENYA




Polisi wa kutuliza ghasia, wamelazimika kutumia mabomu ya machozi nchini Kenya, mji wa Kisumu kuwatawanya waandamanaji waliokuwa wakipinga matokeo ya urais ambayo mgombea wao, Raila Odinga alishindwa katika uchaguzi uliofanyika nchini humo.
Vurugu hizo ziliibuka, baada ya kutangazwa kwa matokeo ya urais yaliyompa ushindi Uhuru Kenyatta.

DOKEZO
Mahakama Kuu ya Kenya ndicho chombo pekee chenye uwezo wa kutengua matokeo ya urais yaliyotangazwa IEBC.

Jopo la majaji watano ndilo litakalosikiliza rufaa ya mgombea wa Cord, Raila Odinga; nao ni Jaji Mkuu, Dk. Willy Mutunga ambaye ni Rais wa Mahakama hiyo, wengine ni Majaji Dk. Smokin Wanjala, Njoki Ndung’u, Philip Tunoi, Jackton Boma Ojwang na Mohamed Ibrahim.

Source: Mwananchi, Jumatatu, Marchi 11, 2013

MAAFISA WA POLISI MBEYA WASIMAMISHWA KAZI KWA UPOTEVU WA DAWA ZA KULEVYA

Sehemu ya mbele ya gari ikiwa imefunguliwa kwa uchunguzi zaidi
Picha chini :Askari polisi akilinda sehemu ya madawa ya kulevya yaliyotolewa kwenye gari hiyo

TAARIFA zilizotufikia hivi punde zimesema kuwa Waziri wa mambo ya ndani Dr. Emmanuel Nchimbi amewasimamisha kazi badhi ya maofisa wa polisi kwa upotevu wa madawa ya kulevya uliotokea mwaka jana 2012 mkoani Mbeya katika mazingira ya kutatanisha.

Baadhi ya maofisa hao ni kamanda wa kikosi cha upelelezi mkoani Mbeya (RCO) Elis Mwita, naibu RCO Jacob Kiangi na mkuu wa kikosi cha FFU Charles Kinyongo.

WAKATI WABUNGE WAKITESA, MADEREVA WAO WALIA NA NJAA KALI

WAKATI wananchi wengi, wakikabiliwa na ugumu wa maisha, madereva wa wabunge nao wameibua kilio chao wakilalamikia ukali wa maisha. Madereva hao, walilazimika kumwandikia barua Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila wakilalamikia haki zao kukaliwa na wabunge. MTANZANIA imefanikiwa kunasa barua hiyo ya Julai, 2012 ambayo imesainiwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Madereva wa Wabunge, Juvenille Joseph.

Pamoja na mambo mengine, barua hiyo inaishutumu Ofisi ya Bunge kushindwa kusimamia maslahi yao, hali inayowafanya waishi kwa shida.

Katika barua hiyo, madereva hao walilamikia suala la ukosefu wa mikataba ya kazi, huku wakitaka posho na mishahara yao itenganishwe kutoka katika akaunti za wabunge.

“Mheshimiwa Katibu wa Bunge, sisi ni madereva wa waheshimiwa wabunge, tunaleta kwako hoja zetu ili ziweze kupatiwa ufumbuzi wa kina katika ofisi yako.

“Kwa kipindi chote, madereva wa wabunge hatukuwa na mikataba ya ajira zaidi ya makubaliano ya mdomo baina ya dereva na mbunge.

“Ndiyo maana kunakuwa na unyanyasaji mkubwa kwa baadhi ya waheshimiwa wabunge dhidi ya madereva wao.


“Tunaomba ofisi yako izingatie kuwa kazi ya ubunge ni ya kipindi cha miaka mitano, bila mkataba ni vigumu kujua suala la haki za kikazi.

“Hivyo basi, tunaomba ofisi yako isimamie kuhakikisha kuwa wabunge wote wanatoa mikataba ya ajira kwa madereva wao,” ilisema sehemu ya barua hiyo.

WALIOSEMA MHE. LOWASSA ALIKUWA HAPENDWI NA MWALIMU NYERERE NA AELEWANI NA FAMILIA YAKE WAUMBUKA

Ni baada ya kualikwa kuongoza harambee ya kuchangia miradi ya maendeleo Wilayani Butiama



Mke wa Baba wa Taifa,Mama Maria Nyerere na Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa wakiwasili kwenye hafla ya harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Butiama mkoa wa Mara chini ya Padri Wojciech Adam wa kanisa Katoliki la Kiabakari,iliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Rais wa Bodi ya Mradi huo,Dkt. Patrick Mugoya.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akizungumza machache kabla ya kuanza harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Butiama mkoa wa Mara chini ya usimamizi wa Padri Wojciech Adam (hayupo pichani) wa kanisa Katoliki la Kiabakari lililopo wilayani humo,Hafla hii ilifanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Mke wa Baba wa Taifa,Mama Maria Nyerere akizungumza machache wakati wa hafla ya harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Butiama mkoa wa Mara chini ya Padri Wojciech Adam wa kanisa Katoliki la Kiabakari,iliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.ambapo Mgeni Rasmi katika harambee hiyo,alikuwa ni Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa.
Padri Wojciech Adam wa kanisa Katoliki la Kiabakari akitoa historia fupi ya mradi huo toka kuanza kwake mpaka walipofikia wakati wa hafla ya harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Butiama mkoa wa Mara,iliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.ambapo Mgeni Rasmi katika harambee hiyo,alikuwa ni Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa.
Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini,Mh. Nimrod Mkono akizungumza machache wakati wa kukabidhi mchango wake na kuahidi kuendelea kuchangia ili kuhakikisha ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Butiama mkoa wa Mara inafanikiwa huku akisikilizwa kwa makini na Mgeni Rasmi wa Harambee hiyo,Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa pamoja na Mke wa Baba wa Taifa,Mama Maria Nyerere.
Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini,Mh. Nimrod Mkono akikabidhi mchango wake kwa Mke wa Baba wa Taifa,Mama Maria Nyerere huku akisaidiwa na Mgeni Rasmi kwenye hafla hiyo,Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akimkaribisha Brigedia Jenerali,Zoma Kongo kukabidhi mchango wake kwa Mama Maria Nyerere kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Butiama mkoa wa Mara.
Mke wa Baba wa Taifa,Mama Maria Nyerere akiteta jambo na Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa wakati wa hafla ya harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Butiama mkoa wa Mara,iliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Free Media,Ansbert Ngurumo ampa mkono Mama Maria Nyerere mara baada ya kutoa ahadi yake ya kuchangia ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Butiama mkoa wa Mara.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akimkabidhi picha Boss Mkuu wa Mgahawa wa BreakPoint mara baada ya kununua kwenye mnada aliouendesha yeye mwenyewe.Katikati ni Mke wa Baba wa Taifa,Mama Maria Nyerere.
Padri Wojciech Adam wa kanisa Katoliki la Kiabakari akipeana mkono na Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini,Mh. Nimrod Mkono.
Rais wa Bodi ya Mradi huo,Dkt. Patrick Mugoya akizungumza machache kwenye hafla hiyo.
Meza kuu.
Mke wa Baba wa Taifa,Mama Maria Nyerere (kushoto) na Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa (kulia) wakiwa kwenye hafla ya kuchangisha fedha za ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Butiama mkoa wa Mara chini ya Padri Wojciech Adam (katikati) wa kanisa Katoliki la Kiabakari,iliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
 
 
Wadau Mbali mbali waliohudhulia hafla hiyo.
NA ISSA MICHUZI MATUKIO

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...