Wednesday, June 17, 2015

PROF. LIPUMBA, DK. SLAA, ZITTO, KUVAANA KWENYE MDAHALO

Dk.Wilbroad Slaa akiwa na Profesa Ibrahim Lipumba 

Umoja wa watendaji wakuu wa kampuni wa CEO RoundTable (CEOrt) umeandaa mdahalo wa kuzungumzia mbio za urais utakaowahusisha viongozi wa vyama vya upinzani, Profesa Ibrahim Lipumba, Dk Willibrod Slaa, Zitto Kabwe na Emmanuel Makaidi, lakini Chadema imesema itakuwa tayari kwa midahalo baada ya mchakato wa ndani kukamilika.

Kauli hiyo ya Chadema inaweza kuwa kikwazo kingine kwa CEOrt kuendesha midahalo hiyo baada ya wa kwanza uliokuwa uhusishe makada 10 wa CCM wanaoomba ridhaa ya chama hicho kuwania urais, kushindwa kufanyika kutokana na viongozi wa sekretarieti kutoa kauli tofauti siku moja kabla.

Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNI 17, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.


. .
 Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

SERIKALI YA MUUNGANO WA PALESTINA KUVUNJIKA


Rais Mahmoud Abbas wa Palestina
Rais wa Palestina amesema kuwa serikali ya muungano kati yake na wanamgambo wa Hamas itavunjika.
Bwana Mahmud Abbas ameliambia vuguvugu lake la Fatah, kuwa lazima uhusiano huo uvunjike kwa kuwa Hamas haitairuhusu serikali yake kuendesha shughuli katika eneo la Gaza, ambako wameshikilia wao.
Kiongozi wa Hamas kushoto Khaled Meshaal na rais wa Palestina Mahmoud Abbas
Serikali hiyo iliundwa mwaka uliopita na ilitarajiwa kumaliza uhasama kati ya makundi hayo mawili lakini malengo yake yamekumbwa na matatizo mengi.
Hamas wanaongoza Gaza ilhali kundi la bwana Abbas la Fatah limeshikilia maeneo ya wa Palestina ya West Bank.

 Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

OPERATION ZA UN ZIFANYIWE MABADILIKO

Baraza la usalama la umoja wa mataifa
Ripoti iliyoandaliwa kwa hisani ya umoja wa mataifa imeelezea kuwa oparesheni za kulinda usalama za shirika hilo zinahitaji kufanyiwa mabadiliko makubwa.
Ripoti hiyo imekusanywa baada ya madai kutolewa hivi karibuni dhidi ya vikosi vya umoja huo vya kulinda amani kwamba baadhi wamekuwa wakiwanyanyasa kingono watoto wadogo.
Miongoni mwa mapendekezo ya ripoti hiyo ni kuwa nchi ambako maafisa husika wanatoka, zisikubaliwe kuchangia tena wanajeshi katika vikosi vya umoja wa mataifa.
Pia ripoti hiyo inasema kuwa wanajeshi waliotajwa kuhusika na uovu huo wanastahili wakabiliwe na sheria, na nchi zao pia zinafaa kushurutishwa kueleza wazi ni hatua zipi za adhabu zilizochukuliwa dhidi yao.
Pendekezo jingine lililotolewa katika ripoti hiyo ni kuwa madai yote ya unyanyasaji wa ngono yanastahili kufanyiwa uchunguzi wa kina kwa chini ya miezi sita.
 Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

RATIBA YA MECHI ZA EPL YATOLEWA


Meneja wa Chelsea Jose Mourinho
Chelsea itaanza utetezi wa taji la ligi ya Uingereza wakati itakapoikaribisha nyumbani Swansea katika wikiendi ya tarehe 8-9 mwezi Agosti.
Manchester City iliomaliza pointi nane nyuma ya Chelsea itaelekea West Bromwich huku Manchester United ikikabiliana na Tottenham katika uwanja wa Old Trafford.
Arsenal
Arsenal itaialika West Ham ,Liverpool ikienda Stoke,Newcastle itakabiliana na Southampton huku Leicester ikiialika Sunderland nyumbani.
Bournemouth iliopandishwa daraja,Watford na Norwich zitakabiliana na Aston Villa,Everton na Crystal Palace mtawalia.
Manuel Pellegrini
Msimu huu utanza wiki moja mapema ikilinganishwa na msimu uliopita.  Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

MAN CITY YATOA MILIONI 35 KUMNUNUA STERLING

Man City yatoa pauni milioni 35m kumnunua Raheem Sterling

Klabu ya Manchester City imeimarisha ombi la kumsajili mashambulizi machachari wa Liverpool Raheem Sterling.
Mabingwa hao wa mwaka wa 2014 wametoa pauni milioni 35 sawa na dola milioni 55 kusajili huduma za mshambulizi huyo.
The Reds walikataa ombi la kwanza la kumsajili kiungo huyo mwenye umri wa miaka 20 wakisema thamani yake ni pauni milioni 50.
Kuwepo kwa mchezaji huyo raia wa Uingereza katika soko kumetokana na nia yake ya kuondoka Liverpool .
Sterling alijiunga na Liverpool mwaka wa 2010 akitokea QPR kwa mkataba utakaomalizika mwaka wa 2017.
Brendan Rodgers anamtarajia Sterling kusalia Anfield hadi kandarasi yake itakapokatika 2017.
Hata hivyo alizua mjadala baada ya kuzima pendekezo la nyongeza ya mshahara wake hadi pauni laki moja kwa wiki.
Manchester City inaaminika kuwa iko tayari kutoa marupurupu mengine yatakayofikisha gharama yake hadi pauni milioni 40 japo wanalalamika kuwa Liverpool imeongeza maradufu thamani yake ikifahamika kuwa wenyewe hawakuwa hata wakimlipa pauni laki moja kwa juma.
Kwa upande wake kocha Brendan Rodgers anashikilia kukutu kuwa anamtarajia Sterling kusalia Anfield hadi kandarasi yake itakapokatika.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...