Wednesday, June 17, 2015

SERIKALI YA MUUNGANO WA PALESTINA KUVUNJIKA


Rais Mahmoud Abbas wa Palestina
Rais wa Palestina amesema kuwa serikali ya muungano kati yake na wanamgambo wa Hamas itavunjika.
Bwana Mahmud Abbas ameliambia vuguvugu lake la Fatah, kuwa lazima uhusiano huo uvunjike kwa kuwa Hamas haitairuhusu serikali yake kuendesha shughuli katika eneo la Gaza, ambako wameshikilia wao.
Kiongozi wa Hamas kushoto Khaled Meshaal na rais wa Palestina Mahmoud Abbas
Serikali hiyo iliundwa mwaka uliopita na ilitarajiwa kumaliza uhasama kati ya makundi hayo mawili lakini malengo yake yamekumbwa na matatizo mengi.
Hamas wanaongoza Gaza ilhali kundi la bwana Abbas la Fatah limeshikilia maeneo ya wa Palestina ya West Bank.

 Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...