Wednesday, March 13, 2013

CARDINAL JORGE MARIO BERGOGLIO ACHAGULIWA KUWA PAPA MPYA; KUTUMIA JINA LA PAPA FRANCIS

Hatimae Jopo la Makardinali 115 wa Kanisa katoliki wamemchagua Kardinali wa Buenos Aires kutoka Latin Amerika Jorge Mario Bergoglio (68) kuwa kiongozi mpya atakaye chukuwa nafasi ya  Papa Benedict aliyejiuzuli hivi karibuni.

Jorge Mario Bergoglio ambaye ni Muagrgentina tayari amechagua jina la atakalo litumia katikakipindi chake cha Uongozi kuwa atatambulika kama Papa Francis.

Jopo la Makardinali wamemchagua Cardinali kutoka Latin America Cardinal Jorge Mario Bergoglio, kushika wadhifa mpya wa  Papa katika uchaguzi uliofanyika kwa mara ya tano kwa kura zilizopugwa na Makadinali 115 waliokuwa wakikutana katika kanisa la Sistine Chapel huko Vatican , Roma.

Maelfu ya watu walikuwa wamefurika katika eneo la la St. Peters huko Vatican huku mamilioni wengine wakishuhudia Papa huyo mpya akitangzawa mbele yao.

MOSHI MWEUPE ISHARA YA PAPA MPYA KUPATIKANA

White smoke appeared from the chimney above the Sistine Chapel, and bells from St. Peter's Basilica have pealed, meaning the 115 Roman Catholic cardinals gathered at the Vatican from all over the world have chosen a new pope.
The church's 266th pontiff will replace Benedict XVI, whose surprise resignation last month prompted the cardinals to initiate a conclave, a Latin phrase meaning "with a key," to pick a new leader for the world's almost 2 billion Catholics.

Although it's not immediately clear who received the necessary two-thirds vote, several candidates were mentioned as front runners, including what could be the first African pope or the first pope from the U.S. or Canada.

The new church leader takes over an organization many say is in crisis, from damaging allegations of internal squabbling to the cover-up and abetting of sexual abuse, though the latter issue came to light before Benedict's papacy.

Some sources say the Catholic Church in the U.S. has paid out as much as $3 billion to settle sexual abuse claims, though others estimate a billion less. At least eight U.S. Catholic dioceses declared bankruptcy protection. Benedict said in a 1998 U.S. visit that he was ashamed of the sex abuse scandal, and assured that the church would not allow pedophiles to become priests.

The Pope Emeritus also faced criticism for his role in overseeing the church's reaction to the sexual abuse crisis, as well as revelations from the "Vatileaks" incident. The pope's butler was implicated in the leaking of documents that included what Italian media first characterized as evidence of blackmail and disarray among church leaders regarding how to address growing concerns about money laundering.

Though Benedict basically dismissed those allegations as exaggerated, he remarked that the leaks and results of the ensuing investigation he commissioned had saddened him. Church outsiders have speculated that the results of Benedict's investigation may have led to his decision to resign from the papacy, a move unprecedented in six centuries.

The new pope will also face pressure to modernize the church on issues from reforming the clergy to allowing contraception. It's unclear if the cardinals will pick a pope who will change the church or a conservative leader who will remain dedicated to its current principals.

MZEE KINGUNGE ATAKA VIONGOZI KUENZI LUGHA YA KISWAHILI

 Mwanasiasa mkongwe Mzee Kingunge Ngombale Mwiru akisisitiza jambo wakati  uzinduzi wa kitabu historia ya Hayati Sheikh Kaluta Amri Abedi  katika hafla iliyofanyika leo kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dares Salaam.Kushoto ni Balozi Mstaafu Job Lusinde na kulia ni Brigedia Hashimu Mbita.
Baadhi wa wadau  wakifuatilia kwa makini  uzinduzi wa kitabu historia ya Hayati Sheikh Kaluta Amri Abedi  katika hafla iliyofanyika leo  kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dares Salaam.
Mwanasiasa mkongwe Mzee Kingunge Ngombale Mwiru akizindua kitabu historia ya Hayati Sheikh Kaluta Amri Abedi  katika hafla iliyofanyika leo  kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dares Salaam. Picha na Magreth Kinabo – Maelezo
*******************************************

NA: FRANK SHIJA & BENEDICT LIWENGA- MAELEZO

VIONGOZI wahimizwa MWANASIASA mkongwe Mzee Kingunge Ngombale Mwiru kuwataka viongozi nchini kukienzi na kuthamini lugha ya Kiswahili ili kuendelea kujenga taifa lenye umoja na mshikamano.

Kauli hiyo ilitolewa leo (jana) na Mzee Kingunge ambaye alikuwa  mgeni ramsi katika hafla ya uzinduzi wa Kitabu cha Historia ya Hayati Sheikh Kaluta Amri Abedi iliyofanyika kwenye ukumbi wa Karimjee,  jijini Dar es Salaam .

“Hatima ya Taifa inategemea lugha ya Kiswahili. Viongozi wanawajibu mkubwa katika kuhakikisha kuwa lugha ya Kiswahili inakuwa kwani wao ndio wanaweza kukipandisha au kuiua lugha ya Kiswahili kwakuwa jamii inawategemea kwa kiasi kikubwa,” alisema Mzee Kingunge.

Aidha  Mzee Kingunge anawaasa kuwa wazalendo na kutumia lugha ya hiyo kwa ufasaha tofauti na ilivyo sasa katika shughuli mbalimbali mfano Bungeni.

Hata hivyo, aliunga mkono  lugha hiyo kuwa rasmi kufundishia, lakini ametoa changamoto kuwa yatupasa kuwa makini katika kuitumia hususani katika ngazi elimu ya msingi, sekondari hadi vyuo vikuu.

Mzee Kingunge alitolea mfano wa wajukuu zake kuwa masomo mengine kama vile hesabati wanapata  alama 90 hadi 95,lakini lugha hiyo wanapata alama ya 60 mpaka 70. Hivyo inaelekea ufundishaji wake ni tatizo.

“Kama kufundisha lugha ya Kiswahili katika elimu ya sekondari ni tatizo na Kiingereza ni tatizo . Kiswahili kipi kifundishwe katika elimu ya Chuo Kikuu,”alisema. Huku akitolea mfano kuwa kumekuwa na matumizi ya maneno ambayo si sahihi kama vile neno masaa badala ya saa.

Kwa upande wake mwanazuoni na mdau wa lugha hiyo  Profesa Mugyabuso Mulokozi na  Profesa Joshua Madumula wameiomba serikali kuwa na utaratibu wa kuenzi   fasihi za Watanzania.

GODBLESS LEMA AITISHA MAANDAMANO

Lema aitisha maandamano
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema, ametangaza kuandaa maandamano makubwa yatakayoshirikisha wanawake na watoto katika Jiji la Arusha ili kushinikiza Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Arusha (AUWSA) kuwasambazia maji.

Akizungumza jana, Lema alisema ameamua kuandaa maandamano hayo ya kudai maji kwani kwa zaidi ya miezi sita sasa asilimia 70 ya wakazi wa Jiji la Arusha hawapati maji safi.
“Nimewaandikia barua AUWSA wiki mbili sasa nikiwataka wanipe mipango yao ya muda mfupi na mrefu ya kuondoa tatizo la maji Arusha, kwani mimi kama mbunge ninaweza kushirikiana nao kupunguza tatizo hili, lakini hawajajibu sasa tutawashinikiza kwa nguvu wa umma,” alisema Lema.
Hata hivyo, Mkurugenzi Mkuu wa AUWSA, Mhandisi Ruth Koya hakupatikana kuelezea kama amepokea barua hiyo baada ya kutopatikana ofisini, pia simu yake ya mkononi ilikuwa haipatikani.

MAPOZI" YA LULU MICHAEL AKIWA KITAA.


Lulu back to basics how sweet

MUONEKANO MPYA WA WEMA SEPETU BAADA YA KUZITIA MKASI NYWELE ZAKE



Mrembo na Miss Tanzania wa zamani, Wema Sepetu ameamua kubaki natural baada ya kuzinyoa nywele zake. Kupitia Instagram, Wema ameshare picha hizo na kuandika, ‘me apa nimenyoa nywele’. Ingia ndani kusoma maoni aliyoyapata baada ya kunyoa.

Mh. Pinda kubariki Tamasha la Pasaka jijini Dar

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye Tamasha la Pasaka Machi 31 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Taarifa kwa vyombo vya habari, iliyotolewa jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama ilieleza kuwa tayari Ofisi ya Waziri Mkuu imeshathibitisha kuhusiana na ujio wake kwenye tamasha hilo.

“Tunafurahi kwamba tamasha letu mwaka huu Dar es Salaam mgeni rasmi atakuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, mwaka jana alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Benard Membe,” ilisema taarifa hiyo ya Msama.

Waimbaji mbalimbali wa ndani na nje ya Tanzania wanatarajiwa kutumbuiza kwenye tamasha hilo, ambapo wan je ya nchi ni Sipho Makhabane wa Afrika Kusini, Ephraim Sekeleti wa Zambia na Solomon Mukubwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) anayeishi Kenya, pamoja na kwaya ya Ambassadors of Christ ya Kigali Rwanda.

Kwa upande wa wasanii wa hapa nchini watakaotumbuiza ni Upendo Kilahiro, Rose Muhando, Upendo Nkone na John Lissu, kwaya ya Kinondoni Revival na kundi la Glorious Celebration.

Tamasha la Pasaka litafanyika Dar es Salaam Machi 31 na litaendelea Aprili mosi kwenye Uwanja wa Sokoine Mbeya, wakati Aprili 3 ni Uwanja wa Samora Iringa na Aprili 6 Uwanja wa Jamhuri, Dodoma na siku inayofuata itakuwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza. 
 
 

Mbunge wa Bumbuli-CCM na Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia January Makamba Aula World Economic Forum(WEF) Young Global Leader 2013



MOSHI MWEUSI WAFUKA VATICAN KUASHIRIA KUWA BADO PAPA HAJAPATIKANA....


Moshi mweusi ulifuka jana jioni kutoka kwenye  dohani huko Vatican ikiwa ni ishara kwamba Baraza la siri la Makadinali bado halijampata Kiongozi mpya wa Kanisa Katoliki baada ya kupiga kura ya kwanza.

Mchakato wa kupiga kura ulianza mapema jana  ambapo Makadinali 115 kutoka nchi 48 walikutana kwa faragha ili kumchagua atakaechukua nafasi ya aliyekuwa papa Benedikt wa 16 aliejiuzulu mwishoni mwa mwezi uliopita. 

Zoezi la kupiga kura litaendelea hadi hapo mmoja wa Makadinali atakapopigiwa theluthi mbili ya kura yaani kura 77.

Atakaefikia kiwango hicho atakuwa Baba Mtakatifu wa 266.

Ikiwa Makadinali, wanaopiga kura watakubaliana juu ya Kiongozi mpya wa Kanisa Katoliki, moshi  mweupe utatoka dohani na kengele zitapigwa kwenye makao makuu ya Kanisa Katoliki, Vatican.

Mama Salma Kikwete akitaka kituo cha utamaduni cha Bujora kuhifadhi utamaduni wa mtanzania.


Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amekipongeza kituo cha utamaduni cha Bujora kwa kutunza na kuhifadhi  utamaduni wa mtanzania unaolitambulisha kabila la wasukuma jambo litakalosaidia kizazi kijacho kuweza kujifunza utamaduni huo.
Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na  Maendeleo (WAMA) ametoa pongezi hizo hivi karibuni alipokitembelea kituo hicho kilichopo wilayani Magu katika mkoa wa Mwanza.
Amesema kuwa kituo hicho kimeonyesha mfano wa kuigwa kwani amejionea na kujifunza mambo mbalimbali ambayo hakuwa anayafahamu hapo awali kuhusiana na kabila hilo jambo la muhimu wahakikishe kuwa wanaendelea kutunza utamaduni wao.
Akisoma taarifa ya kituo hicho Padre Fabian Mhoja ambaye ni Mkurugezi amesema kuwa kituo kilianza mwaka 1954  kikiwa na lengo la kuhifadhi na kuendeleza tunu bora ya maisha ya watu ili waweze kumfahamu Mungu na kuishi kadiri ya mpango wake kwa kutumia utamaduni.
Amesema kuwa wanajihusisha  na shughuli za kutunza  na kuendeleza urithi wa utamaduni wa mtanzania kwani kupitia kituo hicho wameweza kutangaza utalii na utamaduni ndani na nje ya nchi kupitia ngoma , nyimbo na michezo mbalimbali.
Kituo hicho kimekuwa kikiandaa tamasha la Bulabo ambapo Rais Dk. Jakaya  Mrisho Kikwete amekuwa akichangia ufanikishaji wa tamasha hilo ambalo hufanyika kila mwaka na kukusanya watu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi.

Mchakato wa kumpata Papa mpya huko Vatican bado hakijaeleweka makadinali leo waingia siku ya pili ya kupiga kura.


Moshi mweusi ulifuka jana jioni kutoka kwenye  dohani huko Vatican ikiwa ni ishara kwamba Baraza la siri la Makadinali bado halijampata Kiongozi mpya wa Kanisa Katoliki baada ya kupiga kura ya kwanza.
Mchakato wa kupiga kura ulianza mapema jana  ambapo Makadinali 115 kutoka nchi 48 walikutana kwa faragha ili kumchagua atakaechukua nafasi ya aliyekuwa papa Benedikt wa 16 aliejiuzulu mwishoni mwa mwezi uliopita.
Zoezi la kupiga kura litaendelea hadi hapo mmoja wa Makadinali atakapopigiwa theluthi mbili ya kura yaani kura 77.
Atakaefikia kiwango hicho atakuwa Baba Mtakatifu wa 266.
Ikiwa Makadinali, wanaopiga kura watakubaliana juu ya Kiongozi mpya wa Kanisa Katoliki, moshi  mweupe utatoka dohani na kengele zitapigwa kwenye makao makuu ya Kanisa Katoliki, Vatican. 

WASTARA AAGWA.............!!!!!


WASTARA Juma amabaye ni mke wa marehemu Juma Kilowoko “Sajuki” Jumpili jioni alisindikizwa na ndugu na jamaa katika uwanja wa ndege wa Kimataita wa Mwalimu Nyerere katika safari yake ya kuelekea Oman.
Wastara ambaye amekwenda Oman kwaajili ya mapumziko ya miezi miwili ikiwa ni pamoja na kumaliza eda ya mumewe alipelekea huzuni nyingi kwa watu waliomsindikiza kuanzia nyumbani hadi Airpot.
Zifuatazo ni picha mbali zilizopigwa nyumbani, barabarani na uwanja wa ndege zikimuonyesha Wastara katika pilika za safari hiyo.

KOCHA WA TAIFA STAR ATAJA TIMU YA KUIVAA MOROCCO



Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametaja wachezaji 23 watakaoingia kambini Jumamosi (Machi 16 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mechi ya mashindano dhidi ya Morocco.

Mechi hiyo ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Brazil itachezwa Machi 24 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Kocha Kim, wachezaji wa Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager wanatakiwa kuripoti kambini katika hoteli ya Tansoma, Machi 17 mwaka huu.

Wachezaji walioitwa ni makipa Juma Kaseja kutoka Simba ambaye pia ndiye nahodha wa Stars, Aishi Manula (Azam), Hussein Shariff (Mtibwa Sugar) na Mwadini Ally (Azam). Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Issa Rashid (Mtibwa Sugar), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Nassoro Masoud Cholo (Simba) na Shomari Kapombe (Simba).

Viungo ni Salum Abubakar (Azam), Athuman Idd (Yanga), Amri Kiemba (Simba), Khamis Mcha (Azam), Frank Domayo (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Simba) na Shabani Nditi (Mtibwa Sugar).

Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Mrisho Ngasa (Simba), Simon Msuva (Yanga), na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).

Mbali ya Kim, benchi la ufundi la Taifa Stars linaundwa na Sylvester Marsh (Kocha Msaidizi), Juma Pondamali (Kocha wa makipa), Leopold Tasso (Meneja), Dk. Mwanandi Mwankemwa (Daktari wa timu), Frank Mhonda (Mtaalamu wa tibamaungo) na Alfred Chimela (Mtunza vifaa).

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...