Friday, October 10, 2014

MAMBO HAYA: MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI AMTUNDIKA MIMBA MWALIMU WAKE....!!!


Hii ni moja ya picha mbalimbali za wajawazito kama inavyonekani siyo ya mwalimu muhusika kwa tukio hilo.

WAKATI ikiwa imezoeleka kuwa baadhi ya walimu wa kiume huwarubuni wanafunzi wao wa kike na hata kuwaharibia kabisa ndoto zao za kielimu kutokana na kuwapa ujauzito, hali imekuwa tofauti mkoani Rukwa ambako mwanafunzi wa Kidato cha Pili anadaiwa kumzalisha mwalimu wake.

Mwanafunzi huyo aliyemzalisha mwalimu wake ana umri wa miaka 17, wakati mwalimu huyo anayefundisha katika Shule ya Sekondari ya Umma ya Nkasi, iliyopo mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Nkasi, Rukwa, ana umri wa miaka 25.

Tukio hilo linalotajwa kuwa la kwanza kutokea wilayani hapa, limekuwa gumzo kubwa kwa wakazi wa Nkasi na wilaya jirani.

Hata hivyo, kwa wanafunzi, wamekuwa wakimpongeza mwenzao kwa kujaliwa kupata mtoto katika umri wake huo mdogo, huku mzazi mwenzake akiwa na uhakika wa maisha kutokana na kuwa ni mtumishi serikalini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

NEC: HAKUNA KURA YA MAONI BILA DAFTARI JIPYA




Rais Jakaya Kikwete akipokea Katiba Inayopendekezwa kutoka kwa Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta wakati wa hafla iliyofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma juzi. Katikati ni Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein. 


Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema haitaendesha uchaguzi wa aina yoyote, wala kuitisha kura ya maoni hadi kazi ya kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura itakapokamilika.

Kauli ya NEC imekuja siku moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kukabidhiwa Katiba inayopendekezwa na Mwenyekiti wa lililokuwa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta na kulitaja suala la uboreshaji wa daftari la hilo kama mambo matatu yanayoiweka kura ya maoni kupitisha Katiba hiyo njiapanda.

Mambo mengine ni Sheria inayotaka kura hiyo ipigwe ndani ya siku 84 baada ya Katiba inayopendekezwa kuchapishwa na kufanyiwa marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.

Mwenyekiti wa NEC, Jaji Damian Lubuva alisema jana kwamba kuendesha uchaguzi bila kuboresha daftari hilo ni kuongeza malalamiko kwa wananchi na wadau, hususan vyama vya siasa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WASHUKIWA 7 WA UCHAWI WAUAWA KIGOMA



Moja ya nyumba zilizoteketezwa katika Kijiji cha Murufiti ambapo watu saba waliuawa kwa kuchomwa moto.

Kigoma. Watu saba wameuawa kwa kuchomwa moto ndani ya nyumba katika tukio ambalo nyumba 18 ziliteketezwa na mbili kubomolewa na wananchi waliodai wanawaua wachawi katika Kijiji cha Murufiti, Kasulu, mkoani Kigoma.
Polisi wameeleza kuwa tayari watu 17 wamekamatwa kwa kuhusika kwenye tukio hilo.
Miongoni mwa waliouawa katika tukio hilo lililotokea Jumatatu iliyopita ni John Mavumba (68) na mkewe Elizabeth Kaje 55 ambao pamoja na wenzao walikuwa wakituhumiwa kuwa ni washirikina. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 10, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RAIS MUSEVEN AKATAA WATU KUSALIMIANA....!!!

shaking hands 
October 9 2014 nchi ya Uganda iliazimisha uhuru wake huku rais wake Yower Museven akizungumza mambo muhimu matatu kwa wananchi wake ambapo ishu ya kwanza ni kuwataka wananchi wake kuwa makini kutokana na tishio la magonjwa ya Marburg pamoja na Ebola hivyo waache kusalimiana kwa kushikana mikono pamoja na kukumbatiana bila kuwepo ulazima wa kufanya hivyo.
Alisema magonjwa hayo kwa sasa yameonekana kuchukua nafasi kubwa duniani na amewataka kuwa makini zaidi ili yasizidi kusambaa lakini pia kumekuwa na utamaduni wa baadhi ya watu hasa wanaoishi maeneo yenye misitu kula nyama za nyani ambazo magonjwa hayo yanaaminika kuanzia huko, nao pia amewataka waache ili haya magonjwa ya ajabu yasije kwa binadamu.
Kitu kingine ambacho rais huyo alizungumza ni kitendo cha mabosi wa mahakama ya The Hague  ya Uholanzi kumtaka rais mwenzake wa Kenya, Uhuru Kenyatta kuhudhuria kikao cha kujibu tuhuma dhidi yake kuhusiana na ghasia zilizotokea nchini kwake na kusema kililenga kudharau na kusitisha mkutano uliofanyika juzi nchini kwake.
Alisema pamoja na Serikali ya nchi hiyo kuomba rais Kenyatta kuhudhuria mkutano huo muhimu lakini mahakama hiyo ilionekana kukataa na kulazimisha ahudhurie katika kesi hiyo.
Hata hivyo Kenyatta alikanusha tuhuma za yeye kuhusika na ghasia zilizosababisha kupoteza maisha ya zaidi ya watu 1200 huku wengine zaidi ya laki sita wakikosa mahali pa kukaa mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu na jambo la mwisho alilozungumzia ni kuhusu timu ya Taifa ilo ambalo inakabiliwa na mchezo dhidi ya Togo ambapo aliwatakia kila la Kheri. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ENGLAND YASHINDA TENA, ROONEY BADO BAO MOJA AVUNJE REKODI YA CHARLTON

article-2786987-22162C8600000578-875_964x386
Mshambulizi wa England, Wayne Rooney anahitaji kufunga bao moja tu ili kufikia rekodi ya ufungaji mabao ‘ wa muda wote’ katika kikosi cha ‘ The Three Lions’. Mshambulizi wa zamani wa ‘ Simba Watatu’ Gwiji Sir Bobby Charlton alifunga mabao 49 rekodimbayo haijapata kufikiwa. Miaka lifunga moja yakumi iliyopita, Michael Owen alionekana kama mchezaji ambaye angeifikia rekodi hiyo lakini majeraha yalimfanya kuwa nyuma kwa tofauti ya mabao tisa.
Nahodha wa England, Rooney ‘ Baba Kai’ alifunga moja ya mabao matano ya England usiku wa kuamkia leo wakati England ilipochomoza na ushindi wa kishindo dhidi ya San Marino katika uwanja wa Wembley. Mlinzi wa kati, Phill Jargierka alifunga bao la kuongoza dakika ya 24 kabla ya Rooney kufun ga bao la 48 kwa England kwa mkwaju wa penalti.
Danny Welbeck alifunga bao lake la Tatu katika michezo miwili ya England mara baada ya kuanza kwa kipindi cha pili, Andros Townsend alifunga bao la nne dakika ya 72, kabla ya wageni kujifunga bao la tano kupitia kwa Alessandro Della Valle dakika tano baada ya bao la Townsend. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...