Friday, August 30, 2013

MAGAZETI YA LEO IJUMAA AGOSTI 30, 2013


DSC 0078 77901
DSC 0079 4f4bd
DSC 0080 cea9f
DSC 0081 8f173

DIAMOND AMKABIDHI MZEE NGURUMO GARI AINA YA FUNCARGO

DIAMOND SHOW 020-1 8998c
Msanii Diamond Platnum amefanya kufuru usiku huu kwa kutoa zawadi ya Gari kwa Mzee Ngurumo Mwanamziki wa miaka mingi na mkongwe nchini aliyestaafu majuzi kufanya kazi za mziiki.
Tukio hilo limetokea usiku huu ndani ya ukumbi wa SERNA HOTELkatikati ja jiji la DSM ambapo Diamond Platnum anazindua video yake ya wimbo wa #one fun.
DIAMOND SHOW 025 b03d6
Mzee Ngurumo amesema"Haamini macho na masikio yake,hanachakusema zaidi ya ASANTE kwa msanii huyo"Lakini pia amesema hajui hata mke wake atasemaje baada ya kumwona akiingia na gari ndani ya nyumba yake.
Mzee ngurumo amekuwa na matatizo ya kiafya siku za karibuni nakupelea kustaafu mziki kabisa.Wazee wa msondongoma ndio wanajua makali ya Mzee Ngurumo.

"KAJALA NDIO KILA KITU KWANGU KWA SASA, YEYE NI ZAIDI YA MUME KWANGU"......WEMA


KASUMBA ya wanawake wengi kuwaambia mashoga zao siri zao nzito inadaiwa kumfanya msanii maarufu wa filamu Bongo, Wema Sepetu kufunguka kuwa, bila kuwa karibu na Kajala Masanja itakuwa ni kama kuamua kutembea mtupu.
Wema Sepetu na Kajala Masanja.
Wema alifikia hatua ya kutoa maneno hayo katikati ya wiki hii kwa kuposti picha kwenye mtandao wa Instagram ikimuonesha yeye, meneja wake Martin Kadinda na Kajala huku akisindikiza na ujumbe mzito uliosomeka:
“I always call my poch and I fell so naked without, I need her everywhere with me. I hope that’s how they out each other.”
Aliandika kimombo, alimaanisha nini?

Tafsiri ya maneno hayo ni kwamba, Wema anamchukulia Kajala kama pochi yake na bila yeye anajihisi yuko uchi kiasi kwamba anataka kila sehemu wawe wote.
Kajala amjibu
Baada ya Wema kutundika ujumbe huo, Kajala naye alijitutumua na kutupia maneno ya kumshukuru (Wema) huku akieleza kuwa, kama ni hivyo yeye hana la kusema.
Nimeyapenda maneno hayo, kama ni hivyo mimi sina la kusema,” aliandika Kajala kwenye mtandao huo.


Kwa nini Wema aseme hivyo?

Yawezekana Wema alimaanisha vingine lakini wachambuzi wa mambo wamekuwa na maoni yao huku wengi wakieleza kuwa, inawezekana Wema anasema hivyo kutokana na ukweli kwamba Kalaja anajua siri zake nyingi.

KATIBA YATAKIWA IRUHUSU WAFUNGWA KUSHIRIKI TENDO LA NDOA NA WENZA WAO ILI KUPUNGUZA USAGAJI NA USHOGA GEREZANI

BAADHI ya wadau wa masuala ya jinsia wamependekeza kuwa ili kukabiliana na masuala ya ushoga na usagaji, Katiba Mpya iruhusu wafungwa kukutana kimwili na wenza wao, kwani vitendo hivyo chanzo chake ni gerezani hasa kwa vijana wanaokula 'unga' na kuvuta bangi.




Hayo yalisemwa juzi kwenye kikao cha maboresho ya Rasimu ya Katiba Mpya, kilichofanyika siku tatu kwenye Kijiji cha Makaburini kwa kuratibiwa na asasi ya Tanzania Environment Relatives Organization (TERO) ya mjini Korogwe kwa ufadhili ya Shirika la The Foundation for Civil Society la jijini Dar es Salaam. 

"Mfungwa akubaliwe kukutana kimwili na mume au mke wake. Kitendo cha kuwakatalia wafungwa kukutana kimwili na wake au waume zao kunachochea vitendo vya kufanya mapenzi ya jinsia moja na vijana wengi wameharibikia gerezani na kujikuta vitendo hivyo vinaingia mitaani"

RAIS KIKWETE AMUOMBA RAIS WA UGANDA AONGEE NA KAGAME ILI KUMALIZA UGOMVI ULIOPO


RAIS Jakaya Kikwete, amewasiliana na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, ili azungumze na Rais wa Rwanda, Paul Kagame kwa nia ya kumaliza mvutano wa maneno kati yao kwa busara.
 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisema hayo jana bungeni, alipokuwa akijibu swali la Kiongozi wa Upinzani bungeni, Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe (Chadema).
 
“Tunataka suala hili limalizike kwa njia ya busara, ili watu waendelee kuchapa kazi, ninaamini busara zitatumika kumaliza tatizo hilo,” alisema.

Akiuliza swali katika kipindi cha maswali ya Papo kwa Hapo kwa Waziri Mkuu jana, Mbowe alitaka kujua kauli ya Serikali na mikakati iliyopo kupata suluhu katika mvutano wa maneno uliojitokeza kati ya Rais Kikwete na Rais Kagame.
 
Pia Mbowe alitaka Serikali kuunda jopo la ushawishi wa kimataifa, kutokana na Rwanda kuonekana kushawishi nchi za Uganda na Kenya, jambo ambalo linaashiria kuitenga Tanzania katika shughuli mbalimbali za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
 
Kwa mujibu wa Mbowe, kitendo cha marais wa Kenya, Uganda na Rwanda kukutana katika mikakati ya kuanza kutumia bandari ya Mombasa ambayo ingekuwa ya nchi za Afrika Mashariki, ni dalili kuwa Tanzania imeanza kutengwa.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...