Thursday, December 04, 2014

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS DESEMBA 04, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

2014 NI MWAKA WA JOTO KALI DUNIANI

Viwanda vikitoa moshi angani na kuchafua mazingira
Mwaka huu unaoishia unasemekana kuwa na kiwango cha juu zaidi cha joto duniani na kwa Uingereza tangu kumbukumbu zianze kutunzwa.
Makadirio ya awali yanaonyesha kuwa katika miezi kumi ya kwanza ya mwaka 2014, wastani wa kiwango cha hali ya joto duniani kilikuwa 0.57C juu ya wastani uliokuwepo muda mrefu.
Dhoruba nchini Uingereza iliyosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi
Na miezi kumi na mmoja ya kwanza nchini Uingereza imezalisha wastani wa joto la 1.6C likiwa juu ya wastani uliokuwepo kwa muda mrefu.Utafiti mwingine uliofanywa na Ofisi ya Hali ya Hewa ya Uingereza umeonyesha kuwa ongezeko la viwango vya joto vilivyoshuhudiwa, visingetokea bila ya ongezeko la gesi zinazoharibu mazingira kutokana na shughuli za binadamu. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

IS WAFUNGUA KAMBI ZA MAFUNZO LIBYA

 Wapiganaji wa Islamic State katika jimbo la Anbar,Syria Marchi 2014 
Wapiganaji wa kundi la Islamic State wafungua kambi za mafunzo Libya
Wapiganaji wa kundi la Islamic State wameanzisha kambi za mafunzo mashariki mwa Libya, amesema mkuu wa kamandi ya Marekani ya masuala ya Afrika.
Wapiganaji wa Kikurd wakiwa katika mafunzo ya kijeshi kukabiliana na wapiganaji wa Islamic State Septemba 2014 nchini Iraq.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

AFCON 2015 MAKUNDI YA TIMU 16 YATAJWA

Kombe la Shirikisho la Soka Afrika, AFCON 
 
Upangaji wa makundi ya timu kumi na sita zilizofuzu kucheza fainali za mashindano ya 30 ya kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2015 yamefanyika katika mji mkuu wa Equatorial Guinea, Malabo.
Mashindano hayo yataanza Januari 17, 2015.
Upangaji wa makundi ulirudishwa wiki moja nyuma ili kuiwezesha Equatorial Guinea, kujiandaa baada ya kuchukua nafasi ya Morocco, iliyokuwa iandae mashindano hayo, lakini ilishindwa kufanya hivyo baada ya kutaka mashindano hayo yasogezwe mbele kuhofia ugonjwa wa Ebola ambao umeyakumba baadhi ya mataifa ya Afrika Magharibi, ambako zinatoka timu nyingi zinazoshiriki michuano hiyo.
Mabingwa watetezi Nigeria ni moja ya timu kubwa zilizoshindwa kufuzu kucheza fainali za mwakani, pamoja na Misri na Angola ambazo zote kwa mshangao hazitaweza kushiriki.
Haya hapa makundi manne ya AFCON 2015:

Kundi A Equatorial Guinea, Burkina Faso, Gabon, Congo
Kundi B Zambia, Tunisia, Cape Verde, DR Congo
Kundi C Ghana, Algeria, South Africa, Senegal
Kundi D Ivory Coast, Mali, Cameroon, Guinea

Wenyeji Equatorial Guinea na Congo zitacheza mechi ya ufunguzi wa michuano hiyo. Kundi D ndilo linaloonekana kuwa gumu zaidi kutokana na timu zilizopangwa kundi hilo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

CHELSEA HAISHIKIKI LIGI KUU ENGLAND

Ivanovic akishangilia na Drogba baada ya Drogba kuifungia timu yake ya Chelsea bao la pili katika mechi hiyo 

Mzunguko wa 14 umekamilika kwa timu zote 20 za ligi kuu ya England kushuka viwanjani.
Chelsea, wameendeleza wimbi la ushindi na kukataa katakata kuzipa nafasi timu nyingine 19 kupunguza pengo la pointi lililopo kati yake na timu hizo.

Sergio Aguero, mchezaji wa Manchester City akishangilia moja ya magoli yake katika ligi kuu ya England
Chelsea imeendelea kuwa na tofauti ya pointi sita na Man City inayoifuatia baada ya kuirarua Tottenham mabao 3-0, huku Manchester City yenye pointi 30 ikiisasambua Sunderland magoli 4-1. Sergio Aguero ameifungia timu yake ya Manchester City magoli mawili katika mchezo huo, huku Jovetic na Zabaleta kila mmoja akifunga bao moja. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...