Friday, September 05, 2014

TAZAMA PICHA ZA AJALI ILIYOTOKEA MUSOMA NA KUUA WATU ZAIDI YA 40

 Basi la Kampuni ya J4 EXPRESS lenye nambari za usajili T 677 CYC lililokuwa likitoka Musoma kuelekea Silari Mkoani Mara likiwa limeumia vibaya sana baada ya kugongana uso kwa uso na Basi lingine la Kampuni ya MWANZA COACH lenye nambari za usajili T 736 AWJ katika eneo la SabaSaba, Mjini Musoma mchana wa leo.
Watu zaidi ya 40 wamepoteza maisha papo hapo na wengine kujeruhiwa vibaya kwa mujibu wa Ripota wetu aliopo eneo la tukio, ilielezwa kuwa chanzo cha ajali hiyo ni Basi la J4 ambalo lilikuwa likijaribu kuipita gari ndogo aina ya Nissan Terano lenye nambari za usajili T 332 AKK katika sehemu ambayo mbele kuna daraja linaloweza kupitisha gari moja kwa wakati huo, kutokana na kuwa basi hilo lilikuwa kwenye mwendo kasi liliweza kuisukuma kwa ubavuni gari hiyo ndogo ambayo haikuweza kuhimili nguvu ya Basi hilo na kutoka kwenye njia na kwenda kuingia mtoni hali iliyoipelekea dereva wa basi hilo kuamini kuwa atawahi kupita katika daraja hilo bila kufahamu kuwa Basi lingine linalokuja mbele nalo liko kwenye mwendo kasi huku nalo likitaka kuwahi kupita kwenye daraja hilo. Ndani ya gari hiyo ndogo kulikuwa na watu watatu, ambapo wawili wamefariki na mmoja amejeruhiwa.
Basi la Kampuni ya MWANZA COACH lililokuwa likitokea Musoma kwenda Mwanza linavyoonekana baada ya kugongana uso kwa uso na Basi la Kampuni ya J4 EXPRESS.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz 

BUNGE LA KATIBA LAKATAA ELIMU YA KIDATO CHA NNE KWA WABUNGE


Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Pandu Amir Kificho (kulia) akiwaeleza jambo wajumbe wa bunge hilo walipohudhuria kikao cha 32 cha Bunge mjini Dodoma jana.

Pendekezo la Rasimu ya Katiba kuwa wabunge walau wawe na elimu ya kidato cha nne limetupiliwa mbali na wajumbe wa Bunge Maalumu, baada ya Kamati karibu zote kulikataa.
Kamati hizo zimependekeza kigezo cha elimu kuanzia walau kidato cha nne kama sharti muhimu la mtu anayetaka kugombea Ubunge kiondolewe, badala yake mgombea ama ajue tu kusoma na kuandika, au ajue kusoma na kuandika Lugha ya Kiswahili au Kiingereza kama ilivyo kwenye Katiba ya sasa.Mbali na pendekezo hilo, kamati hizo zimegawanyika kuhusu Ibara ya 129 ya Rasimu ya Katiba inayowapa wananchi nguvu ya kumuondoa mbunge wao madarakani kabla ya miaka mitano kumalizika.
Hayo yalijitokeza bungeni Dodoma jana, wakati kamati hizo zikiwasilisha taarifa zake kuhusu Sura ya 9 na 10 ya Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa bungeni na Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

NISHA AZUA TAHARUKI HEKALU LA FREEMASON...!!!


STAA wa sinema za Kibongo, Salma Jabu 'Nisha', Jumanne iliyopita alijikuta akizua taharuki kufuatia kuegesha gari lake nje ya Hekalu la Freemason lililopo nyuma ya Hyatt Regency Dar es Salaam The Kilimanjaro Hotel jijini Dar es Salaam.


Staa wa sinema za Kibongo, Salma Jabu 'Nisha'.

Taharuki hiyo ilikuja pale Nisha alipoegesha gari lake eneo hilo na kushuka kisha wanafunzi na watu wengine kusitisha shughuli na kumzunguka kutaka kujua kulikoni staa huyo kufika eneo hilo linaloaminika kuwa kila anayekwenda ni muumini wa imani ya Freemason.

Baadhi ya watu walimuuliza Nisha alichofuata kwenye hekalu hilo huku mwenyewe akishindwa kujibu kwani alitupiwa maswali mfululizo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

DIAMOND AELEZA JINSI ALIVYODHALILISHWA UJERUMANI


SIKU chache baada ya kufanyiwa fujo katika shoo yake nchini Ujerumani, staa wa Mdogo Mdogo, Nasibu Abdul ‘Diamond’ ameibuka na kueleza namna ambavyo alidhalilishwa nchini humo.
Diamond aliponea chupuchupu kupewa kipigo baada ya kuchelewa kwenye shoo iliyokuwa ifanyike katika Ukumbi wa Sindelfingen katika mji wa Stuttgart, Ujerumani.
Staa wa Mdogo Mdogo, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Akizungumza na paparazi wetu baada ya kutua Bongo Jumanne iliyopita, Diamond alisema anasikitika kwani alidhalilishwa wakati alipokuwa akidai haki ya kumaliziwa malipo yake ya shoo euro 250 (zaidi ya sh 500,000). Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SULUHU: HUYU NDIYE SHIBUDA ORIJINO

Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samia Suluhu.

WAKATI Mbunge wa Bariadi Magharibi (Chadema), John Shibuda akiwasilisha maoni ya wachache ya Kamati namba 8 ya Bunge Maalum la Katiba linaloendelea na vikao vyake mjini Dodoma Jumatano mchana, Makamu Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samia Suluhu alimsifu na kusema kuwa mwakilishi huyo wa wananchi ndiye orijino, ukimuona mwingine ni photokopi.
Shibuda aliyeingia katika ukumbi huo akipingana na msimamo wa chama chake kilichoamua kususia vikao hivyo kwa kushirikiana na vyama vya CUF na NCCR-Mageuzi, alitumia pia nafasi hiyo kuwapiga vijembe viongozi wake, akisema hana matatizo na Chadema, isipokuwa ana ‘bifu’ na mfumo wa utumishi wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini.
Akifafanua kauli yake hiyo, Shibuda anayefahamika kwa mbwembwe na mikogo ya lugha, alisema yeye ni kama mchezaji wa mpira aliye staa, akiwatolea mfano Cristiano Ronaldo na Lionel Messi, ambao wanaponunuliwa na timu yoyote, huenda kwa ajili ya kuiimarisha na si vinginevyo.
Mbunge wa Bariadi Magharibi (Chadema), John Shibuda.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 05, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MCHEKESHAJI MAARUFU DUNIANI 'JOAN RIVERS' AFARIKI


Enzi za uhai wake Joan Rivers
Mchekeshaji maarufu nchini Marekani Joan Rivers amefariki dunia akiwa na umri wa miaka themanini na na mmoja.
Joan alikua amelazwa katika hospitali moja mjini New York kwa wiki kadhaa sasa akisumbuliwa na maradhi ya moyo.
Melissa binti wa Joan,Akitangaza juu ya kifo cha mamake alimuelezea mama yake kua maishani mwake alikua akipenda kuona watu wana tabasamu usoni ama vicheko.
Joan River alianza shughuli zake za ucheshi kama muigizaji wa kawaida tu nusu karne iliyopita, na anatajwa kua mwanamke maarufu na bora katika ucheshi jukwaani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAJANGA: BOKO HARAM WAZUIA WATU KUZIKA MAITI...!!!

Wapiganaji wa Boko Haram wamesababisha maafa Kaskazini ya Nigeria ngome yao ya vita
Taarifa za kutisha zimeibuka kutoka mjini Bama moja ya miji ambayo ilitekwa na wapiganaji wa kiisilamu wa Boko Haram Kaskazini Mashariki ya Nigeria
Seneta mmoja wa eneo hilo,Ahmed Zanna, aliambia BBC kwamba wakazi hawaruhusiwi kuwazika jamaa wao waliouawa na wapiganaji hao.

Inaarifiwa miili imetapakaa katika barabara za mji huo ambao Boko Haram imeuteka.
Kundi hilo linasemekana kuuteka mji huo huku wapiganaji wa kundi hilo wakishika doria katika barabara zake.
Maelfu ya watu wametoroka huku idadi kubwa ya wengine wakiuawa.
Seneta huyo ameitaka serikali ya Nigeria kupeleka wanajeshi mjini Maiduguri ambao ni mji mkuu wa jimbo hilo ili kuulinda dhidi ya wapiganaji hao.
Mnamo siku ya Jumatano serikali ya jimbo hilo ilikanusha madai kuwa jimbo hilo limetekwa na wapiganaji hao.
Maafisa wakuu wanakisia kuwa watu 26,000 wameachwa bila makao kutfuatia mapigano katika mji wa Bama.
Bwana Zanna anasema kuwa barabara za mji huo zimejaa miili ya watu na Boko Harama imewakata wakazi kuwazika jamaa wao. ''Kwa hivyo hali ni mbaya na inaendelea kuzorota,'' asema bwana zANNA
Boko Haram wameteka miji kadhaa Kaskazini Mashariki ya Nigeria, katika miezi ya hivi karibuni na kusababisha hofu kuwa huenda wakaufikia mji mkuu Maiduguri.
Bwana Zanna amesema kuwa itakuwa janga kubwa ikiwa Boko Haram wataushambulia mji wa Maidiguri ambao una watu zaidi ya milioni mbili. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WATOTOMILIONI 120 WAFANYIWA UKATILI DUNIANI

Mtoto akijilia nyama
Umoja wa mataifa umetoa kauli kwamba wasichana zaidi ya milioni 120 duniani kote,sawa na msichana mmoja kati ya kumi atakua amaebakwa ama amewahi kufanyiwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kabla hajatimiza umri wa miaka 20.
Kitengo cha umoja wa mataifa kinachoshughulikia masuala ya watoto UNICEF kimegundua mnamo mwaka 2012 pekee watoto na mabinti wapatao elfu tisini na watano waliuawa,wengi wao ni kutoka Marekani kusini na Caribbean.
Ripoti hiyo ya UNICEF iliangazia nchi zipatazo mia moja na tisini, na kusema kwamba duniani kote watoto wametendewa ukatili,mauaji na mashambulizi ya kingono ikiwemo kuonewa na uadabishaji watoto unaokiuka haki zao. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...