Tuesday, June 27, 2017

'MARUFUKU CHAKULA KUSAFIRISHWA NJE YA NCHI' MAJALIWA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amepiga marufuku usafirishaji wa chakula nje ya nchi bila kibali na kuwataka wafanyabiashara kuuza chakula kwenye maeneo yenye uhaba nchini.

Majaliwa ametoa agizo hilo jana, Jumatatu wakati akihutubia Baraza la Eid katika Msikiti wa Masjid Riadha mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Waziri Mkuu huyo amesema kuwa kuna maeneo ambayo wananchi hawakupata chakula vizuri kutokana na uhaba wa mvua hivyo wafanyabiashara wapeleke chakula kwenye maeneo hayo.

“Serikali bado haijatoa kibali cha kutoa chakula nje ya nchi, kama unaona kuna umuhimu kaombe kibali, lakini utapewa kibali cha kusaga upeleke unga na siyo mahindi,”amesisitiza  Majaliwa.

Majaliwa ameonya kuwa kwa wale watakao kamatwa wakisafirisha mahindi nje ya nchi kinyume na utaratibu, mahindi hayo yatataifishwa na kupelekwa kwenye ghala la Taifa na magari yatapelekwa polisi.

Amesema kuwa Serikali imepokea barua za maombi ya kupeleka chakula nchi jirani, lakini bado haijatoa ruhusa.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...