Friday, December 06, 2013

HII NDIO SENTENSI YA KISWAHILI ALIYOIANDIKA NICK MINAJ INSTAGRAM KUHUSU KIFO CHA MZEE MANDELA


Kifo cha Rais wa zamani wa Afrika Kusini Mzee Nelson Mandela kimewasikitisha watu wengi wakiwemo watu wa maarufu duniani kama rapper Nicki Minaj mwenye wafuasi zaidi ya milioni tatu na nusu kwenye instagram amevunja rekodi ya kuwa staa pekee wa dunia ambae ameandika yake ya moyoni na kuongezea maneno ya lugha ya Kiswahili.
1
2

HISTORIA YA KUSISIMUA YA NELSON MANDELA


JINA KAMILI: Nelson Rolihlahla Mandela
A.K.A: Mandela
MAJINA YA UTANI: Madiba, Black Pimpernel
MAHALI ALIKOZALIWA: Mveso, Transkei, South Africa
KAZI: Mwanaharakati, Kiongozi wa dunia
TAREHE YA KUZALIWA: Julai 18, 1918
TAREHE YA KUFA: DESEMBA 05, 2013
MAHALI ALIKOFIA: Johannesburg, South Africa
ELIMU: Taasisi ya Clarkebury, Chuo cha Wesleyan, Chuo Kikuu Kishiriki cha Fort Hare, Chuo Kikuu cha London, Chuo Kikuu cha Witwatersrand, Johannesburg.
ASILI YAKE
Nelson Mandela, Mwanasiasa maarufu nchini Afrika Kusini na duniani kwa ujumla ambaye alikuwa mtu muhimu katika kuutokomeza ubaguzi wa rangi nchini mwake, ni mtoto wa Chifu wa kabila la Tembu, Chifu Henry Mandela. Mandela alizaliwa katika mji mdogo wa Transkei.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA DESEMBA 6, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.

MZEE NELSON MANDELA AFARIKI DUNIA, TANZANIA KUOMBOLEZA SIKU TATU

Marehemu Nelson Rolihlahla Mandela enzi za uhai wake.


Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela amefariki dunia muda mfupi uliopita akiwa na umri wa miaka 95 jijini Johannesburg, Afrika Kusini. Rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma amethibitisha taarifa hizo!




Rais Zuma amesema "taifa limepoteza mtu muhimu" na kuongeza "kwa sasa amepumzika. Yupo mahala pema"


Mzee Mandela aliyekuwa akisumbuliwa na homa ya mapafu amefariki akiwa amezungukwa na familia yake nyumbani kwake Johannesburg.


Mandela atazikwa kitaifa na bendera zitapepea nusu mlingoti alisema Rais Zuma.


Alikuwa akipatiwa matibabu kwa takribani miaka mitatu iliyopita na hali yake ilibadilika zaidi katika miezi sita ya mwisho kabla ya kifo chake.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...