Tuesday, February 21, 2017

MBOWE ANASWA NA POLISI

Saa 48 zilizotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Siro kwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe awe amejisalimisha zimetimia akiwa mikononi mwa jeshi hilo jana jioni.

Kamanda Sirro alitoa muda huo Jumamosi iliyopita akimtaka Mbowe afike Kituo Kikuu cha Polisi, vinginevyo wangemsaka kwa namna ambayo wanaona inafaa.

Mbowe alifikishwa kituoni hapo jana jioni, baada ya kupewa saa 48 kujisalimisha muda ambao mwisho wake ulikuwa jana.

Mwenyekiti huyo ambaye pia ni Kiongozi wa Upinzani bungeni, alijikuta mikononi mwa polisi akiwa kwenye gari barabarani katika Daraja la Mlalakuwa, lililopo Mikocheni na kufikishwa Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam.

Kukamatwa kwake, ni baada ya Februari 8 kutajwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda katika orodha ya watu 65, waliotakiwa kwende kuhojiwa juu ya dawa za kulevya.

Baada ya Mbowe kupelekwa polisi, Ofisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene alisema mwenyekiti huyo alikuwa kwenye gari akitoka nyumbani kwake Kawe, alikutana na gari la polisi na kutakiwa kusimama. 

Wakili wa Mbowe aliyefuatana naye kituoni hapo, Frederick Kihwelo alisema baada ya kutoka kituoni, zaidi ya polisi 10 walikwenda nyumbani kwake kufanya upekuzi hadi saa 3:10 usiku.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...