Thursday, September 26, 2013

BAADA YA KENYA SASA AL-SHABAAB YAIGEUKIA TANZANIA....WATISHIA KUIVAMIA MUDA WOWOTE


*Yajigamba kufanya mashambulio muda wowote
*Watanzania wapewa mafunzo ya ugaidi nje ya nchi
*Polisi nchini wasema vyombo vya ulinzi viko macho
*Mtanzania akamatwa Kenya akihofiwa gaidi
 
WAKATI wananchi wa Afrika Mashariki wakijawa na hofu ya mashambulio yanayopangwa kufanywa na vikundi vya ugaidi vya Al Qaeda na Al Shabab, imebainika kuna Watanzania waliopewa mafunzo ya ugaidi wanaojiandaa kufanya maovu.

Hayo yamebainika siku chache baada ya wanamgambo wa kundi la Al Shabab kufanya mashambulio katika Jengo la Biashara la Westgate mjini Nairobi na kuua watu zaidi ya 70 na kuacha mamia wengine wakiwa wamejeruhiwa.

Mkuu wa Interpol Tawi la Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Gustav Babile aliyasema hayo jana katika mahojiano maalumu na MTANZANIA.

YAFAHAMU MAJINA YA ASILI YA BAADHI YA MASTAR WA BONGO MOVIES

 KWA kawaida binadamu yeyote huzaliwa na kubatizwa jina ambalo hulitumia katika masomo na hata kazi yake.

Tofauti na ilivyo katika fani nyingine, wasanii wamekuwa wakijibatiza majina ya ziada (a.k.a). Mbaya zaidi, majina hayo huwa yanaanza kama utani lakini inafika wakati msanii husika

analizoea jina hilo jipya na kulifanya kuwa kama rasmi. Leo Amani linakuletea orodha ya baadhi ya mastaa ambao majina waliyopewa na wazazi wao ‘yamekufa’, hawayatumii kabisa: LULU

Jina lake halisi ni Elizabeth Michael, Lulu lilizoeleka kupitia tasnia ya uigizaji. Alianza kulitumia wakati alipojiunga na Kundi la Sanaa la Kaole.

Hadi leo hii, siyo rahisi kabisa mtu kutokea na kumuita jina la Elizabeth, wengi wanamfahamu kwa jina la Lulu.
RAY
Ray ndiyo jina ambalo limezoeleka na wengi. Vincent Kigosi alilopewa na wazazi wake ni kama limekufa. Kwa zaidi ya miaka kumi sasa tangu alipokuwa kwenye Kundi la Sanaa la Kaole hadi sasa.
Jina la Ray ndiyo watu wanalolifahamu zaidi ingawa hivi karibuni baadhi ya wasanii wenzake wamekuwa wakijaribu kumuita Vincent ili kurudisha uhai wa jina hilo.

JOHARI
Jina lake halisi ni Blandina Chagula. Johari lilizaliwa kwenye Tamthiliya iliyobeba taito ya jina hilo. Akiwa katika Kundi la Kaole, alianza kujiita Blandy, baadaye alibadilisha jina hilo na kuwa Johari walipoingiza tamthiliya hiyo ambayo pia ilizaa filamu.

MWANAFUNZI AMCHINJA MWALIMU WAKE DARASANI...!!!

KUSHOTO: Mwalimu Sun Wakang. KULIA: Damu ikiwa imetapakaa darasani muda mfupi baada ya tukio hilo.
Mwanafunzi wa China amemchinja mwalimu wake katika kulipiza kisasi baada ya simu yake ya mkononi kutaifishwa.
Mwanafunzi huyo, aliyetajwa kwa jila la Lei katika taarifa za habari za mjini humo, alibambwa na mwalimu wake, Sun Wakang akiwa anachezea simu wakati wa somo la Kemia katika shule moja mjini Fuzhou, mashariki mwa jimbo la Jiangxi nchini China.
Siku iliyofuata Lei alikwenda kwenye darasa analofundisha Sun ambako mwalimu huyo alikuwa ameketi akisahihisha mitihani, na kumchinja kutokea kwa nyuma.
Mwalimu huyo mwenye miaka 32 ambaye ni baba wa watoto watatu alifariki papo hapo huku mwanafunzi huyo akitokomea kusikojulikana.
Jana Lei alipiga namba ya simu ya dharura na kukiri kuhusika na uhalifu huo kabla ya kujisalimisha mwenyewe polisi mjini Shanghai.
Sun alifanya kazi kama mwalimu wa Kemia katika Shule ya Kati ya Linchuan No. 2 kwa miaka mitano kabla ya mauaji yake ya kutisha, ofisa wa shule Xiong Hainshuo alieleza.

NI AL-QAEDA, SI AL SHABAAB

westgate 870d9
  • Magaidi wa Marekani, Uingereza, Syria wahusika
SHAMBULIO la kigaidi lililofanywa nchini Kenya Jumamosi iliyopita na watu waliodhaniwa kuwa wafuasi wa Al- Shabab, sasa limeelezwa kutekelezwa na mtandao mpana zaidi wa kigaidi wa kundi la Al-Qaeda.


Baadhi ya wachambuzi na wachunguzi wa masuala ya kiusalama na kimataifa, wameyataja mambo matatu ambayo yanathibitisha pasipo shaka kwamba waliotekeleza tukio hilo la kuvamia, kuteka nyara na kuua watu wapatao 68 katika Kituo cha Biashara cha Westgate, ni wa aina ya kundi ambalo kinadharia na kimatendo linafanana na lile la kigaidi duniani la Al-Qaeda. Mambo yanayotajwa na wachambuzi na wachunguzi hao ni pamoja na mbinu, teknolojia na aina ya watu waliotumika kutekeleza shambulio hilo.
Katika uchambuzi wao, wameeleza kuwa mbinu iliyotumiwa na magaidi hayo kuvamia pasipo kujulikana mara moja na vyombo vya ulinzi na usalama vya nchini Kenya, lakini pia aina ya silaha walizokuwa nazo, inaonyesha kuwa kundi hilo limeamua kutumia kivuli cha Al-Shabab kufikisha ujumbe kwa dunia kwamba lipo licha ya uongozi wake kubadilika.
Kwamba mbali na mbinu pamoja na teknolojia, pia aina ya watu waliohusika kutekeleza shambulio hilo ambao wamebainika kutoka katika mataifa mbalimbali duniani, ndio ambao wamewafanya wachambuzi na wachunguzi hao waanze kupata shaka kwamba huenda kuna kundi kubwa zaidi lililotekeleza shambulio hilo, ambalo limejivika taswira ya Al-Shabab.

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI SEPTEMBA 26, 2013

DSC 0054 223dc
DSC 0055 3bc8f

MANJI AWATULIZA WACHEZAJI YANGA


MWENYEKITI wa Yanga SC, Alhaj Yussuf Mehboob Manji amewaambia wachezaji wa timu hiyo kwamba hana matatizo nao kwa matokeo ya awali ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na amewataka waelekeze nguvu zao katika mechi zijazo.
Yanga imeambulia pointi sita katika mechi tano za awali za Ligi Kuu ya Vodacom, kutokana na sare tatu, kushinda moja na kufungwa moja, hivyo kuachwa kwa pointi tano kileleni na wapinzani wao wa jadi, Simba SC.
Jana Manji alikutana kwa chakula cha jioni na wachezaji wa timu hiyo katika hoteli ya Serena, Dar es Salaam akiwa ameambatana na Makamu wake Mwenyekiti, Clement Sanga, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Isaac Chanji na Mjumbe wa Sekretarieti, Patrick Naggi.
Katika kikao hicho, Manji aliwaambia wachezaji wa Yanga hamlaumu yeyote kwa matokeo hayo, kwani ligi bado mbichi, ila akawataka waunganishe nguvu zao kuelekea mechi zijazo, ili kurejesha ushindi na furaha klabuni.
Pamoja na hilo, Manji alizungumzia suala la madai ya baadhi ya
wachezaji ya fedha za usajili na akaliweka sawa kwa wale ambao walikuwa wanadai kuwawekea utaratibu wa malipo haraka, jambo ambalo Naggi ametakiwa kuhakikisha analishughulikia mara moja.

M23 WAHOFIWA KUJIFICHA MAKANISANI DAR

m23 pic 40eb7
WASIWASI umeibuka miongoni mwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, kuhusu uwepo wa makamanda wa wapiganaji wa kikundi cha waasi wa M23, ambao wamejipenyeza nchini kwa kivuli cha kuendesha shughuli za kihoro katika baadhi ya makanisa.
Duru za uchunguzi zimeonyesha kuwa baadhi ya watu walioingia nchini kwa mwamvuli wa uchungaji wakitokea nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, majina yao yamo kwenye orodha ya wapiganaji wa kikundi hicho cha waasi.
Taarifa mbalimbali zilizokusanywa na gazeti hili zimeonyesha kuwa, raia hao wa Kongo mbali na kufanya kazi za kiroho, pia wanajihusisha na shughuli mbalimbali za kijamii pamoja na kufanya biashara ndogo ndogo.
Baadhi ya wachungaji waliozungumza Jumatano kuhusu suala hilo, walishindwa kukubali au kukanusha kuhusu taarifa hizo.
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Mikocheni B, Assemblies of God, Getrude Lwakatare, ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro (CCM), alipoulizwa kupitia simu yake ya kiganjani iwapo anazo fununu za uwepo watu wa aina hiyo ambao kwa kiasi kikubwa wameanza kujenga taswira mbaya katika baadhi ya makanisa, alikaa kimya kwa muda kisha akakata simu.

PAPA BENEDICT AKANUSHA KUTOKUWAJIBIKA KWA KASHFA ZA KANISA.

papa_g_2_1b32e.jpg
Papa wa zamani Benedict ameibuka kutoka kwenye ukimya binafsi ndani ya Vatican na kukanusha hadharani kwamba alificha vitendo vya manyanyaso ya kingono kwa watoto na mapadri wa kanisa katoliki.
Katika barua ndefu kwa mtunzi wa vitabu wa Italia asiye na dini na mwanamahesabu (Piergiorgio Odifredi) na kuchapishwa jana Jumanne na gazeti la La Republica , Benedict alikana kutokuwajibika kwa kashfa ya ngono kwa watoto.Lakini amesema kanisa lazima lifanye kila iwezalo kuzuia vitendo kama hivyo kutokea tena.
Makundi ya waathirika wamemshutumu Papa huyo kwa kutokufanya vya kutosha kuzuia manyanyaso hayo, kabla ya kuwa Papa na baada , wakati alipoongoza ofisi ya kanuni ya Kanisa, ambayo ilihusika na kesi za manyanyayaso.

ALL HAIL FOR THE KING "HE'S BACK" - HUU NDIO UJIO MPYA WA CPWAA

CherekoCherekoArtwork_1_7a659.jpgCross-Borders_Therapy_Artwork_bd180.jpg
Mashabiki wake hupendelea kumuita "King of BongoCrunk"....jina halisi ni Ilunga Khalifa a.k.a CPwaa! Msanii wa muziki wa kizazi kipya Tanzania ambaye baada ya ukimya mrefu sasa kuachia kazi zake mpya.

C.P a.k.a CPwaa mwenye tuzo 3 za Tanzania Kilimanjaro Music Awards na Multiple Channel O Africa Music Video Awards nominations anakuja kivingine kabisa mwaka huu. Tarehe 1 mwezi wa October 2013, CPwaa ataachia single yake mpya na ya kwanza kabisa kwa mwaka huu.Single hiyo iitwayo "Chereko Chereko" yenye mahadhi ya AfroDance imefanywa chini ya studio za 'De Fatality Music" na producer "Mesen Selekta" ambaye mwaka huu alichukua tuzo ya mtayarishaji bora Tanzania anayechipukia.Nyimbo hii itapatikana kwenye mitandao yote na media zote kuanzia tarehe moja October.

TANZANIA NA BURUNDI WAICHARUKIA EAC....WATAKA MAELEZO YA KINA KUTOKA RWANDA UGANDA NA KENYA



HALI ya mambo imezidi kuwa tete katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), baada ya Tanzania na Burundi kutaka maelezo ya kina kutoka kwa nchi nyingine tatu wanachama za Kenya, Uganda na Rwanda zilizoanzisha ushirikiano mpya kinyemela kati yao, kwa kuzitenga nchi hizo mbili.
Katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita kumekuwa na mfululizo wa matukio yanayoashiria kuwa Tanzania na Burundi zimetengwa na nchi hizo tatu ambazo zimeanzisha ushirikiano mpya kati yao kinyemela, kinyume cha mkataba ulioanzisha Jumuiya hiyo mwaka  1999.
Jumuiya ya sasa ilizaliwa tena upya Novemba 30, mwaka 1999 ikishirikisha nchi za Tanzania, Uganda na Kenya, wakati Rwanda na Burundi zilikaribishwa baadaye mwaka 2008.
Jumuiya hiyo mpya ilizaliwa baada ya ile ya awali iliyoanzishwa mwaka 1968 kuvunjika mwaka 1977 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kushindwa kuelewana kwa wakuu wa nchi wanachama kwa wakati huo, Mwalimu Julius Nyerere (Tanzania), Jommo Kenyatta (Kenya) na Idd Amin (Uganda).
Habari za hivi karibuni zilizopatikana kutoka ndani ya EAC zinabainisha kwamba Tanzania na Burundi zimekerwa na hatua ya nchi wanachama wenzao za Kenya, Uganda na Rwanda kuanza mchakato wa kuanzisha shirikisho la kisiasa bila ya kuzishirikisha nchi hizo.

BABU WA LOLIONDO AINENEA MAZITO TANZANIA.....AMWELEZA PINDA MAMBO ALIYOOTESHWA NA MUNGU

 
MCHUNGAJI Ambilikile Mwaisapila wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) amesema Mungu ameendelea kujifunua kwake na kumuonyesha kuwa Tanzania itakuwa kioo cha Afrika na baadaye kioo cha dunia.

Ametoa kauli hiyo Jumanne, Septemba 24, 2013 mbele ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Samunge, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha wakati msafara wa Waziri Mkuu uliposimama nyumbani kwake ili kumsalimia akiwa njiani kurejea mjini Arusha. 
Mchungaji Mstaafu Mwaisapila maarufu kama Babu wa Samunge alisema kuna mambo mengi ambayo yameandikwa kwenye Biblia lakini hayakutokea Israeli na sasa yatafanyika hapa Samunge. “Mungu ametupenda sana, yanakuja mambo makubwa na wala hayako mbali. Kama mimi ni mzee na nitayaona, kwa hiyo mtarajie kuwa hayako mbali kutokea,” alisema huku akishangiliwa. 

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...