Tuesday, May 23, 2017

HUYU NDIYE MWANAFUNZI ALIETUMIA UZOEFU WA KUOGELEA KUWAOKOA WENZIE WASIFE MAJI, GEITA.

Mwanafunzi Tisekwa Gamungu wa shule ya msingi Butwa wilayani Geita, aliyetumia uzoefu wake wa kuogelea kuokoa wenzake tisa baada ya mtumbwi waliokuwa wanasafiria kupinduka jana jioni. Wanafuzni watatu wamepoteza maisha katika ajali hiyo iliyohusisha mtumbwi uliokuwa umewabeba wanafunzi 12.

MIILI YA WANAFUNZI WATATU WALIOZAMA NA MTUMBWI GEITA YAPATIKANA

Wanafunzi watatu kati ya 24 wa shule ya msingi Butwa, waliozama katika ziwa Victoria, kisiwa cha Butwa, wamefariki dunia.

 Awali wanafunzi 21 waliokolewa na watatu hawakuonekana lakini saa chache baadaye, miili mitatu iliopolewa. Ajali hiyo ilitokea jana saa 10 alasiri.

 Mkuu wa Wilaya ya  Geita, Herman Kapufi amesema wanafunzi hao walikuwa kwenye mtumbwi waliotumia kuvuka wakitoka shuleni.

YUSUF MANJI AJIUZULU UENYEKITI YANGA.....!!!

Barua iliyosainiwa na Yusuf Manji Mei 22, 2017 inaonesha kwamba Manji ameachia rasmi nasasi ya uenyekiti wa klabu ya Yanga na makamu mwenyetiki wa klabu hiyo Clement Sanga atakuwa mwenyekiti na kuiongoza klabu hadi hapo uchaguzi utakapofanyika ili kumpata mwenyekiti mpya.

Kwa mujibu wa maelezo ya barua, Manji alifikia uamuzi wa kujiuzulu Mei 20 mwaka huu siku ambayo Yanga ilitangazwa kuwa bingwa wa ligi kuu Tanzania bara 2016/2017.

Katika barua hiyo, Manji amsema ameamua kuachia ngazi ili kutoa nafasi kwa wengine nao kushika uongozi ndani ya klabu hiyo.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...