Wednesday, April 02, 2014

POMBE ZA VIROBA KUTOKA NJE YA NCHI ZILIZOPIGWA MARUFUKU ZAINGIZWA NCHINI KWA NJIA ZA PANYA

http://jambotz8.blogspot.com/
 Pichani ni baadhi ya pombe kutoka nje ya nchi zilizopigwa marufuku kuingizwa nchini.
http://jambotz8.blogspot.com/
Meneja wa Mamlaka ya chakula na dawa (TFDA) Mkoa wa Mbeya Rodney Alananga (picha na maktaba)

Na Mwandishi Wetu Wa Jambo Tz, Mbeya

LICHA ya Serikali kukataza uingizaji wa pombe haramu kutoka nchi
jirani za Malawi na Zambia maarufu kama viroba hatimaye wananchi wamezidi kuziingiza pombe hizo na kutapakaa jijini Mbeya.

Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hii Mkoani Mbeya umebaini kuwa pombe
hizo zimekuwa  zikiingizwa kwa njia za panya kupitia vivuko visivyohalali Wilayani Kyela na kusafirisha hadi jijini Mbeya ambako imeonekana kuwa ndiko kuna watumiaji wengi wa pombe hizo.

Katika wilaya ya Kyela wafanyabiashara wa pombe hizo wamekuwa
wakisafirisha mithiri ya gunia la Mchele, juu yake wakiwa wamejaza maharage na wengine huweka dagaa za Nyasa ili vyombo husika visiweze kubaini kilichomo ndani yake.
 

 Imebainika pia kuwa wafanyabiashara hao wamekuwa wakipitisha pombe hizo katika Wilaya ya Ileje kwa kutumia Baiskeli na kuziingiza nchi kupitia eneo la Mbebe, Msia, Mapogolo, Ikumbilo, Bupigu, Ilondo na Ilulu.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz  

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...