Thursday, August 29, 2013

SHILOLE: MADEE AU OMMY DIMPOZ..?KILA MMOJA ANASWA NAE CHOBINGO....!!!

STAA wa Muziki wa Mduara, Zuwena Mohammed ‘Shilole’, amewashangaza wasanii wenzake baada ya kunaswa chobingo kwa nyakati tofauti akiwa na wasanii wenzake, Hamad Ally ‘Madee’ na Omari Faraj ‘Ommy Dimpoz’.

 Shilole akiwa na Madee.

Mpango mzima ‘uli-happen’ Agosti 25, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Singida Montel wakati wasanii hao walipokuwa katika shoo ya Serengeti Fiesta 2013 ‘Noma Sana’
Kwanza paparazi wetu alimfotoa Shilole picha kadhaa akiwa anafungwa zipu na Madee.


                                   ...Akiwa na Ommy Dimpoz.
 

BAADA YA KIMYA KIREFU, GK AIBUKA NA NGOMA MPYA

GK (katikati) akiwa na DJ Fetty (kushoto) na msanii Pauline Zongo (kulia) ndani ya Studio za Clouds FM  
 GK akiwa ndani ya Studio za Clouds FM wakati akielezea kuhusu ujio wake.
MSANII mahiri katika anga za muziki wa Bongofleva, Gwamaka Kaihura 'King Crazy GK' leo ameibuka na singo yake mpya iitwayo Baraka au Laana aliyomshirikisha msanii Yuzo. aka sita baada ya kuwa busy na masomo kitendo kilichopelekea kuupa kisogo muziki kwa muda na kuwafanya mashabiki wake kum-mis katika fani hiyo. Memba huyo wa East Coast Team ameachia ngoma yake mpya leo na anataraji kuachia video yake siku ya Ijumaa Agosti 30, mwaka huu. 
GK alisema kuwa amerudi kwenye game kwa nguvu zote na amewashukuru baadhi ya wadau kama Eric Shigongo, Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga kwa kumtia hamasa ya kurudi kwa nguvu mpya baada ya kupotea kwa muda.

ETO'O AWASILI LONDON KUFANYIWA VIPIMO NA KUJIUNGA NA CHELSEA

eto c6562
Eto'o akiwasili London (HM)
eto2 85114
Chelsea inakaribia kumsajili mshambuliaji Samuel Eto'o kwa dili la mwaka mmoja lenye thamani ya £7million kwa mkataba wa mwaka mmoja leo Alhamisi baada ya kukiri kushindwa kumpata mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney.

Eto'o, 32, amekubali kupunguza dau lake alilokuwa akilipwa na Anzhi kiasi cha £17m kwa mwaka na sasa atasaini atasaini akiwa huru.

Pamoja na hilo, lakini inaeleweka kwamba Anzhi wamemlipa Eto'o millioni kadhaa ili kuweza kumuondoa katika listi wachezaji wanaolipwa fedha nyingi ndaniya klabu ya Anzhi.

Eto'o aliwasili jijini London jana usiku na anategemewa kufanyiwa vipimo vya afya mchana wa leo katika uwanja wa mazoezi wa Chelsea Cobham. Chanzo: Shaffihdauda

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI AGOSTI 29, 2013

DSC 0106 63caa
DSC 0107 9b33d
DSC 0108 3505d

MAPYA YAIBUKA KUHUSU TRAFIKI FEKI, KUMBE ALIKUWA MFUNGWA ALIYETOROKA JELA.... !!!

MAZITO tena yameibuka kuhusu yule trafiki feki James Hussein, mkazi wa Kimara Matangini, jijini Dar es Salaam ambaye yuko Gereza la Segerea, Dar akikabiliwa na kesi ya kujifanya askari wa usalama barabarani.

Habari za ndani kutoka Gereza la Isanga, Dodoma zinadai kuwa, trafiki huyo ana mambo mengi ya kushangaza ambayo Watanzania wengi hawayajui.

Mtoa habari wetu alisema kuwa, James Hussein si jina halisi la trafiki feki huyo. Alisema jina lake halisi ni Ali Kinanda.

“Yule jamaa anaitwa Ali Kinanda, sisi kumwona kwenye picha gazetini akijiita James Hussein tulishangaa sana,” kilisema chanzo chetu.

Chanzo kikazidi kudai kwamba, kuanzia mwaka 1984 jamaa huyo alikuwa ni askari magereza katika Gereza la Butimba, Mwanza hadi mwaka 1987 alipoacha.

Mtoa habari wetu aliendelea kumwanika trafiki feki huyo kuwa, mwaka 2002 mtuhumiwa huyo alidaiwa kupata msala wa tukio la ujambazi lililotokea Mpwapwa, Dodoma ambapo kesi yake iliunguruma hadi mwaka 2003 ambapo hukumu ilitolewa yeye na wenzake kwenda jela miaka 30.

''OCD' ''KUPIGA PICHA ZA UTUPU NI KOSA KISHERIA SASA OLE WAKO UPIGE HALAFU UKAMATWE CHAMOTO MTAKIONA''



Jeshi la Polisi Kanda ya Kinondoni limetoa kauri nzito kuhusu picha za udhalilishaji zilinazosambazwa na wasanii wetu wa bongo movie zikiwemo za Manaiki Sanga.

Akiongea katika mahojiano maarumu mkuu wa kituo cha Polisi Oysterbay “OCD” Mtafungwa alisema kuwa kimsingi kupiga picha za utupu ni kosa kisheria hivyo endapo muhusika akimatwa atashtakiwa kwa mujibu wa sheria.

Mtafungwa aliendelea kufafanua kuwa” Unajuwa Jeshi la Polisi lipo kwa ajili ya kusimamia sheria iliyowekwa na serikali hivyo huwa kuna namna ya kuwakamata wahusika hasa kama kumetokea malalamiko toka idara flani kuhusiana na matukio yoyote yanayopelekea uvunjifu wa amani au kupotosha maadili” Alisema Kamanda huyo kipenzi cha watu

Aidha Kamanda huyo aliendelea kufafanua “ Pia Jeshi la polisi linamamlaka ya kumkamata mharifu yeyote kwa muda wowote endapo kipindi hicho akikutwa anafanya uharifu ni pamoja na upigaji picha hizo chafu, Lakini kubwa tuhajitaji kumkata mtu na ushahidi ili iwe rahisi kumbana na kumfikisha mbele ya sheria” Alisema

Mtafungwa alimaliza kusema “ Tunaendelea kufatilia kupita mitandao ya kijamii ili kuona hizo picha zikoje halafu tuhaahidi kuwatolea taarifa hadharani kupita kwa msemaji wa Jeshi la Polisi Kanda ya Kinondoni RPC Wambura ambae kisheria ndiye mwenye mamlaka ya kusema” Alisema Mtafungwa

MWIGULU NCHEMBA ATAKA MBOWE NA DR. SLAA WAKAMATWE KWA MAUAJI YA RAIA

 MBUNGE wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba (CCM), amechafua hali ya hewa bungeni kwa kuitaka Serikali kuwachukuliwa hatua viongozi wa juu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Mbunge huyo alisema mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe pamoja na Katibu Mkuu wake, Dk. Wilbroad Slaa, wanapaswa kuchukuliwa hatua kwa madai ya kusababisha mauaji ya raia.

Mwigulu, ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bara, alisema katika kipindi cha miaka miwili tangu nchi ilipotoka kwenye uchaguzi, viongozi hao wamekuwa wakihamasisha maandamano na kusababisha umwagaji wa damu za Watanzania.

“Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha miaka miwili tangu nchi yetu ilipomaliza Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, Mbowe na Dk. Slaa wamekuwa wakitoa kauli za wazi na hata kusababisha mauaji ya watu bila hatia.

“Kutokana na hali hii, sijui Serikali inafanya nini katika kuwachukulia hatua, kwani viongozi hawa wamekuwa wakitafuta umaarufu wa kisiasa kwa kuchochea chuki na mauaji dhidi ya raia.

“Kwa hali hiyo, tangu kipindi hicho hadi leo hii wanasubiri nini badala ya kwenda kuwaweka jela, kwani huko ndiko wanatakiwa kuwa,” alisema.

Mwigulu, alisema kukosekana kwa maadili kwa baadhi ya viongozi wa siasa, ambao wamekuwa wakitumia majukwaa na kuhubiri umwagaji damu ni hatari kwa taifa.

Alisema viongozi hao wamekuwa wakitumia majukwaa hayo na kusababisha vifo vya wananchi, huku akitaja vurugu zilizotokea katika mikoa ya Morogoro, Iringa, Arusha na Singida.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...