Tuesday, December 16, 2014

UKAWA MBELE KWA MBELE

Wafuasi wa CHADEMA mjini Nansio Wilaya ya Ukerewe, Mwanza wakishangilia ushindi katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika juzi. 

Matokeo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika juzi, yanaonyesha kuimarika kwa upinzani nchini baada ya kupata viti vingi vya uenyekiti wa mitaa na vijiji, pamoja na mamia ya wajumbe wa Serikali husika.
Hayo yanaonyesha kuwa vyama hivyo vimeanza kuimarika katika ngazi za chini, tofauti na ilivyokuwa mwaka 2009, katika uchaguzi ambao CCM kilipata ushindi wa kishindo wa asilimia 91.72, huku wapinzani wakigawana asilimia 8.28 zilizobaki.
Licha ya uchaguzi wa juzi kugubikwa na kasoro lukuki, upinzani umeonekana kuchomoza huku katika baadhi ya mikoa ukipata ushindi maradufu hasa katika ile ambayo una nguvu kubwa wakati katika maeneo ambayo ulikuwa na viti vichache au kutokuwa navyo kabisa, umeibuka na kuipokonya CCM baadhi ya mitaa na vijiji.

Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year

MARCIO MAXIMO ATUPIWA VIRAGO YANGA NI BAADA YA KICHAPO CHA 2-0 KUTOKA SIMBA

YANGA SC imeirejea historia yake ya kuwatimia makocha wake muda mfupi tu baada ya kula kichapo kutoka kwa watani zao Simba ambapo tayari uongozi wa Yanga umelivunja benchi la ufundi la timu hiyo lililokuwa likiongozwa na makocha Wabrazil, Marcio Maximo na Msaidizi wake, Leonardo Neiva na kuwarejesha Mholanzi, Hans Van der Pluijm na  Charles Boniface Mkwasa 'Master'.

Maximo anaondolewa baada ya kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa mahasimu Simba SC Jumamosi katika mchezo wa Nani Mtani Jembe, wakati Pluijm anawasili usiku huu na kesho atasaini Mkataba na kuanza kazi. Mkwasa tayari alisaini Mkataba wiki kadhaa zilizopita na ameridhika kufanya kazi chini ya Pluijm tena.
Maximo na Leonardo walitua Yanga SC Julai mwaka huu kurithi mikoba ya Pluijm na Mkwasa ambao walipata kazi Uarabuni. Hata hivyo baada ya muda usiozidi mwezi mmoja, Pluijm na Mkwasa waliacha kazi Uarabuni, wakidai kukerwa na kuingiliwa na viongozi wa klabu yao katika masuala ya kiufundi.
  Pluijm alirudi Ghana wakati Mkwasa alirejea nyumbani Tanzania kabla ya kuajiriwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kama Mkufunzi Mkuu. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutoa maoni kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

UTITIRI WA WACHEZAJI WA KIGENI KUTAICHIMBIA KABURI SOKA YA TANZANIA NA KUUWA TIMU YA TAIFA KAMA ILIVYO UINGEREZA

Simon Sserunkuma 
Mshambuliaji huyo raia wa Uganda alikuja nchini na timu ya Express ya nchini humo na kucheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya Simba na Yanga na ndipo viongozi hao wa Yanga walipomwona na kumleta nchini ili kufanya naye mazungumzo lakini mambo yakawa tofauti kwani alitoroshwa kimya kimya na kupelekwa Zanzibar ambako Simba iliweka kambi kujiandaa na mechi ya Nani Mtani Jembe iliyochezwa juzi Jumamosi.
ACHANA na Yanga kufungwa mabao 2-0 na Simba katika mechi ya Nani Mtani Jembe, imebainika kuwa Simba iliifanyia Yanga umafia kwa mchezaji Simon Ssrenkuma baada ya kumtorosha kutoka mikononi mwa viongozi wa klabu hiyo na kwenda kumficha kwenye kambi ya timu hiyo visiwani Zanzibar wiki iliyopita.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutoa maoni kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE DESEMBA 16, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC07117
DSC07114
DSC07116
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year

THIERRY HENRY ATANGAZA RASMI KUSTAAFU SOKA

Theirry-Henry-in-action-o-007 
Katika ulimwengu wa soka leo kuna habari kubwa ambayo imeenea duniani kutokana na staa mkubwa na mkongwe Thierry Henry kutangaza kustaafu soka na kujiunga na shughuli nyingine. Nyota huyo  ambaye ameng’aa kwenye mchezo huo kwa muda mrefu sana akichezea vilabu mbalimbali ikiwemo Arsenal na Barcelona.
download
Henry ametangaza rasmi kustaafu soka dakika chache zilizopita na kusema kuwa kuanzia mwakani ataanza kujishughulisha kama Balozi wa Sky Sports huku akisema kuwa anajisikia furaha kuchezea vilabu vikubwa na pia anaamini anajiunga na kituo kikubwa cha Television na matarajio yake ni kuwa mchambuzi bora wa michezo kwenye kituo hicho.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutoa maoni kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

HAYA NDIYO MAAMUZI MAGUMU YA YANGA KUHUSU MBRAZIL EMERSON

Moja ya vichwa vya habari vilivyokuwa vimepambwa na habari kumhusu Emerson.

Taarifa za usajili na kuachwa wachezaji zinazidi kuingia na safari hii inasemekana kuwa kiungo Mbrazil Emerson amekuwa mhanga wa kwanza wa kuondoka kwa kocha Mbrazil Marcio Maximo baada ya mchezaji huyo kuachwa na Yanga.
Mbrazil huyo anaondoka Yanga baada ya kucheza mechi moja pekee dhidi ya Simba ambako Yanga ilifungwa 2-0.
Emerson alishindwa kuwaridhisha mashabiki wa Yanga ambao wengi walionyesha kukerwa na uwezo mdogo wa kiungo huyo katika dakika 45 alizocheza kwenye mechi dhidi ya Simba.
Emerson alikuja nchini siku chache zilizopita ambapo alipaswa kuziba nafasi iliyoachwa wazi na mshambuliaji Genilson Santos Santana Jaja ambaye hakurudi baada ya kuondoka nchini kufuatia kusimama kwa ligi. 
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutoa maoni kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...