Tuesday, December 16, 2014

UTITIRI WA WACHEZAJI WA KIGENI KUTAICHIMBIA KABURI SOKA YA TANZANIA NA KUUWA TIMU YA TAIFA KAMA ILIVYO UINGEREZA

Simon Sserunkuma 
Mshambuliaji huyo raia wa Uganda alikuja nchini na timu ya Express ya nchini humo na kucheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya Simba na Yanga na ndipo viongozi hao wa Yanga walipomwona na kumleta nchini ili kufanya naye mazungumzo lakini mambo yakawa tofauti kwani alitoroshwa kimya kimya na kupelekwa Zanzibar ambako Simba iliweka kambi kujiandaa na mechi ya Nani Mtani Jembe iliyochezwa juzi Jumamosi.
ACHANA na Yanga kufungwa mabao 2-0 na Simba katika mechi ya Nani Mtani Jembe, imebainika kuwa Simba iliifanyia Yanga umafia kwa mchezaji Simon Ssrenkuma baada ya kumtorosha kutoka mikononi mwa viongozi wa klabu hiyo na kwenda kumficha kwenye kambi ya timu hiyo visiwani Zanzibar wiki iliyopita.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutoa maoni kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.
Mshambuliaji huyo raia wa Uganda alikuja nchini na timu ya Express ya nchini humo na kucheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya Simba na Yanga na ndipo viongozi hao wa Yanga walipomwona na kumleta nchini ili kufanya naye mazungumzo lakini mambo yakawa tofauti kwani alitoroshwa kimya kimya na kupelekwa Zanzibar ambako Simba iliweka kambi kujiandaa na mechi ya Nani Mtani Jembe iliyochezwa juzi Jumamosi.
Simon ambaye ni mdogo wa Dann Sserunkuma anayeichezea Simba pia, aliliambia Mwanaspoti kuwa viongozi wa Yanga ndiyo waliyeongea naye kwa ajili ya kumsajili na alikuja nchini ili kuzungumza nao lakini alishangaa kujikuta akipelekwa kwenye kambi ya Simba visiwani Zanzibar.
“Kusema kweli nilikuja hapa kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Yanga na ndiyo walionileta, nilishangaa kujikuta niko kwenye kambi ya Simba, sijui ni kitu gani kilitokea,” alisema Simon.
Mbali na hilo mshambuliaji huyo aliongeza kuwa anafurahi kuwa amejiunga na kikosi cha Simba kwani kina wachezaji wengi vijana kuliko kile cha Yanga kilichojaa wachezaji ambao wamecheza muda mrefu.
“Nafurahi kuwa nimeingia kwenye kikosi chenye damu changa nyingi, ni rahisi kutengeneza kombinesheni hapa kuliko kwenye kikosi cha Yanga, nafikiri nitafanya makubwa hapa,” alisema Simon.
Katika mchezo wa juzi, Sserunkuma alifanya vizuri na kuzima kabisa harakati za Yanga za kupata ushindi katika mchezo huo wa pili wa Nani Mtani Jembe. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutoa maoni kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.
Na Mwanaspoti

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...