Kikosi cha Taifa Stars.
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen ameita kambini wachezaji 24
kujiandaa kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Gambia
itakayochezwa Septemba 7 mwaka huu nchini humo.
Wachezaji hao
wanatakiwa kuripoti kambini Agosti 29 mwaka huu kabla ya saa 1 kamili
usiku. Kambi ya Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager
itakuwa kwenye hoteli ya Accommondia jijini Dar es Salaam.
Makipa
walioitwa katika timu hiyo Juma Kaseja (Simba), Mwadini Ali (Azam), Ally
Mustafa (Yanga) na Aishi Manula (Azam). Mabeki ni Aggrey Morris (Azam),
Kelvin Yondani (Yanga), Shomari Kapombe (Simba), Nadir Haroub (Yanga),
Erasto Nyoni (Azam), Vincent Barnabas (Mtibwa Sugar) na David Luhende
(Yanga).
Viungo Khamis Mcha (Azam), Salum Abubakar (Azam), Said
Dilunga (Ruvu Shooting), Frank Domayo (Yanga), Athuman Idd (Yanga),
Haruna Chanongo (Simba), Amir Kiemba (Simba), Mrisho Ngasa (Yanga),
Simon Msuva (Yanga), John Boko (Azam), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe,
Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya
Kidemokrasi ya Congo) na Juma Liuzio (Mtibwa Sugar).