Tuesday, June 27, 2017

'MARUFUKU CHAKULA KUSAFIRISHWA NJE YA NCHI' MAJALIWA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amepiga marufuku usafirishaji wa chakula nje ya nchi bila kibali na kuwataka wafanyabiashara kuuza chakula kwenye maeneo yenye uhaba nchini.

Majaliwa ametoa agizo hilo jana, Jumatatu wakati akihutubia Baraza la Eid katika Msikiti wa Masjid Riadha mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Waziri Mkuu huyo amesema kuwa kuna maeneo ambayo wananchi hawakupata chakula vizuri kutokana na uhaba wa mvua hivyo wafanyabiashara wapeleke chakula kwenye maeneo hayo.

“Serikali bado haijatoa kibali cha kutoa chakula nje ya nchi, kama unaona kuna umuhimu kaombe kibali, lakini utapewa kibali cha kusaga upeleke unga na siyo mahindi,”amesisitiza  Majaliwa.

Majaliwa ameonya kuwa kwa wale watakao kamatwa wakisafirisha mahindi nje ya nchi kinyume na utaratibu, mahindi hayo yatataifishwa na kupelekwa kwenye ghala la Taifa na magari yatapelekwa polisi.

Amesema kuwa Serikali imepokea barua za maombi ya kupeleka chakula nchi jirani, lakini bado haijatoa ruhusa.

Monday, June 26, 2017

JAMBO TZ INAWATAKIA EID MUBARAK WAISLAMU WOTE DUNIANI

Uongozi na wafanyakazi wote wa Jambo Tz Blog wanawatakia watanzania wote kwa ujumla Eid Mubarak na mapumziko mema katika sikukuu ya Eid El Fitr.

Sunday, June 18, 2017

OLE SENDEKA AWAKUBALI WAPINZANI MSIBANI KWA MAMA YAKE

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka amesema tofauti za itikadi za kisiasa zisitumike kuwagawa Watanzania, bali ziwe chachu ya kufanikisha maendeleo.

Ole Sendeka aliyasema hayo jana, wakati wa kuaga mwili wa mama yake Raheli Sendeka kwenye ibada iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Engarenarok jijini Arusha.

Alisema baada ya kutokea kwa msiba huo, viongozi wa kwanza kufika nyumbani kwake kumpa pole walikuwa mbunge na diwani wa Chadema, hivyo amepata somo kuwa tofauti za kisiasa hazipaswi kuondoa umoja na upendo wa Watanzania. Alisema mbunge wa kwanza kufika nyumbani kwake Ngarenaro jijini hapa ni wa Siha mkoani Kilimanjaro (Chadema), Dk Godson Mollel na diwani wa Ngarenaro (Chadema), Issaya Doita.

MAJERUHI WA LUCKY VINCENT KUREJEA NCHINI MWEZI WA NANE

Watoto watatu walionusurika katika ajali iliyoua wanafunzi 32, walimu wawili na dereva wa Shule ya Lucky Vincent ya mjini Arusha, huenda wakaruhusiwa kurejea nchini baada ya miezi miwili.

Taarifa hiyo imetolewa na Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu katika mtandao wake wa kijamii wa Facebook.

Pia, Nyalandu ameandika katika mtandao huo kuwa watoto hao; Doreen Mshanga, Saidia Ismael na Wilson Tarimo wanategemewa kutembea tena.

Hata hivyo, kwa sasa Doreen, atahamishiwa katika kituo maalumu kwa ajili ya matibabu ya uti wa mgongo cha Madonna katika mji wa Lincoln, Nebraska.

“Katika watoto wote hao watatu, Doreen ni muujiza mkubwa zaidi,” amesema Nyalandu.

UTHAMINI MOYO WAKO, KAA MBALI NA MAUMIVU

HAKUNA ubishi kuwa mapenzi yanachukua nafasi kubwa sana katika maisha ya binadamu, ipo dhahiri kwamba mapenzi yanaweza kuleta furaha maishani mwako lakini wakati huohuo  maumivu, mateso na karaha.

Watu wengi bado wanalizwa na mapenzi na hii ni kwa sababu hawafuati kanuni sahihi za mapenzi. Ndiyo… mapenzi yana kanuni zake.

Kwa bahati mbaya kabisa, kwa sasa mapenzi yamegeuzwa na kuwa kama kitu cha kujaribu au kufanyia biashara ndiyo maana yanawatesa wengi.

Lakini ni kwa nini mapenzi yaendelee kututesa?  Au ni kwa sababu hatujui maana halisi ya mapenzi? Hebu tuyaangalie mapenzi kwa jicho la tatu, kisha tuchukue hatua.

MAPENZI NI NINI?
Katika hali ya kawaida, mapenzi hayaelezeki kuwa ni nini. Ni vigumu sana mtu kukueleza maana ya mapenzi ndiyo maana kila mtu ana uelewa tofauti juu ya suala hilo.

Saturday, June 17, 2017

MANGULA AWATAKA WAPINZANI KUACHA KUDANDIA TRENI KWA MBELE SAKATA LA MCHANGA WA MADINI

Makamu Mwenyekiti wa CCM, Tanzania Bara, Philip Mangula amesema kitendo alichokifanya Rais John Magufuli cha kuwafichua wanaotorosha mchanga wa madini kipo kwenye ilani ya chama hicho hivyo wapinzani waache kudandia treni kwa mbele.

Mangula amesema hayo leo (Jumamosi) wakati akizungumza na wanachama wa CCM kwenye kongamano la kuunga mkono juhudi za Rais na kumpongeza kwa kuwafichua mafisadi lililoandaliwa na wanachama hao.

"Alichokifanya Rais kipo ndani ya ilani ya chama, wapo wanaotaka kudandia treni kwa mbele wakidai wao ndiyo walikuwa na mawazo hayo, nataka niwaambie Rais anatekeleza ilani hiyo ni mipanngo ya CCM, "amesema.

Pia, Mangula amewaonya watu wanaoibuka na kutaka kukwamisha kazi anayofanya Magufuli kuwa hawataweza na nchi haitashtakiwa kama wanavyodai.

“Niwatoe hofu wananchi na wanachama wote kuwa nchi iko salama zaidi tumuunge mkono Rais wetu kuwafichua wezi wa mali za nchi, "amesema

MTANZANIA ATUPWA JELA UINGEREZA KWA KOSA LA KUPOST PICHA ZA MAREHEMU FACEBOOK

Mwanaume mmoja anayedaiwa kuwa ni Mtanzania amehukumiwa kifungo cha miezi mitatu jela nchini Uingereza kwa kosa la kurusha katika ukurasa wake wa Facebook, picha za mtu aliyefariki dunia kutokana na moto uliounguza jengo la ghorofa la Mnara wa Grenfell lililopo nchini humo.

Pia, mtu huyo ametakiwa kulipa faini ya Sh579,880 kwa mwathirika wa tukio hilo.

Mtanzania huyo, Omega Mwaikambo (43) alituma video na picha za mwili wa marehemu uliokuwa kwenye begi  na baadaye picha nyingine tano zikionyesha uso wa  marehemu huyo.

Friday, June 16, 2017

HII NDIO NDEGE BINAFSI ALIYOKUJA NAYO MWENYEKITI WA KAMPUNI YA BARRICK GOLD CORPORATION KWAAJILI YA KUJA KUFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS MAGUFULI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika picha ya pamoja na  Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambayo ni mmiliki mkubwa wa kampuni ya Acacia Mining Limited Prof. John L. Thornton pamoja na Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Ian Myles na Waziri wa Sheria na Katiba Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi.

WANAFUNZI 56 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 207 WABADILISHIWA SHULE

Taarifa kutoka ofisi ya Rais-TAMISEMI imeonyesha mabadiliko ya kuwapangia shule wanafunzi 56 waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano katika Shule ya Sekondari Madibira Tahasusi ya PCB na kuwapeleka katika shule zingine zenye tahasusi (Combination) hiyo ndani ya Mkoa wa Mbeya na Mikoa ya jirani. Mabadiliko haya ni kwa sababu maalum.

Aidha, wanafunzi wapya 56 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha Tano katika shule ya Sekondari Madibira Tahasusi ya CBG kama inavyoonekana kwenye tovuti. Wanafunzi hawa wanapaswa kuripoti katika shule walizopangiwa tarehe 17 Julai, 2017. 
TAARIFA KWA UMMA (15-06-2017)

 Tafadhali bofya chini Kujua Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa na Waliobadilishwa kidato cha 5 kwa sababu maalum.

Wednesday, June 14, 2017

USHAHIDI WA KESI YA WEMA WAKWAMA KUTOLEWA

Kesi ya kukutwa na dawa za kulevya inayomkabili Wema Sepetu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirishwa hadi Julai 10.

Wema ambaye ni mshindi wa taji la urembo, maarufu Miss Tanzania kwa mwaka 2006 na msanii wa filamu, anakabiliwa na kesi hiyo akidaiwa kutumia na kupatikana na bangi.

Wakili wa Serikali, Elizabeth Mkunde mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa alisema kesi ilipangwa leo (Jumatano) kuanza kusikiliza ushahidi wa upande wa mashtaka lakini Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba anayeisikiliza kesi hiyo yupo likizo.

Kutokana na hilo, aliomba iahirishwe hadi Julai 10 ombi lililokubaliwa na mahakama. Wema na wenzake Angelina Msigwa na Matrida Abbas wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na dawa za kulevya na kutumia dawa hizo.

Inadaiwa Februari 4, katika makazi ya Wema, Kunduchi Ununio, walikamatwa wakiwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08. Wema pia anadaiwa Februari Mosi katika eneo lisilojulikana jijini Dar es Salaam alitumia bangi.

MAGUFULI AFANYA MAZUNGUMZO NA ACACIA, WAKUBALI KULIPA FEDHA WANAZODAIWA NA PIA KUSAIDIA UJENZI WA MTAMBO WA KUCHENJULIA DHAHABU NCHINI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika picha ya pamoja na  Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambayo ni mmiliki mkubwa wa kampuni ya Acacia Mining Limited Prof. John L. Thornton pamoja na Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Ian Myles na Waziri wa Sheria na Katiba Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiagana Mhe. Ian Myles balozi wa Canada Nchini pamoja na  Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambayo ni mmiliki mkubwa wa kampuni ya Acacia Mining Limited Prof. John L. Thornton alipofoika ikulu kwa mazungumzo juni 14,2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na  Mwenyekiti wa Barrick  Gold Corporation  Profesa John L. Thornton baada ya mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es salaam  Juni 14, 2017. wakiwa na  Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi na Balozi wa Canada nchini Mhe. Ian Myles.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambayo ni mmiliki mkubwa wa kampuni ya Acacia Mining Limited Prof. John L. Thornton na kukubaliana kuwa kampuni hiyo ipo tayari kufanya mazungumzo na Serikali ya Tanzania ili kulipa fedha ambazo Tanzania imezipoteza kutokana na kampuni hiyo kuendesha shughuli zake hapa nchini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya mawasiliano Ikulu ni kwamba, Prof. John L. Thornton ambaye amesafiri kwa ndege binafsi kutoka nchini Canada hadi Tanzania amekutana na Mhe. Rais Magufuli leo Juni 14, 2017 Ikulu Jijini Dar es Salaam na mazungumzo yao yamehudhuriwa na Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Ian Myles na Waziri wa Sheria na Katiba Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi.

Tuesday, June 13, 2017

LISSU AMGEUKIA KIKWETE ATAKA NAE AJUMUISHWE KWENYE ORODHA YA WASHTAKIWA WA MAKINIKIA.

Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu ameipa changamoto Serikali kwa kuitaka kumuingiza Jakaya Kikwete katika orodha ya watuhumiwa wa sakata la makinikia.

Akichangia bungeni leo Jumanne, katika hotuba ya bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2017/18, Lissu amesema kuwa wakati wa kusaini mikataba ya madini Kikwete alikuwa ni Waziri wa Maji, Nishati na Madini.

“Katika taarifa hii ya jana wamependekeza watu fulani fulani washtakiwe makamishna, mwanasheria mkuu, Andrew Chenge (Mbunge wa Bariadi), Wiliam Ngeleja (Sengerema) jamani naombeni niwaambie kitu ili  wabunge muwe na maarifa,” amesema na kuongeza:

“Mtu wa kwanza kusaini mikataba na leseni za madini alikuwa ni Meja Jakaya Mrisho Kikwete, Agosti 5 mwaka 1994 alisaini leseni ya Bulyankulu inayopingwa leo hii wakati akiwa Waziri wa Maji, Nishati na Madini wakati huo hakuwa na kinga ya urais.”

Amesema wakati aliposaini leseni na mikataba hiyo alikuwa hana kinga kwa masuala ambayo aliyafanya.

“Rais (Kikwete) alisaini si ya Bulyankulu pekee ya Nzega, ya Geita hizo leseni zina saini ya Kikwete anaponaje kwa mapendekezo haya? Anaponaje kama kweli mnataka kuwashughulikia watu walioshiriki kwenye mambo haya?” amehoji.

“Mbona mnachagua chagua hizi? Leseni na hizi sheria tangu mwaka 1999 tumesema tatizo kubwa ni sheria.”

Amemtaka Spika wa Bunge, Job Ndugai kama anataka kukumbukwa wakati wa uongozi wake basi asikubali kupitisha miswada ya sheria kwa hati ya dharura.

Akijibu swali hilo, Ndugai amesema atairuhusu miswada hiyo ya madini na gesi iingie bungeni kwa hati ya dharura.

“Kwanza wanaoamua siyo mimi tu ni kamati ya uongozi ya Bunge, lakini kama itakuja kwa hati ya dharura hii (madini) itaruhusiwa kwasababu moja tu tunaibiwa sana.” amesema.

Wednesday, June 07, 2017

SHILOLE: WATOTO WANGU HAWATAIGA MAISHA YANGU


MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, amesema kwamba watoto wake hawataiga maisha wala mavazi anayovaa kwenye shoo zake wala maisha ya sanaa anayoishi kwa kuwa wanatambua yupo kazini kwa ajili yao.

Shilole akiongea na mwandishi wa habari hii alisema kwamba, malezi anayowalea watoto wake ni tofauti na maisha anayoishi yeye na watoto hao wanatambua kwamba mama yao ni msanii hivyo hawataiga anachofanya.

 “Watoto wangu nawalea katika maadili kama mama, siwezi kuwalea maisha ya kistaa kama ninavyoishi mimi na wanatambua kwamba mama yao nipo kazini kwa ajili yao na pia hawana ndoto za kuishi maisha yangu ya kisanii,” alieleza Shilole.

Shilole aliongeza kwamba licha ya kulea watoto wake kwa maadili ya dini, lakini hataacha kuendelea kuwapa elimu, mafunzo ya maisha na biashara.

HUDDAH: SITAKI KUOLEWA

MWANAMITINDO maarufu nchini Kenya, Huddah Monroe, amefunguka na kusema kwamba hana mpango wa kuolewa katika maisha yake.

Mrembo huyo ambaye hakauki mitandaoni, amekuwa akihusishwa kutoka na nyota wa soka wa timu ya Taifa ya Kenya na klabu ya Tottenham ya nchini England, Victor Wanyama, lakini amekuwa akikana taarifa hizo na sasa ametangaza kwamba hana mpango wa kuolewa kwenye maisha yake.

“Kila mtu ana mipango yake, hivyo kwa upande wangu sina mpango wowote wa kuolewa. Hata hivyo, kama itakuja kutokea nikaolewa hatakuwa mwanamume wa Nigeria.

“Maana kuna taarifa kwamba natoka na Wizkid, sikushangaa sana kwa kuwa niliwahi kuposti picha nikiwa na msanii huyo nilipokutana naye nchini Marekani, picha hizo zikaleta maneno mengi nina uhusiano naye wa kimapenzi hakuna ukweli na sitaolewa na mwanamume wa Nigeria,” alisema Huddah.

ACT WAZARENDO WAMVUA CHEO MAMA MGHWIRA

Chama cha ACT Wazalendo kimmevua uongozi aliyekuwa mwenyekiti wake, Anna Mgwhira ambaye ameteuliwa na Rais John Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Chama hicho kimefikia hatua hiyo kwa kuzingatia ibara ya 17 ya katiba yake ambayo inatamka kuwa kiongozi wa chama atakoma kuendelea na madaraka yake iwapo atashindwa kutekeleza majukumu yake.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano, Kaimu Kiongozi wa ACT, Samson Mwingamba alisema kamati ya uongozi wa ACT ulikutana leo lengo kuu ni kutafakari lililotokea kuona namna gani Mgwhira anaweza kutimiza majukumu yake kama Mwenyekiti na Mkuu wa Mkoa.

“Kama chama baada ya kutafakari kwa kina na baada ya mashauriano baina yake na viongozi kutumia katiba ya chama anakoma kuwa kiongozi kwa kuwa kutakuwa na mgongano wa majukumu, maslahi hivyo anakoma kuwa mwenyekiti,” alisema Mwigamba.

Mwigamba alisema kamati ya chama imemchagua Yeremia Maganja kuwa  Kaimu Mwenyekiti na kamati ilimpongeza Rais Magufuli kwa kumteua Mgwhira.

Hata hivyo, Mwigamba alisema Mghwira bado ataendelea kuwa mwanachama halali wa chama hicho.

Saturday, June 03, 2017

WEMA SEPETU ABADILISHIWA HATI YA MASHTAKA

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeanza kusikiliza kesi inayomkabili msanii wa filamu, Wema Sepetu na wafanyakazi wake wawili, huku upande wa mashtaka ukiiomba mahakama hiyo kubadili hati ya mashtaka.

Akiwasilisha hoja hiyo juzi mbele ya Hakimu Thomas Simba, Mawakili upande wa jamhuri, Constantine Kakula na Paulina Fungameza, walianza kuwasomea  upya mashtaka washtakiwa hao ambao ni Wema Sepetu na wafanyakazi wake wawili, Angelina Msigwa na Matrida Abas.

Alidai shtaka la kwanza linalowakabili watuhumiwa hao ni pamoja na kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya ambapo mnamo Februari 4, mwaka huu katika maeneo ya Kunduchi Ununio, washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kukutwa na msokoto mmoja na vipisi vya dawa za kulevya aina ya bangi yenye gramu 1.08.

MNYIKA ATOLEWA NJE YA BUNGE KWA AMRI YA SPIKA

Mbunge wa Kibamba, John Mnyika ametolewa nje ya Bunge jana Ijumaa kwa agizo la Spika wa Bunge, Job Ndugai.

Licha ya adhabu hiyo, amemzuia kutohudhuria vikao vya Bunge kwa siku saba kuanzia hiyo jana.

Mnyika ametolewa baada ya mmoja wa wabunge kusema 'Mnyika mwizi' akimhusisha na wizi wa madini, hoja inayochangiwa na wengi kwenye mjadala wa Wizara ya Nishati na Madini unaoendelea.

Kutokana na hali hiyo Mnyika alimtaka Spika kuchukua hatua kwa mbunge aliyesema kuwa yeye ni mwizi lakini Spika akasema hajui hilo na haijaingia kwenye hansadi. Hata hivyo Mnyika alisisitiza kuwa mambo hayaweze kwenda hivyo.

Baada ya majibizano kati yake na Spika, Spika akaamuru walinzi wamtoe Mnyika nje ya Bunge na asihudhurie vikao saba vinavyofuata.

Mnyika alikuwa akitoa maelezo baada ya Mbunge wa Mtera, Livingston Lusinde kusema upinzani wa Tanzania ni wa ajabu kwani unatetea wezi wa madini.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...