Tuesday, November 12, 2013

BODI YA LIGI YAFUNGIA VIWANJA SABA


Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPL Board) imefungia viwanja saba vilivyokuwa vikitumiwa na timu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) hadi vitakapofanyiwa marekebisho ili kukidhi mahitaji ya mechi za mpira wa miguu.

Uamuzi huo umefikiwa na TPL Board katika kikao chake cha kwanza kilichofanyika juzi (Novemba 10 mwaka huu) jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine kilipitia ripoti za mechi za VPL na FDL katika mzunguko wa kwanza.

Viwanja vilivyofungiwa na marekebisho yanayotakiwa kufanyika kwanza ili viruhusiwe kutumika tena ni Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba (majukwaa yake yamechakaa, hivyo kuhatarisha usalama wa watazamaji), na Uwanja wa CCM Mkwakwani jijini Tanga (vyumba vya wachezaji kubadilishia nguo (dressing rooms) havina hadhi).
Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya (sehemu ya kuchezea- pitch ni mbovu), Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha (pitch ni mbovu), Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi (vyumba vya kubadilishia kutumika kwa ajili ya shule ya awali), Uwanja wa Majimaji mjini Songea (pitch ni mbovu) na Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro (pitch ni mbovu). 

BREAKING NEWZZZZZZ...!!! DR. SENGONDO MVUNGI AMEFARIKI DUNIA AFRIKA KUSINI

Sengondo Mvungi 1 
Ni jana tu ambapo Waziri wa mambo ya ndani Dr. Emmanuel Nchimbi alitangaza kushikiliwa kwa watu tisa wanaotuhumiwa kuhusika na ujambazi uliofanywa dhidi ya Dr. Sengondo Mvungi aliekua mjumbe wa Tume ya Marekebisho ya Katiba Mpya na kiongozi wa NCCR-Mageuzi.
Taarifa iliyotumwa inasema Dr Mvungi amefariki dunia akiwa mahututi hospitalini nchini Afrika Kusini muda mfupi uliopita na taarifa kutumwa nyumbani Tanzania ambapo wafanyakazi wenzake ofisi ya tume ya mabadiliko ya katiba wameambiwa wakae karibu na simu zao ili kikitokea chochote kingine wafahamishwe.
Tayari viongozi mbalimbali kama Mh. Warioba, Katibu wa tume, naibu na watumishi wengine wachache wamekwenda nyumbani kwa marehemu.
kifo cha Sengondo Mvungi Nov 12 2013 2

Pichani ni Wafanyakazi wenzake baada ya kupata taarifa za msiba ofisini.



kifo cha Sengondo Mvungi Nov 12 2013

Chanzo: millardayo.com

MSIMU WA SIKUKUU UMEWADIA TANGAZA BIASHARA YAKO NASI KWA BEI NAFUU



MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 12, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.

ZAIDI YA WATU 10,000 WAHOFIWA KUFARIKI UFILIPINO


017217323_35400_2f32e.jpg
Wanajeshi na polisi wa Ufilipino wamepelekwa katika miji ilioathirika na kimbunga kikali kuwahi kuipiga nchi hiyo ili kudhibiti wizi wa mali unaohatarisha juhudi za kutoa misaada ya kibinaadamu kwa waathirika.
Zaidi ya watu 10,000 wanahofiwa kufariki kutokana na kimbunga hicho kwa jina Haiyan kilichopiga kwa mawimbi mazito na upepo mkali na kusababisha athari kubwa nchini Ufilipino siku ya Ijumaa, huku mji wa Tacloban ukiwa moja ya miji ilioathirika pakubwa.
Waokoaji kwa sasa wanajaribu kupeleka misaada ya chakula na malazi kwa waathirika wa kimbunga hicho katika mji huo ulio na idadi ya watu 220,000.
Hata hivyo hatua hiyo iliendeshwa kwa changamoto kubwa kutokana na wizi uliokuwa ukiendelea. Waporaji walivunja maduka pamoja na kuvamia gari la misaada la msalaba mwekundu na kuchukua vile vilivyokuwemo ndani.
Baadhi ya waathiriwa ambao ni wafanyabiashara wadogo pia wameripoti kuibiwa kwa televisheni, na mashini za kufulia nguo. 
Kulingana na msemaji wa wizara ya ulinzi wa raia nchini humo, Reynaldo Balido, kurejesha usalama na hai ya utulivu katika mji huo wa Tacloban, ni moja ya mambo wanayoyapa kipaumbele.

KIONGOZI WA MSAFARA WA RAIS AKUTWA NA ZAIDI YA KILO 297 ZA DAWA ZA KULEVYA

558644_610253689038629_153892185_n_a1d1b.jpg
KASHFA NZITO LIBERIA: Msafara wa Rais Ellen Johnson Sirleaf wakutwa na zaidi ya kilo 297 za bangi. Watu 4 akiwemo kiongozi wa msafara washikiliwa kwa mahojiano.
== Liberia's Drug Enforcement Agency has arrested the head of the presidential motorcade for allegedly using an official vehicle to smuggle 297 kilograms (654 pounds) of marijuana into Liberia from neighboring Sierra Leone, officials said Monday.
The motorcade commander, Perry Dolo, was arrested over the weekend along with three other men after crossing from Sierra Leone via the town of Bo Waterside, said DEA Director Anthony Souh. The other three men were a Liberian official, a Guinean and a Sierra Leonean believed to be a member of the armed forces, Souh said. He did not provide further details about the men.
The vehicle used in the operation is known as "Escort 1," the jeep that normally leads the president's convoy, Souh said.
"He took the car during his day off to go do this thing. He was not on duty, but he used the official car," Souh said of Dolo.
Journalists were denied access to the suspects because they were still being interrogated at the DEA after their arrest by a joint force that included members of the Emergency Response Unit.
"They are still with me going through the process," Souh said. "We want to speedily send them to court as soon as possible because the case is too high. Using a presidential car? It's too big."
Liberia's DEA has in recent years tried to combat marijuana farming in Liberia's interior counties, which is primarily done for local sale and consumption. However, weak drug laws have made the practice difficult to curtail.
According to the 2012 World Drug Report from the United Nations Office on Drugs and Crime, 9 percent of Liberian high school students use cannabis.
———
abc News

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...