Thursday, October 31, 2013

WAPINZANI KUSIMAMISHA MGOMBEA MMOJA 2015

mbatia-k1 596f0
UPEPO wa mabadiliko ya kisiasa unaovuma kuelekea kambi ya upinzani, sasa unaonekana kuwaamsha viongozi wa vyama hivyo baada ya kutolewa kwa taarifa kuwa wanafikiria kusimamisha mgombea mmoja wa urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.


Taarifa zilizolifikia gazeti hili kabla ya kuthibitishwa na mmoja wa viongozi hao, zilieleza kuwa hatua ya vyama hivyo imekuja baada ya ushirika wao waliouunda kupinga upungufu uliokuwemo kwenye Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba kuzaa matunda.
Pamoja na hilo, inaelezwa kuwa maamuzi hayo magumu ya wapinzani yametiwa chachu na kauli aliyoitoa Rais Jakaya Kikwete ya hivi karibuni ya kukitabiria anguko Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika uchaguzi wa mwaka 2015 au ule wa 2020, kutokana na kile alichodai kuwa viongozi wa chama hicho kuendekeza rushwa.
Mmoja wa viongozi wanaounda ushirika huo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia alithibitisha taarifa hizo huku akisisitiza kuwa nia ya kufanya hivyo ni kuhakikisha wanaiondoa madarakani CCM mwaka 2015.
Kwa mujibu wa Mbatia, walichokifanya kwenye Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba si nguvu ya soda na badala yake wataendeleza hadi kwenye uchaguzi mkuu ujao.

ANGALIA PICHA ZA MAZISHI YA BABA YAKE WEMA SEPETU YALIYOONGOZWA NA RAIS WA ZANZIBAR DR ALI MOHAMMED SHEIN



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, alipokuwa akiuaga Mwili wa Marehemu Balozi Isaac Sepetu, katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani, Mnazi mmoja Mjini Unguja

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akimpa pole Mjane wa Marehemu Balozi Isaac Sepetu,Mama Miriam Sepetu,alipofika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani,Mnazi mmoja Mjini Unguja, kuuaga mwili wa Marehemu.
Ibada ya Kuuombea Mwili wa Marehemu Sepetu  ikiendelea kwenye Kanisa la Minara Miwili Zanzibar
Baadhi ya watoto wa marehemu Balozi Sepetu wakisikiliza neno la mungu
Wema Sepetu(Aliyesimama Kushoto) akiwa kanisani kwenye maombezi ya baba yake mzazi 

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS OKTOBA 31, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

Q-CHILA "NIMEOTESHWA NDOTO YA USHINDI KUWA PAPII KOCHA ATARUDI URAIANI"

Muimbaji wa Beautiful, Q-Chilla amesema ameota ndoto kuwa Papii Kocha na baba yake Nguza Viking aka Babu Seya wataachiwa huru.

Leo, Jumatano, jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani nchini Tanzania limeipitia upya hukumu yao.

“Nimeota ndoto ya ushindi, nimemuona Papii Kocha Sinza anakatiza barabara. Naotaga mara chache sana na huwa vitu vinatokea. Iko wazi kaka yangu anarudi uraiani. Nimemuona, welcome home, dunia ilikumiss, vita imekwisha,” Q-Chilla ameimbia Bongo5.

“Let the world know that the beloved kid is coming home.”

Katika rufaa hiyo leo wakili wa Babu Seya na Papii Kocha ameiomba mahakama hiyo ifute ushahidi na waachiwe huru lakini serikali imepinga. Kutokana na hatua hiyo, leo mahakama ya rufaa haijafanya uamuzi wowote imewapiga kalenda.

Nguza Viking na Papii Kocha wanatumikia kifungo cha maisha jela kwa makosa ya kubaka na kulawiti watoto wadogo wa shule ya msingi.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...