Thursday, April 20, 2017

TFDA YAPOKEA MAOMBI 767 YA VIWANDA VIPYA

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Chakula na Dawa(TDFA), Hiiti Sillo amesema kuanzia Machi mwaka huu taasisi yake ilimepokea maombi mapya ya usajili wa viwanda 767.

Amesema katika maombi hayo, viwanda 635 vipya vimesajiliwa kati ya hivyo, 613 vya chakula, kimoja cha dawa na 21 vya vipodozi akisema hiyo ni asilimia 82.8 ya maombi yote jambo linaloashiria kwamba waombaji wengi wanazingatia sheria.

Amesema katika kipindi hicho TFDA ilifanya tathmini ya maombi 4,762 sawa na asilimia 82.1 ya usajili wa bidhaa za dawa, chakula, vifaatiba na vipodozi, kati ya maombi 5,802 yaliyowasilishwa na 4,322 (75%) yaliidhinishwa na 440 yalikataliwa kwa kutokidhi vigezo vya ubora.

Sillo ameeleza hayo leo kwenye mkutano na wahariri wa vyombo vya habari walipokutana mkoani Tabora.

'UPINZANI HAUNINYIMI USINGIZI' MUGABE

Viongozi wawili wa vyama vya upinzani nchini Zimbabwe wamekubaliana kuunda umoja kuwania urais kwenye uchaguzi mkuu ujao nchini humo.

Kiongozi wa Movement for Democratic, Morgan Tsvangirai na aliyekuwa makamu wa rais wa nchi hiyo Joice Mujuru wa National people's Party walitia saini makubaliano hayo siku ya Jumatano.

Rais wa nchi hiyo Robert Mugabe awali alitoa maneno ya dhihaka kutokana na mipango ya upinzani aliyodai kuungana kumuondoa madarakani.
Morgan Tsvangirai na Joice Mujuru wameonekana kumaliza baadhi ya tofauti zao.Tsvangirai anasema makubaliano yaliyotiwa saini baina ya vyama viwili ni msingi kuelekea kuunda umoja wa vyama kwa ajili ya kupambana na chama tawala Zanu PF.

Changamoto iliyopo hivi sasa ni kuamua nani kati ya hao wawili ataongoza muungano huo.

Tayari, vyama vingi vidogo vya upinzani vimemuidhinisha Morgan Tsvangirai kuwa mgombea wao wa urais.

Kiongozi wa miaka mingi madarakani Robert Mugabe , alieleza kuwa upinzani umejaa watu wasio na kitu vichwani.

Amesema hakosi usingizi kwa kile kinachoitwa umoja wa wapinzani.

MADAKTARI 258 WALIOKUWA WAKAAJIRIWE KENYA, SASA KUAJIRIWA NCHINI

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu

Madaktari 258 ambao walikidhi vigezo vya kwenda kufanya kazi nchini Kenya, sasa wataajiriwa na serikali ya Tanzania kutokana na kuwepo na zuio la Mahakama ya Kenya la kuwaajiri.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya Rais Magufuli kumwelekeza jana kuwa awaajiri madaktari hao pamoja na wataalam wengine wa afya 11.

Madakatari hao walioomba hizo nafasi za kwenda Kenya walikuwa 496 kati ya 500 waliotakiwa, 258 ndio wakakidhi vigezo.

Mkataba wa Tanzania na Kenya ilikuwa mpaka Aprili 6 wawe wamepatikana hao madaktari na kati ya Aprili 6 mpaka 10 wasafirishwe kwenda Kenya, sasa baada ya kuajiriwa na serikali, Kenya wakiwa tayari na kuhitaji tena madaktari  watatafutiwa wengine.

Sunday, April 16, 2017

MABWENI MAPYA YA UDSM KUHUDUMIA WANAFUNZI 3840

Mabweni mapya ya wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yana uwezo wa kuchukua jumla ya wanafunzi 3,840 kwa uwiano wa wanafunzi 192 kwa kila jengo.

Akizungumza leo wakati Rais John Magufuli akizindua mabweni hayo, Makamu Mkuu  wa Chuo hicho, Profesa  Rwekaza Mukandala, mabweni hayo ni mjumuiko wa majengo 20 yenye ghorofa nne kila moja na vyumba 12 kwa kila ghorofa.

Profesa Mukandala amemwambia Rais  Magufuli kuwa chuo chake kimechangia ujenzi wa mabweni hayo kwa kutengeneza vitanda 1920, makabati 1920, droo 1920, meza 1920, viti 3,840 na magodoro 3,840.

JAMBO TZ TUNAWATAKIA PASAKA NJEMA WAKRISTO WOTE.



Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...