Tuesday, July 04, 2017

MAGUFULI AZITAKA NGO'S ZINAZOTETEA WANAFUNZI WENYE MIMBA WAFUNGUE SHULE ZAO

Rais John Magufuli amezitaka Asasi za Kiraia (NGO’s) kufungua shule kwa wanafunzi wanaopata mimba shuleni kama kweli zinawapenda wanafunzi hao.

Rais ameyasema hayo leo (Jumanne, Julai 4) alipokuwa akihutubia wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji Sengerema.

“Si kwamba nawachukia wenye mimba, hata kwa bahati mbaya akapata mimba, kama hizo NGO zinawatetea sana, zifungue shule za wenye mimba, kwa sababu zinawapenda wenye mimba, wafungue shule zao,”amesema Rais leo.

Amesema hata hao wanaofanya makongamano ya kuhamasisha watu wapate mimba wafungue shule zao kwa ajili ya wanafunzi hao.

“ Haiwezekani fedha za walipa kodi, Sh 17 bilioni kila mwaka za kusomesha watoto wetu, kwenda kusomesha wakinamama, wazunguke, waimbe, waseme nini mimi ndiyo Rais, huo ndio ukweli,” amesema.

Amesema tatizo si wanaopata mimba, kwani wapo waliopata matatizo, kama kuugua kwa muda mrefu wakashindwa kwenda shule lakini ulianzishwa mpango maalum wa kuwasomesha katika mfumo usio rasmi.

KINGA YA UKIMWI YAANZA KUONESHA MAFANIKIO

Utafiti wa kinga ya kuzuia maambukizi ya virusi vya  Ukimwi, ulioanza kufanywa nchini miaka kadhaa iliyopita umeana kuonyesha mafanikio.

Lakini watafiti wamesema Watanzania watahitaji kuwa uvumilivu wa miaka michache ijayo kusubiri hatua za mwisho za ukamilishaji utafiti wa kinga hiyo kabla haijaanza kutimika rasmi.

Taarifa hizo zinakuja ikiwa wiki moja baada ya Kenya kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kuanza kutumia dawa ya ugonjwa wa Ukimwi ambayo inaweza kuboresha afya na kurefusha maisha ya maelfu ya watu ambao wanasumbuliwa na magonjwa nyemelezi na ambayo hayakubali tiba nyingine.

Kwa miaka kadhaa  Chuo Kikuu cha Afya na Tiba Muhimbili (MUHAS) imekuwa ikiendesha utafiti kuhusiana na chanjo ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi na katika hatua ya awali utafiti huo uliwahusisha baadhi ya watu wanaishi na virusi hivyo.

TIMU YA SINGIDA UNITED YAONESHA JEURI YA PESA, YANUNUA BASI LA MILLION 350/-

Baada ya kupata udhamini mnono kutoka katika kampuni ya michezo ya kubashiri ya SportPesa hatimaye klabu ya Singida United inazidi kutanua misuli yake katika ligi kuu ya Tanzania Bara kwa kutambulisha usafiri wao utakao tumika katika kusafirishia wachezaji.
 Akizungumza na waandishi wa habari jana katibu Mwenezi wa klabu hiyo Festo Sanga amethibitisha Singida United kununua Basi jipya lenye gharama ya shilling milioni 350.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...