Saturday, October 12, 2013

HUU NDIO UTARATIBU MPYA WA KUINGIA MLIMANI CITY BAADA YA KUTOKEA UVAMIZI WESTGATE

 
 Kijana akikaguliwa kwa umakini baada ya kutiliwa mashaka na walinzi wa Mlimani City leo mchana
 
 Mlinzi wa kike akiwasubilia wananwake watakaotaka kuingia kwenye jengo la mlimani city ili hawakague
Ukaguzi ukiendela
PICHA NA PAMOJAPURE/PAMOJA BLOG

STEWART ADAI SIMBA NA YANGA ZINABEBWA NA TFF


Hall1 1eb67
KOCHA Mkuu wa Azam FC, Muingereza Stewart Hall amesema kwamba ni kazi ngumu Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kupata bingwa nje ya Simba na Yanga kwa sababu timu hizo zinapendelewa mno na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).



Akizungumza Hall amesema kwamba timu nyingine nje ya Simba na Yanga SC ili kuwa bingwa inabidi ifanye kazi ngumu sana ambayo kwa sasa yeye na timu yake, Azam FC wanajaribu.
Kwanza amesema ratiba ya Ligi Kuu inapopangwa inakuwa katika mazingira mazuri kwa timu hizo na mazingira magumu kwa timu nyingine ambazo zinaonekana zikitendewa haki zinaweza kuzima ubabe wa timu hizo katika soka ya Tanzania.
Stewart alitoa mfano hadi sasa katika mechi za Ligi Kuu ambazo tayari zimechezwa, Simba na Yanga kila moja imecheza mechi mbili tu ugenini, wakati Azam FC imecheza mechi sita ugenini, jambo ambalo amesema huwezi kulikuta katika ligi nyingine yoyote duniani.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI, OKTOBA 12, 2013

DSC 0092 59997
DSC 0093 e41e4

RIPOTI YA UN: YAIANIKA SERIKALI, YADAI WATANZANIA NI WATU WASIO NA FURAHA


saada_35554.jpg
Naibu waziri wa fedha, Saada Salum
Wakati Tanzania ikitajwa kuwa ni miongoni mwa nchi zenye amani na utulivu, imebainika kuwa Watanzania ni miongoni mwa watu wasio na furaha na waliokata tamaa hapa duniani.
Ripoti inayoonyesha orodha ya nchi zenye furaha duniani ya mwaka 2013 (World Happiness Report 2013), imeitaja Tanzania kuwa ni miongoni mwa nchi 10 za mwisho duniani kati ya nchi 156 zilizofanyiwa utafiti huo.
Ripoti hiyo iliyoandaliwa na kundi la wataalamu kutoka Umoja wa Mataifa (UN), kati ya mwaka 2010 na 2012, inaonyesha kuwa Tanzania imeshika nafasi ya 151 ikiburuta mkia pamoja na nchi za Rwanda, Burundi, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Benin na Togo.
Upatikanaji wa huduma za jamii, mtazamo wa watu kuhusu rushwa, umri wa kuishi, ukosefu wa kazi, pato la taifa na ukarimu wa watu katika nchi husika, ni baadhi ya vigezo vilivyoangaliwa wakati wa kuandaa taarifa hiyo.
Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka alieleza kushtushwa na ripoti hiyo kwa maelezo kwamba ni asilimia 11.7 tu ya Watanzania wasio na ajira na kwamba wale wanaofanya kazi, wanapata huduma zote za msingi, ikiwa ni pamoja na kwenda likizo na mishahara inayolingana na taaluma zao.

GARI LA SERIKALI LAKAMTWA LIKITUMIKA KWENYE UTAPELI

2135728_orig_459dd.jpg
Jeshi la Polisi mkoani Temeke, linamshikilia dereva wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, aliyefahamika kwa jina la Bw. Samwel Mulagalazi, ambaye anadaiwa kushirikiana na watu wawili waliotaka kumtapeli mteja wa Shirika la Umeme nchini (TANESCO), sh. milioni 60.
Tukio hilo limetokea juzi saa 11 jioni katika kiwanda kilichopo Mbagala, Dar es Salaam (jina tunalo), ambapo matapeli (vishoka), waliojifanya wafanyakazi wa TANESCO, Makao Makuu, Ubungo, walitaka kufanya utapeli huo kwa mmiliki wa kiwanda hicho.
Matapeli hao walimpigia simu mmiliki wa kiwanda hicho (jina tunalo), wakidai kiwanda chake kinaiba umeme hivyo walimtaka atoe sh. milioni 60 asiweze kukatiwa umeme.


Mmiliki huyo akitambua kuwa mita zake hazikuwa na tatizo lolote na hahusiki na wizi huo, aliwasiliana na Meneja wa TANESCO wilayani Temeke, Mhandisi Richard Mallamia na kumweleza vitisho alivyopewa na matapeli hao na pesa waliyotaka kupewa.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...