Thursday, February 13, 2014

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS FEBRUARI 13, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS



Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

TOYOTA YATOA AGIZO LA KUREJESHA MAGARI KIWANDANI...!!!

prius22_b3ff7.jpg
Kampuni ya kutengeza magari ya Toyota nchini Japan, imeagiza kurejeshwa kwa magari milioni 1.9 aina ya Prius katika kiwanda cha magari hayo nchini Japan.
Hii ni kutokana na hitilafu ya kimitambo ambayo inaweza kusababisha gari hilo kukwama.
Gari la Prius ni moja ya magari yenye muundo unaonyesha ubunifu wa hali ya juu wa kampuni ya Toyota.
Gari hilo linaweza kutumia petroli na betri huku likitoa kiwango kidogo sana cha moshi kuliko magari ya kaiwada.
Sasa kampuni hiyo imetambua hitilafu ya programu ya gari hilo ambayo inaweza kusababisha vifaa vya elektroniki vya gari hilo kukwama.
Magari mengi yenye hitilafu hiyo yako nchini Japan na Amerika ya Kaskazini na Toyota inasema kuwa haijapokea taarifa zozote za ajali au majeraha kutokana na hitilafu hiyo. CHANZO BBC
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

KAULI YA ZITTO KABWE KUHUSU MADAI YA WAFANYABIASHARA NA TRA...!!!

Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia Chadema Zitto Kabwe muda mfupi uliopita kupitia kwenye ukurasa wake wa Facebook ametoa yake ya moyoni kwa hili seke seke linaloendelea nchini juu Wafanyabiashara na Mamlaka ya Mapato Tanzania[TRA]kuhusu mashine za kutolea risiti za EFD.
Zitto alianza kwa kuandika>>’EFD zilianza kutumiwa mwaka 2010 kwa jumla ya wafanyabiashara 16,000 waliosajiliwa kwenye Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT). Mwaka wa fedha 2009/2010, kabla ya EFD, makusanyo ya kodi ya VAT yalikuwa tshs 791 bilioni’
‘Mwaka 2011/2012 makusanyo yaliongezeka kwa asilimia 40 mpaka tshs 1,086 bilioni. Mwaka 2012/2013 makusanyo yakaongezeka kwa asilimia 63 mpaka kufikia tshs 1,770 bilioni. Makusanyo haya ni kwa Wafanyabiashara 16,000′
‘Iwapo awamu ya pili ya EFD itatekelezwa bila vikwazo jumla ya Wafanyabiashara 200,000 watafikiwa ikiwemo ni pamoja na vituo vya mafuta (Petrol Stations), Mahoteli na Migahawa nk. Mamlaka ya Mapato inatarajia kukusanya zaidi ya tshs 3,500 bilioni kutoka VAT peke yake iwapo EFD zitatumika’
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

GHASIA ZAONGEZEKA JAMHURI YA AFRIKA YA KATI

dede_d2268.jpg

Takriban wanajeshi 1,600 wa Ufaransa na 6,000 wa Umoja wa Afrika wamo nchini humo kujaribu kulinda raia wakati ghasia zenye maafa zikiendelea kati ya Wakristo na Waislam.
Waziri wa ulinzi wa Ufaransa anasema lazima tahadhari zichukuliwe ili Jamhuri ya Afrika ya Kati isigawanyike. Onyo hilo limetolewa huku makundi ya kutetea haki za binadamu yakionya kuwa mauaji ya kikabila yanaendelea katika taifa hilo lililokumbwa na mgogoro wa kisiasa.
Waziri huyo Jean Yves Le Drian alifanya mazungumzo mjini Bangui na maafisa wa ngazi ya juu ya jeshi la Ufaransa pamoja na kaimu rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati Catherine Samba- Panza aliyeungana naye wakati wa ziara yake kusini magharibi mwa nchi.
Hii ni mara ya tatu kwa waziri Le Drian katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, tangu Ufaransa ilipozindua operesheni ya kijeshi mwishoni mwa mwaka jana. Onyo lake limetolewa huku makundi mawili ya kutetea haki za binadamu Amnesty International na Human Rights Watch yakionya juu ya mauaji ya kikabila katika baadhi ya maeneo ya nchi yanayolenga waislam walio wachache.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...