Wednesday, June 12, 2013

KIFO CHA KASHI...YALIYOTABIRIWA NA MCHUNGAJI YAMETIMIA

Marehemu Jaji Hamisi ‘Kashi’.

KIFO cha msanii wa siku nyingi  katika tasnia ya filamu za Kibongo, Jaji Hamisi ‘Kashi’ kilichotokea Jumatatu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kimehitimisha maono ya mchungaji aliyetabiri kuwa mastaa wawili mmoja wa Bongo Fleva na mwingine wa Bongo Movie watafariki dunia ndani ya mwaka huu.

Marehemu Albert Mangwea.
TAARIFA ZA KIFO
Saa 5 asubuhi taarifa za kifo zilitua katika chumba chetu cha habari na haraka waandishi wetu wakafika nyumbani kwa baba mzazi wa msanii huyo Kinondoni Mkwajuni jijini Dar es Salaam na kuwashuhudia waombolezaji wakiangua vilio kufuatia kifo cha mpendwa wao huyo.
Akizungumza na paparazi wetu rafiki wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Mwamtoro Mzura alisema wiki mbili kabla ya kifo hicho, Kashi akiwa anaendesha gari maeneo ya Karume, Ilala jijini Dar alikosea njia na kwenda kujikita kwenye ukingo wa barabara na kuumia miguu.
“Baada ya kupata ajali hiyo alikimbizwa Hospitali ya Amana na kupatiwa matibabu, kisha akaruhusiwa kurudi nyumbani, kuanzia siku hiyo hali yake ilianza kudhoofu,” alisema.
Mwamtoro alisema kuwa Ijumaa iliyopita hali yake ilibadilika na kuwa mbaya, hivyo akakimbizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kupatiwa matibabu hadi Jumatatu iliyopita alipoaga dunia.

MASTAA WAFURIKA NYUMBANI KWAKE
Jacqueline Pentzel ‘Jack wa Chuz’, Sabrina Rupia ‘Cathy’, Mayasa Mrisho ‘Maya’, Seif Mbembe, Herieth Chumila, Happy Nyatawa ambaye alikuwa na marehemu katika Kundi la Shirikisho la Msanii Afrika.
Mastaa hao walinaswa na mapaparazi wetu nyumbani kwa baba mzazi wa Kashi.

TANGAZO LA MAFUNZO YA UALIMU DARAJA 'A' NA STASHAHADA MWAKA 2013/2014

clip_image002
Nafasi za Mafunzo ya Ualimu Ngazi ya Cheti Daraja A na Stashahada kwa mwaka wa masomo 2013/2014.
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi anawatangazia Wahitimu wa Kidato cha Nne mwaka 2012 na Kidato cha Sita mwaka 2013 kuwa muda wa kupokea maombi kwa ajili ya mafunzo ya Ualimu ngazi ya Cheti na Stashahada mwaka wa masomo 2013/2014 umeongezwa mpaka tarehe 28/06/2013.
Sifa za mwombaji ni kama zilivyoainishwa katika tangazo la Wizara lililopo katika tovuti ya Wizara www.moe.go.tz linalohusu “Nafasi za Mafunzo ya Ualimu Ngazi ya Cheti Daraja A na Stashahada kwa mwaka wa masomo 2013/2014”.Bofya hapa
Aidha, wahitimu wa kidato cha Sita kuanzia mwaka 2008 hadi mwaka 2013 wanahimizwa kutuma maombi yao.
Barua za maombi zioneshe Jina na anuani kamili ya mwombaji na kuambatisha nakala ya matokeo yake ya mtihani (wahitimu wa Kidato cha Nne 2012 na Kidato cha Sita 2013 waambatishe ukurasa wenye matokeo yao kutoka Baraza la Mitihani la Tanzania Au kuonesha namba yake ya mtihani)

Maombi yatumwe kwa:-

Katibu Mkuu,  

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi,

S.L.P.9121,

DAR ES SALAAM 

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

SUGU AFUNGUKA KUHUSU WAUZA UNGA WANAVYO WATUMIA WANAMUZIKI KUBEBA UNGA


USHUHUDA WA SUGU 
Ukweli wa jinsi matajiri wauza unga wanavyowatumia wanamuziki wa Kitanzania kama punda, unapewa nguvu na ushuhuda aliowahi kuutoa Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’. Mbunge huyo ambaye anapewa heshima kwamba ni mmoja wa waasisi wa Bongo Fleva, alimweleza mwandishi wetu kuwa kabla hajawa memba wa jumba hilo la kutunga sheria, aliwahi kufuatwa na wauza unga kumshawishi awe anabeba mzigo kwenda nao nje ya nchi.
 
 “Jamaa waliniambia kwa sababu mimi nasafiri safiri sana, passport (hati ya kusafiria) yangu itakuwa imeshagongwagongwa sana, kwa hiyo ni rahisi kwenda nchi tofautitofauti kwa urahisi, kwa hiyo wakataka niwe nabeba unga. “Kigezo cha pili waliona kwa sababu mimi ni mwanamuziki,
kwa hiyo ni rahisi watu kuamini ziara zangu ni za kimuziki. Nilikataa, niliwaambia siwezi kufanya biashara hiyo kabisa,” alisema Sugu.
 
 Mwaka 2011, mbunge huyo aliwahi kugusia hilo, wakati akitoa hoja kuchangia bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kuwa serikali ni lazima iwasaidie wanamuziki wa Kitanzania kwa sababu wanaibiwa sana, hivyo kuwafanya vijana kuona kimbilio rahisi la kutajirika ni kuuza madawa ya kulevya. “Mheshimiwa spika, serikali isifanye ili kijana wa Kitanzania afanikiwe lazima auze unga, madawa ya kulevya,” alisema Sugu na kueleza mfano huo wa jinsi alivyofuatwa kushawishiwa na matajiri wa unga ili naye awe punda.

WASTARA AKIRI KUTOKEWA NA MZIMU WA SAJUKI KITANDANI...!!

SIKU chache baada ya staa wa sinema za Kibongo, Wastara Juma kumaliza eda na kurejea Bongo akitokea Uarubuni ameanza kuona maruweruwe ndani ya chumba alichokuwa akilala na mumewe marehemu, Sadick Juma Kiwoloko  ‘Sajuki’, Risasi Mchanganyiko lina habari za uhakika.
 
 
Wastara Juma akiwa na mumewe Sadick Juma Kiwoloko ‘Sajuki’ enzi za uhai wake.
 
Kwa mujibu wa Wastara siku hiyo akiwa amelala chumbani humo, usiku wa manane alihisi uwepo wa Sajuki kitandani kwake.
“Niliongea naye kwa kweli siwezi kukumbuka haswa ni nini tulichoongea lakini tulikuwa katika hali ya furaha sana,” alisema Wastara.
Pia, Wastara alisema kuwa wakiwa katika maongezi yao, aliuchukua mkono wake na kuuweka juu ya mwili wa Sajuki katika hali ya mapenzi na akapitiwa na usingizi.


“Asubuhi nilipoamka nilihisi kama nilikuwa na Sajuki  pale kitandani, kuangalia vizuri, mkono wangu ulikuwa juu ya shuka badala ya mwili wa Sajuki,” aliongeza.
Hata hivyo, Wastara alisema kuwa alihisi ni ndoto lakini alipochunguza alihisi kama kulikuwa na mtu aliyekuwa amelala naye pale kitandani.
“Sijui kama ni maruweruwe, ndoto au Sajuki alikuja kweli kitandani kwangu, kikubwa ninachokiamini ni kwamba mapenzi kwa marehemu mume wangu ndiyo yamepelekea hali hiyo,” alisema

FAMILIA YAMKATAA MTOTO WA NGWEA....!!!

SIKU chache baada ya aliyekuwa mkali wa Hip Hop Bongo, Albert Kenneth Mangweha ‘Ngwea’ kupumzishwa kaburini kufuatia kifo cha usingizini nchini Afrika Kusini kilichotokea Mei 28, mwaka huu, mambo kibao yanazidi kuibuka.

Habari zinadai kuwa familia ya marehemu Ngwea imemkataa mtoto aliyeletwa na mama yake makaburini akidaiwa kuwa ni mtoto wa Ngwea.
MTOTO WA NGWEA
Juni 6, mwaka huu wakati wa mazishi, mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Paulina Jeremiah, mkazi wa Kigamboni, Dodoma alitimba akiwa na mtoto huyo wa kike aitwaye Neema Albert na kudai kuwa alimzaa na Ngwea mwaka 2001, wakati msanii huyo akisoma Sekondari ya Mazengo.

Wakati akijieleza, ndugu wa Ngwea, Anthony Mangweha alikuwa akimsikiliza ambapo aliwataja wanandugu wa marehemu waliokuwa wakijua suala hilo.
Waliotajwa kujua kuwa mtoto huyo alikuwa wa Ngwea ni Frank, Jotam na Amani ambao waliwahi kutumwa na marehemu kwenda kumwangalia mkoani Dodoma.
Hata hivyo, ndugu huyo aliyekuwa akimsikiliza alimtaka mama Neema kupoa, hadi familia ikae kikao.
.
FAMILIA YAKAA KWA SAA 7, YATOA UAMUZI MZITO!
“Kweli wikiendi iliyopita familia ilikaa kikao kwa zaidi ya saa 7, pamoja na mambo mengine lakini wanadaiwa kufikia uamuzi mzito wa kumkataa mtoto huyo hadi mama Neema apeleke vigezo vya uthibitisho,” kilisema chanzo chetu ndani ya kikao hicho.
Akizungumzia suala hilo kwa sharti la kutotajwa gazetini, mmoja wa dada zake Ngwea alisema: “Ni kweli yule mtoto aliondoka na mama yake lakini kama akileta uthibitisho tutampokea.”

MWANAMKE AFUNGWA MIAKA 3 KWA KOSA LA KUMNG'ATA MUMEWE SEHEMU ZA SIRI HUKO IRAMBA SINGIDA ...!!!

 
MAHAKAMA ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida umemhukumu mwanamke mmoja mkazi wa kijiji cha Kisana wilayani humo, Sayuni Ramadhani (42) kwenda jela miaka mitatu baada ya kukiri kosa la kumng’ata mumewe sehemu zake za siri.

Mwendesha mashitaka mkaguzi wa polisi, Vincent Ndasa alidai mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Iramba, Kariho Mrisho kuwa Juni 4 mwaka huu saa 12.00 jioni katika kijiji cha Kisana, mshitakiwa kwa makusudi alizing’ata kwa meno sehemu za siri za mume wake, Onesmo Nathania (42) na kumsababishia maumivu.
Ndasa alidai kuwa siku ya tukio, wanandoa hao waliporejea nyumbani kutoka kwenye klabu cha pombe ya kienyeji kijijini hao, kulitokea kutokuelewana na hivyo kuanza kugombana.

WASANII WA MOVIE WANASWA WAKIFANYA MAPENZI VICHAKANI


Chipukizi wawili wa filamu za Kibongo, Tabasamu Mohamed na Neema Ibrahim, walikutwa ‘laivu’ wakifanya mambo ya chumbani hadharani.

Hili ni tukio la aina yake lililowahi tikisa bongo movie kati ya mwaka 2011/ 2012.......

Tangu mwaka jana kumekuwa na mfumuko wa kasi kwa wasanii wa kibongo kupiga picha za utupu na kuzisambaza mitandaoni huku wengine wakijiuza live...!!!


Awali wasanii hao walishuhudiwa wakiwa karibu kimahaba ambapo walikwenda kukaa chini ya mti na kuanza ‘kudendeka’ kabla ya kuzama katika hatua mbaya zaidi ya kutomasana na kuvuana nguo bila kujali kuwa ilikuwa mchana tena hadharani.


Inasikitisha sana kuona binadamu wa leo tukifanya mapenzi kama wanyama wa porini..Huu ni ushamba..!!

MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNI 12, 2013

1 84bff
2 d40ab
10 ac447

ANGALIA PICHA ZA LWAKATALE ALIVYOPATA DHAMANA JANA

Mkurugenzi wa Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilfred Lwakatare akiingia katika chumba cha ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo, kabla ya kupata dhamana katika kesi yake inayomkabili ya kula njama ya kutaka kumzuru kwa sumu Mhariri wa gazeti la wananchi.

Wilfred Lwakatare akiwa na furaha pamoja na wakili wake baada kupata dhamana katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni mshtakiwa wa pili katika kesi inayomkali akiwa amerudi rumande baada ya kushindwa kukamilisha masharti ya dhamana.

IGP MWEMA AKUTANA NA MAASKOFU KATOLIKI JIMBO KUU DAR

 
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Said Mwema akiwa na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki nchini Kardinali Pengo wakiingia katika ukumbi wa mkutano wakati wa kikao cha Mashauriano kati ya Jeshi la Polisi na viongozi wa makanisa ya kikatoliki uliofanyika jijini Dar es Salaam.(Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi)
Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Dar es Salaam Mwadhama Kardinal Pengo amesema viongozi wa dini hawawezi kukwepa jukumu lao la kuhakikisha kuwa uhalifu unapungua hapa nchini kwa kuwa jukumu hilo linaanzia kwao.
Pengo alisema kuongezeka kwa uhalifu ni changamoto kwa viongozi wa dini kwa kuwa wao ndio wenye kazi ya kujenga maadili katika jamii na polisi kusimamia sheria na kuwachukulia hatua wale wanaokaidi
Hayo yalisemwa wakati wa kikao cha mashauriano kati ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Said Mwema vongozi wa dhehebu la Romani Katoliki uliofanyika jijini Dar es Salaam .
Naye Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Dar Es Salaam, Mhashimu Eusebius Nzigilwa akisoma maazimio yaliyofikiwa katika kikao hicho alisema wamekubaliana kuziimarisha kamati za ulinzi na usalama katika nyumba za ibada zilizopo hivi sasa wakati wakiendelea kupata mafunzo ya ukamataji salama kutoka Jeshi la Polisi.
“Parokia ambazo hazijaunda kamati za ulinzi na usalama zihakikishe zinafanya hivyo ndani ya mwezi huu na zile ambazo zimeundwa lakini hazifanyi kazi mziimarishe ili kwa pamoja tuwe salama katika nyumba zetu za ibada”Alisema Askofu Nzigilwa.

Katika mazungumzo hayo IGP Said Mwqema alisema kwamba Viongozi wa dini wana nafasi kubwa katika jamii ya kupunguza uhalifu kwa kuwa wao wanauwezo wa kuwabadili watu kimatendo na kifikra  kwa kufanya doria ya mwili na roho kwa pamoja hivyo wanaweza kusaidiana na Polisi katika kupunguza
uhalifu.

NIKIFA ASHA BARAKA ASIJE KWENYE MAZISHI YANGU- ALLY CHOKI

ALLY CHOKI ATOA KAULI NZITO: “NIKIFA ASHA BARAKA ASIJE KWENYE MAZISHI YANGU” … “Katika watu nisiowapenda kabisa ni Asha na Baraka Msilwa” 

ASHA BARAKA NAYE AJIBU MAPIGO: “HAYO NI MAMBO YA KIKE” …“Wamanyema peke yake wanatosha kunizika, amtaka Chocky akapime kwanza
MKURUGENZI wa Extra Bongo Ally Chocky ametoa kauli nzito kuhusu waajiri wake wa zamani, Asha Baraka na Baraka Msilwa.
Katika maongezi yake mahususi na Saluti5 Chocky alisema katika watu asiowapenda duniani ni Asha Baraka (Mkurugenzi wa ASET) na Baraka Msilwa (Mwenyekiti wa ASET). Asha Baraka na Baraka Msilwa ni mtu na kaka yake.

MWENYEKITI WA CCM JAKAYA KIKWETE AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM KUPOKEA RASIMU YA KATIBA MPYA

Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete, akiongoza kikao cha Maalum ya CCM ‘Kamati Kuu’ kilichokutana jana usiku mjini Dodoma kwa ajili ya kuipokea Rasimu ya Katiba mpya, iliyosomwa hivi karibuni. Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imekutana jana tarehe 10/06/2013 chini ya
uenyekiti wa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM Dr. Jakaya Mrisho Kikwete. Kikao hicho
kilikuwa cha siku moja na maalum kwa ajili ya kupokea rasimu ya katiba mpya.
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imekutana jana tareh 10/06/2013 chini ya uenyekiti wa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM Dr. Jakaya Mrisho Kikwete. Kikao hicho kilikuwa cha siku moja na maalum kwa ajili ya kupokea rasimu ya katiba mpya.
Kamati Kuu inaipongeza Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini kwa kazi nzuri na kukamilisha kazi kwa wakati.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...