Thursday, May 25, 2017

RIPOTI YA MCHANGA YAONESHA NCHI ILIVYOLIWA

 Kamati maalumu iliyoundwa na Rais John Magufuli kuchunguza mchanga wa madini, imebaini kwamba makontena 277 yaliyozuiliwa katika Bandari ya Dar es Salaam yana tani 7.8 za dhahabu yenye thamani ya kati ya Sh676 bilioni na Sh1.147 trilioni.

Rais John Magufuli akizungumza awali alisema kiwango cha juu kinaweza kufika tani 15.5.

Kiwango hicho ni tofauti na kile ambacho kamati hiyo ilielezwa na Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA), kwamba makontena hayo yalikuwa na tani 1.1 za dhahabu yenye thamani ya Sh97.5 bilioni.

Kutokana na tofauti iliyopo kati ya taarifa ya TMAA na hali halisi, kamati hiyo iliyokuwa na wajumbe wanane imebaini kwamba Taifa limekuwa likiibiwa kupitia usafirishaji wa mchanga wa madini (makinikia).

Akitoa muhtasari wa kamati hiyo Ikulu jijini Dar es Salaam jana, kabla ya kumkabidhi Rais Magufuli ripoti ya uchunguzi, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Abdulkarim Mruma alisema kamati yake ilipewa hadidu za rejea ambazo ziliwaongoza katika uchunguzi wao ambazo alizitaja kuwa ni kuchunguza makinikia yaliyopo kwenye Bandari ya Dar es Salaam, bandari kavu na migodini kwa kupekua na kubaini vilivyo ndani. Pia, kufanya uchunguzi wa kimaabara kujua aina, kiasi na viwango vya madini vinavyoonekana kwenye makinikia.

ZARI WA DIAMOND ATHIBITISHA KIFO CHA MUMEWE WA ZAMANI

Zarinah Hassan ‘ZariTheBossLady’ amethibitisha taarifa za kifo cha aliyekuwa mpenzi na baba wa watoto wake watatu, Ivan Semwanga.

Zari ametoa taarifa hzo kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram kwa kuandika,” God loves those that are special and that’s exactly who you were & I guess that’s why he wanted you to himself. You have touched and helped thousands, you did wonders and I remember you telling me “life is too short let me live it to the fullest”, this very dark hour it makes sense why you always said those words to me. To your sons, you were a hero-some kind of superman. Anyone who has ever been in your presence knows what a charming person you were. You will be missed and remembered in so many ways. You were IVAN THE GREAT! Rest in peace DON”

Kwa Kiswahili, “Mungu anawapenda wale walio muhimu na hakika ndivyo ilivyokuwa kwako, nadhani hiyo ndiyo sababu ya yeye kukuhitaji kwake. Umewagusa na kuwasaidia maelfu, ulifanya maajabu na ninakumbuka ulinambia ”maisha ni mafupi sana acha niishi kwa ukamilifu”, muda huu wenye giza ndiyo inaleta maana kwanini ulisema maneno hayo kwangu. Kwa watoto wako ulikuwa shujaa. Kila mtu aliyekuwepo sehemu ulipokuwa alijua kwa kiasi gani wewe ni mcheshi. Nitakukumbuka kwa namna nyingi. Ulikuwa IVAN THE GREAT. Pumzika kwa amani DON”

Kabla ya taarifa hiyo kulikuwa na taarifa nyingi zikisema kuwa Iavn amefariki lakini Zari alikuwa akikanusha, na taarifa za uhakika akizitoa Zari mwenyewe ambaye wamezaa watoto watatu wote wakiwa wa kiume alfajiri ya alhamisi ya Mei, 25.

RAIS WA FIFA AIPONGEZA YANGA KWA KUSHINDA UBINGWA WA VPL 2016/2017

Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Gianni Infantino ametuma salamu za pongezi kwa uongozi, wachezaji na mashabiki klabu ya Yanga kwa kuibuka washindi wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu wa 2016/2017.

Salamu za Infantino zimetumwa kwa Yanga kupitia Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na kuwa pamoja na kuwapongeza kwa ushindi walioupata pia anaitakia kila la kheri Yanga katika michuano iliyopo mbele yake.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...