Thursday, May 25, 2017

RIPOTI YA MCHANGA YAONESHA NCHI ILIVYOLIWA

 Kamati maalumu iliyoundwa na Rais John Magufuli kuchunguza mchanga wa madini, imebaini kwamba makontena 277 yaliyozuiliwa katika Bandari ya Dar es Salaam yana tani 7.8 za dhahabu yenye thamani ya kati ya Sh676 bilioni na Sh1.147 trilioni.

Rais John Magufuli akizungumza awali alisema kiwango cha juu kinaweza kufika tani 15.5.

Kiwango hicho ni tofauti na kile ambacho kamati hiyo ilielezwa na Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA), kwamba makontena hayo yalikuwa na tani 1.1 za dhahabu yenye thamani ya Sh97.5 bilioni.

Kutokana na tofauti iliyopo kati ya taarifa ya TMAA na hali halisi, kamati hiyo iliyokuwa na wajumbe wanane imebaini kwamba Taifa limekuwa likiibiwa kupitia usafirishaji wa mchanga wa madini (makinikia).

Akitoa muhtasari wa kamati hiyo Ikulu jijini Dar es Salaam jana, kabla ya kumkabidhi Rais Magufuli ripoti ya uchunguzi, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Abdulkarim Mruma alisema kamati yake ilipewa hadidu za rejea ambazo ziliwaongoza katika uchunguzi wao ambazo alizitaja kuwa ni kuchunguza makinikia yaliyopo kwenye Bandari ya Dar es Salaam, bandari kavu na migodini kwa kupekua na kubaini vilivyo ndani. Pia, kufanya uchunguzi wa kimaabara kujua aina, kiasi na viwango vya madini vinavyoonekana kwenye makinikia.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...