Friday, February 28, 2014

MASIKINI YA MUNGU MTOTO HUYUUU...!!! KICHWA NA MWILI VYAUNGANA BAADA YA KUUNGUA MOTO

MTOTO Adolotea Njavike(1.4) ambae Kichwa na Kiwiliwili vimeungana baada ya kupata na ajali ya Moto akiwa na mama yake Mzazi.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

BENKI YA DUNIA YAISIMAMISHIA UGANDA MISAADA

S_77135.png
Benki ya dunia imesitisha mkopo wa dola milioni 90 kwa Uganda wa kuimarisha sekta ya afya kufuatia kupitishwa kwa sheria inayoharamisha ushoga na kutoa adhabu kali kwa watakaopatikana na hatia
Hatua hiyo ya benki ya dunia haikutarajiwa na wengi kwani taasisi hiyo mara nyingi hujiepusha kuingilia masuala ya ndani ya kisiasa ya nchi wanachama au kuhusiana na masuala kama haki za mashoga, kuepuka kuzishurutisha nchi wanachame wake 188.
Hata hivyo msemaji wa benki hiyo David Theis amesema katika barua pepe kuwa wamesitisha mradi huo wa kuboresha sekta ya afya ya Uganda hadi watakapoufanyia tathmini na kuhakikisha malengo yake ya maendeleo hayataathiriwa na sheria hiyo mpya ya kuharamisha ushoga.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

AJALI, BASI LAGONGA TRENI, WANNE WAFARIKI

ajali_c4aaf.jpg
Basi la Bunda Express lililokuwa likitokea Dodoma kwenda Mwanza asubuhi ya leo limegonga Treni Eneo la Manyoni mkoani Singida. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

ajali1_6a6b0.jpg
Basi la Bunda Express lililokuwa likitokea Dodoma kwenda Mwanza asubuhi ya leo limegonga Treni Eneo la Manyoni mkoani Singida.
ajali3_57f09.jpg
Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka eneo la tukio kinasema kuwa watu wanne wamefariki dunia na kadhaa kujeruhiwa.
Majeruhi Tayari wamepelekwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Manyoni.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARI 28, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Wednesday, February 26, 2014

HIKI NDICHO KINACHOENDELEA MSIBANI KWA DADA YAKE LADY JAY DEE...!!!

Msanii mkongwa wa Bongo Flava Lady Jay Dee amefiwa na dada yake Aitwaye Lucy Lameck Isambwa Mbibo
Lady Jay Dee Ameshare Taarifa Hizo za msiba wa dada yake kupitia mitandao yake ya kijamii

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

SERIKALI YATANGAZA TAREHE YA USAILI KWA WAOMBAJI WA NAFASI ZA KAZI ZA KILIMO NA MIFUGO

Serikali inapenda kuwaarifu waombaji wa nafasi za kazi kwa tangazo la tarehe 27 Novemba, 2013 wa kada za Kilimo, Mifugo, Uvuvi na Udereva kuwa usaili utaanza tarehe 4 Machi, 2014 takriban katika mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar.

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Xavier Daudi amesema hayo leo ofisini kwake wakati akiongea na baadhi ya wadau waliomtembelea kwa lengo la kufahamu masuala mbalimbali ya uendeshaji wa mchakato wa ajira serikalini.
Amesema usaili huo unaoanza tarehe 4 Machi katika mikoa takribani yote nchini utahusisha jumla ya wasailiwa 6,087 wa fani za Kilimo, Mifugo, Uvuvi na udereva kwa kada ambazo sio za Maofisa. Amefafanua kuwa vigezo vya kupanga mikoa ya usaili vimetokana na anwani ambazo waombaji waliwasilisha katika barua zao za maombi husika ya kazi.
Daudi alibainisha kuwa kila mwombaji aliyekidhi vigezo na kuchaguliwa kwa ajili ya usaili anapaswa kwenda kufanyia usaili katika mkoa aliopangiwa kama anwani yake inavyoonyesha katika tangazo kwenye tovuti ya Sekretarieti ya Ajira, isipokuwa kwa waombaji wa mkoa wa Katavi wao wataenda kufanyia usaili mkoa wa Rukwa na waombaji waliotumia anwani za mkoa wa Singida wao watafanyia usaili mkoa wa Manyara kutokana na sababu zisizozuilika.
Aliongeza kuwa kwa mwombaji ambae hatazingatia anwani, siku na muda aliopangiwa na kuamua kwenda mkoa mwingine tofauti na utaratibu uliopangwa ajue wazi hatasailiwa kwa kuwa ratiba na idadi ya majopo ilishapangwa kwa kila mkoa na haitabadilishwa ili kuweza kurahisisha kazi hiyo kukamilika  kwa ufanisi.

ANGAALIA PICHA ZA MECHI YA JANA KATI YA OLYMPIACOS NA MAN UTD WALIOCHAPWA 2 BILA MAJIBU

Celebration: Alejandro Dominguez (centre) wheels away after scoring the opener in Greece
Celebration: Alejandro Dominguez (centre) wheels away after scoring the opener in Greece
Arrival: Joel Campbell slides on his knees in celebration of his goal just after half-time
Arrival: Joel Campbell slides on his knees in celebration of his goal just after half-time
Outstretched: David De Gea is well beaten by Campbell's shot in the 55th minute to deflate United
Outstretched: David De Gea is well beaten by Campbell's shot in the 55th minute to deflate United
Flat out: Robin van Persie lies on the floor after missing United's best chance of the game late on
Flat out: Robin van Persie lies on the floor after missing United's best chance of the game late on. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO FEBRUARI 26, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

PBF_8384-w480-h580
PBF_8385-w480-h580 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

DAKTARI FEKI AKAMATWA MUHIMBILI...!!!

daktari_553f2.jpg
Askari akimwongoza mtuhumiwa Mustafa Kitano, anayedaiwa kutoa huduma za utabibu Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kinyume na utaratibu,Picha na Michael Jamson
Dar es Salaam. Maofisa Usalama wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), wamemkamata mtu anayedaiwa kutoa huduma kwa wagonjwa kinyume cha utaratiba na kwamba, amekuwa akiwatapeli wagonjwa wanaokwenda kupata matibabu.
Akizungumza ofisini kwake jana, Ofisa Uhusiano wa MNH, Aminieli Eligaesha alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Mustafa Kitano na kwamba, amekuwa akitumia majina ya Dk Nyirabu na Koba, alikamatwa wakati akimsaidia mgonjwa mmoja.
Eligeisha alisema Februari 22 mwaka huu walipata taarifa kutoka kwa Hussein Haji kuwa, kuna daktari anaitwa Koba alitaka kumtapeli Sh200,000 ili amtafutie kazi ya udereva kwenye tawi la MNH lililopo Kahama Shinyanga. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

OPERESHENI DHIDI YA WAASI WA UGANDA ADF

UGANDA_98bb6.jpg
Waasi wa Uganda ADF.
Operesheni zinaendelea katika wilaya ya Beni, jeshi la serikali limetangaza kuwa, operesheni hizo, zimelipelekea jeshi hilo kuyakomboa maeneo kadhaa, toka mikononi mwa waasi.
Operesheni dhidi ya waasi wa Uganda ADF wanaojihifadhi katika misitu
ya wilaya ya Beni mashariki mwa jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zikiwa zinaendelea,huku wanajeshi wakiwa wamepelekwa katika eneo hilo, raia wa mji na wilaya za Beni wameanza kulalamikia usalama wao,kutokana na jinsi wanavyo nyanyaswa na wanajeshi wa serikali. Ili kukomesha vitendo vya unyanyasi wa raia, jeshi la Congo limelivalia njuga suala hilo.
Mwandishi wetu John Kanyunyu na ripoti kamili kutoka Beni. Kusikiliza ripoti hiyo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz
Chanzo, dw.de.com/swahili.

Tuesday, February 25, 2014

'ANAYEONA POSHO HAITOSHI AFUNGASHE VIRAGO'

bunge_4f64b.jpg
Wizara ya Fedha imepigilia msumari maombi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba ya kutaka waongezewe posho na kusema anayeona ameacha kazi inayomlipa zaidi kwenda bungeni afungashe virago na kuondoka.
Msimamo huo umekuja siku moja tu baada ya gazeti hili kudokeza kuwa madai ya wajumbe wa bunge hilo kutaka waongezewe posho kutoka Sh300,000 za sasa kwa siku, yamegonga mwamba baada ya kamati iliyoteuliwa kuchunguza uhalali wake kusema kiwango hicho kinatosha.
Mwenyekiti wa muda wa bunge hilo, Pandu Kificho alisema jana bila kutaja viwango, kuwa ripoti ya kamati hiyo imewasilishwa kwa Rais Jakaya Kikwete kwa uamuzi.
Madai ya wajumbe kutaka waongezewe posho, yamechafua hali ya hewa ndani na nje ya Bunge, huku baadhi ya wananchi wakipaza sauti zao na kumsihi Rais Kikwete alivunje bunge hilo iwapo wajumbe watashikilia msimamo wa kutaka nyongeza ya posho.
Jana, Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba alisema wanaoshiriki kutunga Katiba ni Watanzania na siyo wataalamu washauri waliokodiwa kutoka nje.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

NYALANDU APANGUA WAKURUGENZI MALIASILI


nyalandupx_745e8.jpg
Dar es Salaam. Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, amewaondoa katika nyadhifa zao, Wakurugenzi mbalimbali kwa sababu zilizoelezwa kushindwa kutekeleza majukumu yao.
Hatua ya Nyalandu imekuja ikiwa ni utekelezaji wa azimio la Bunge la Desemba 22, 2013 lililotaka Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori kuwajibishwa kutokana na tuhuma za uzembe na ukiukwaji wa haki za binadamu katika Operesheni Tokomeza.
Nyalandu alisema: "Namwondoa Prof Alexander Songorwa (Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori) na kumteua Paul Sarakikya kukaimu nafasi hiyo."


Alisema pia kuwa amemwondoa Mkurugenzi Msaidizi wa Matumizi Endelevu ya Wanyamapori, Profesa Jafari Kidegesho kwenye nafasi hiyo na Dk Charles Mulokozi ameteuliwa kushika wadhifa huo.
Mwingine aliyeteuliwa ni Julius Kibebe kuwa Mkurugenzi Msaidizi Uzuiaji-Ujangili, nafasi iliyoachwa wazi na Sarakikya wakati Mkurugenzi Msaidizi wa Mafunzo, Utafiti na Takwimu, Nebbo Mwina anabaki kwenye nafasi yake. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE FEBRUARI 25, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

. 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

KUANGALIA MECHI YA TWIGA STARS, ZAMBIA BURE

twiga star by mafoto1 97507
Washabiki wa mpira wa miguu nchini watashuhudia bure mechi ya timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya wanawake (Twiga Stars) dhidi ya Zambia (Shepolopolo).
Mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya kwanza ya michuano ya Afrika kwa Wanawake (AWC) itachezwa Ijumaa (Februari 28 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili alasiri.
Twiga Stars ambayo ilipoteza mechi ya kwanza iliyochezwa Lusaka, Februari 14 mwaka huu kwa mabao 2-1 iko kambini chini ya Kocha Rogasian Kaijage na msaidizi wake Nasra Juma ikijiwinda kuwakabili Wazambia wanaotarajiwa kutua nchini Alhamisi (Februari 26 mwaka huu).
Waamuzi wa mechi hiyo Ines Niyonsaba, Jacqueline Ndimurukundo, Axelle Shikana na Suavis Iratunga kutoka Burundi kutoka Burundi wanatarajiwa kuwasili nchini keshokutwa (Februari 26 mwaka huu). Kamishna Fran Hilton Smith kutoka Afrika Kusini yeye atatua nchini Februari 27 mwaka huu kwa ndege ya South Africa Airways. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 
 Chanzo: TFF

MILIPUKO YA MABOMU YARINDIMA Z'BAR

bomu_b1855.png
Na Mwinyi Sadallah, Mwananchi
Zanzibar. Watu wanne wamejeruhiwa baada ya milipuko minne inayoaminika kuwa ni mabomu kutokea katika maeneo matatu tofauti Zanzibar.
Katika moja ya matukio hayo, watu wanne walijeruhiwa, mmoja akikatika mguu, katika eneo la Unguja Ukuu, Mkoa wa Kaskazini Unguja. Majeruhi wawili wamelazwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja, Unguja.
Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Mkoa wa Kusini Unguja, Hamad Said Masoud alisema mlipuko wa kwanza ulitokea juzi katika eneo la Fuaoni Maili Nne wakati watu wasiojulikana waliporusha kitu kinachoaminika kuwa ni bomu wakati waumini wa Kanisa la Evangelist wakiendelea na ibada ya Jumapili.
Kamishna wa Polisi Zanzibar, Hamdan Omar Makame alisema tukio la juzi, kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu kilirushwa wakati waumini wa kanisa hilo wakiendelea na ibada na kutoa mlipuko na kishindo kikubwa. Alisema wakati wakiendelea na uchunguzi wa tukio hilo, milipuko mingine mitatu ilitokea jana.
Katika mlipuko wa kwanza kwa jana uliotokea saa 6.30 mchana katika kituo kimoja cha fundi vyuma aliyetambulika kwa jina la Juma Abdallah huko Unguja Ukuu ndiko kulikokuwa na watu waliojeruhiwa.
Waliojeruhiwa katika tukio hilo ni Pandu Haji Pandu aliyekatika mguu na Shaaban Khamis Ibrahim ambaye aliumia sehemu za kiuno.
Hamad alisema mtu mmoja aliokota chuma kizito na kukipeleka kwa fundi akitaka atengenezewe nanga kwa ajili ya uvuvi.
Alisema mhunzi huyo alipokea kazi hiyo na alipokuwa akijiandaa kwa matengenezo ndipo mlipuko huo ulipotokea. Mlipuko huo ulitokea sambamba na mwingine katika Mgahawa wa Mercury's uliopo Malindi, Mkoa wa Mjini Magharibi na kusababisha huduma za chakula kusitishwa kwa muda.
Tukio la mwisho lilikuwa saa 7:15 mchana katika Kanisa la Anglikana, Mkunazini. Katibu wa Kanisa hilo Dayosisi ya Zanzibar, Nuhu Saranya alisema: "Nilisikia kishindo cha mlipuko, wakati nikitafakari ni kitu gani hicho, nikasikia mlipuko wa pili nje ya kanisa letu," alisema.
Mmoja wa majeruhi, Mohamed Ibrahim alisema hakujua kilichotokea huku akilalamika kuwa masikio yake hayasikii vizuri kutokana na kishindo hicho.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Monday, February 24, 2014

FANYA HAYA KUZUIA WATU WASIINGILIE MAPENZI YENU...!!!

http://jambotz8.blogspot.com/
Sio mbaya kwa marafiki wa karibu au ndugu na jamaa kufahamu kushirikiana nanyi katika mapenzi yenu kama vile wakati wa sherehe au msiba. Pia sio mbaya kujuliana hali na kutambulisha mambo ya msingi yanayoendelea katika mahusiano yako wewe na mpenzi wako. Hata hivyo kuna wakati watu wengine wa pembeni, wawe majirani, ndugu, wazazi au marafiki wanaweza kuwa ‘sumu’ ya mahusiano yako, hasa pale unapowategemea sana kutoa msaada, maoni au maelekezo katika maisha yako ya mapenzi.  Makala hii inaeleza mambo ya msingi unayoweza kufanya ili kupunguza uwezekano wa rafiki, ndugu, jamaa, au wazazi kuwa ‘sumu’ ya mapenzi yako.

1. Udhibiti wa taarifa kwa wengine:  Kadri unavyoelezea mahusiano yako kwa watu wengine ndivyo unavyowapa nafasi watu kutoa maoni, na hata kudhani kuwa wana dhamana ya kukuelekeza unavyotakiwa kuishi na mwenza wako. Hivyo basi, chukua muda wa kutosha kutafakari na kufanya uchunguzi kuhusu maswala yako ya mahusiano kabla haujaanza kutafuta maoni, ushauri kwa watu wengine. Ni bora ukasoma vitabu, na makala mbalimbali, hususani zihusuzo tabia na maisha ya mahusiano, zitafakari vema ili kuona zinahusiana vipi na unayokumbana nayo katika mahusianao yako.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Wednesday, February 19, 2014

UGANDA WATUNGA SHERIA KALI KWA WANAOVAA 'MINI SKIRT'


Maandamano ya kupinga agizo la wanawake kutovalia sketi fupi

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, ametia saini sheria mpya inayotoa adhabu kali kwa wanaopatikana na hatia ya kutembea nusu uchi au kuhusika na vitendo vinavyohusisha picha zenye watu uchi.
Wanawake pia wamezuiwa kabisa kuvalia sketi fupi sana au 'Mini Skirt' kama zinavyojulikana au blausi ambazo zinaonyesha kifua chao hadharani na kusababisha hisia za kingono .
Sheria hiyo inasema kuwa nguo kama hizo zitakubalika tu ikiwa zinatumika kwa ajili ya mafunzo au wakati wa michezo na hafla za kitamaduni.
Akihutubia waandishi wa habari, mjini Kampala, waziri wa maadili na utawala bora, Reverend Simon Lokodo alisema kuwa Rais Museveni alipitisha sheria hiyo tarehe 6 mwezi huu, miezi mwili bada ya bunge kuipitisha. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

BOKO HARAM BADO NI HATARI NIGERIA

Wapiganaji wa Boko Haram
Taarifa kutoka nchini Nigeria, zinasema kuwa kumekuwa na mashambulizi mabaya sana dhidi ya wakazi wa mji wa mpakani wa Bama, siku moja baada ya msemaji wa Rais kusema kuwa jeshi linashinda vita dhidi ya wapiganaji wa Boko Haram.
Seneta wa jimbo la Borno, Ahmed Zanna ameambia BBC kuwa mashambulizi hayo yaliyotokea Jumatano asubuhi yalidumu kwa masaa 5
Siku ya Jumanne, msemaji wa jeshi Doyin Okupe, alisema kuwa jeshi limeweza kudhibiti hali.
Zaidi ya watu 254 wameuawa mwaka huu pekee na watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa kundi la Boko Haram.
Maelfu wameuawa tangu Boko Haram kuanza vita dhidi ya serikali mwaka 2009.
Taarifa ya bwana Okupe, ilitofautiana na matamshi ya gavana wa jimbo la Borno ambalo ni kitovu cha Boko Haram.
Gavana Kashim Shettima, ametoa wito wa kutaka wanajeshi zaidi na ambao wamejihami vilivyo kupelekwa katika jimbo hilo, kuliko vikosi vya usalama vilivyoko katika jimbo hilo.
Taarifa kuhusu mashambulizi ya leo bado hazitajitokeza lakini wakazi wa eneo hilo wamewasiliana na idhaa ya BBC Hausa kuhusu mashambulizi ya leo. Mji huo hata hivyo umewahi kushambuliwa katika siku za nyuma. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz
Chanzo BBC

TAHADHARI YA MVUA KUBWA FEB 19-21/2014

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
Simu: 255 22 2460735/2460706

FAKSI: 255 22 2460735/2460700 S.L.P. 3056
Barua pepe: met@meteo.go.tz DAR ES SALAAM
Tovuti:  www.meteo.go.tz
Unapojibu tafadhali nakili:
Kumb. Na.: TMA/1622 18 Februari, 2014

TAARIFA KWA UMMA: VIPINDI VYA MVUA KUBWA VINATARAJIWA.
Taarifa Na. 201402-03
Muda wa Kutolewa
Saa za Afrika Mashariki
Saa 8:30 Mchana

Daraja la Taarifa:- Tahadhari
Kuanzia: Tarehe 19  Februari, 2014 

Mpaka: Tarehe 21 Februari, 2014
Aina ya Tukio Linalotarajiwa ni vipindi vya mvua kubwa (zaidi ya mm 50 ndani ya saa 24) kwa siku.

Kiwango cha uhakika:- Wastani (60%)
Maeneo yanayotarajiwa kuathirika ni Kanda ya kati (mikoa ya Singida na Dodoma), nyanda za juu kusini magharibi (mikoa ya Iringa, Mbeya na Njombe) na maeneo ya kusini  (Mikoa ya Ruvuma na Morogoro).

Maelezo:-
Hali hii inatokana na kuimarika kwa mfumo wa mgandamizo mdogo 
wa hewa katika rasi ya Msumbiji. Mfumo huu unatarajiwa kuvuta 
upepo kutoka misitu ya Congo kupitia maeneo tajwa hapo juu.

Angalizo:-
Idara zinazohusika na hali ya tahadhari pamoja na wakazi wa maeneo 
hatarishi wanashauriwa kuchukua tahadhari.

Maelezo ya Ziada:-
Mamlaka ya Hali ya Hewa inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa 
mrejeo kila itakapobidi.

Imetolewa na 
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.

Monica Mutoni
Public Relation Office
Tanzania Meteorological Agency

VITA VYAZUKA TENA MALAKAL, SUDAN KUSINI

Haya ni mapigano ya kwanza tangu kutia saini mkataba wa kusitisha vita
Mapigano yanaripotiwa kuzuka Sudan Kusini kwa mara ya kwanza tangu serikali na waasi kutia saini makubaliano ya kusitisha vita mwezi Januari.
Waasi wanaomtii makamu wa Rais wa zamani Riek Machar, wameshambulia mji wa Malakal, ambao ni mji mkuu wa jimbo la Upper Nile linalozalisha mafuta kwa wingi.
Majeshi ya serikali, yamepambana vikali na waasi hao katika maeneo tofauti ya mji huo.
Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa mjini Juba, (Toby Lanzer), amezitaka pande zote kwenye mzozo huo, kulinda raia.
Makabiliano hayo bila shaka yanazua wasiwasi kuhusu hali ya usalama katika visima vya mafuta Kaskazini mwa nchi. Mafuta ya Sudan Kusini ndio uti wa mgongo wa uchumi wa nchi hiyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz
Chanzo BBC Swahili

CHADEMA WATOA SIKU TATU KWA RAIS KIKWETE...!!!

Rais Jakaya Kikwete ametakiwa kufuta kauli yake ya kuwataka wana CCM kuacha unyonge na kujibu mapigo dhidi ya upinzani na ametakiwa kuomba radhi ndani ya siku tatu, vinginevyo suala hilo litafikishwa jumuiya za kimataifa.
Rais Kikwete alitoa kauli hiyo wakati wa kufunga Mkutano wa Halmashauri Kuu ya chama hicho Mjini Dodoma mwishoni mwa wiki iliyopita, ambapo Chadema wanaitafsiri kama kielelezo cha kuvuruga amani ndani ya nchi.
Kwa majibu CCM kupitia Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema kamwe hawatafanya hivyo.
"Kauli aliyoitoa Rais Kikwete ni ndogo na kutokana na vitendo vinavyofanywa na viongozi na wanachama wa Chadema kuvuruga amani nchini," alisema na kuongeza kuwa dawa ya moto ni moto.
Mkurugenzi wa Mafunzo na Operesheni wa Chadema, Benson Kigaila alisema kuwa Rais Kikwete anatakiwa kufuta alichokizungumza ndani ya siku tatu kuanzia jana, vinginevyo watalifikisha suala hilo mbele ya jumuiya ya kimataifa kama sehemu ya malalamiko yao.
Alisema kuwa Rais Kikwete ni Amiri Jeshi Mkuu, na alihoji kwanini awatake WanaCCM kujibu mapigo dhidi ya wapinzani badala ya kuacha hatua za kisheria zikafuatwa kwa kutumia vyombo husika ambavyo ni polisi na majeshi na mahakama. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz
Chanzo:Mwananchi

MAGAZETI YA LEO FEBRUARI 19, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MATOKEO YA MANCHESTER CITY vs BARELONA

Screen Shot 2014-02-19 at 7.09.55 AM 
Kwenye zile game za UEFA ambazo zitaingia kwenye rekodi ya kutazamwa na mamilioni mwaka 2014 na hii imo ambapo Manchester City wamefungwa goli mbili zote kwenye kipindi cha pili.
Screen Shot 2014-02-19 at 7.11.49 AM 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

WACHEZAJI WATATU KUFUATA NYAYO ZA AKINA MBWANA SAMATTA

Wadau wengi wa michezo wanakua wakiwaangalia sana wachezaji waliotoka Bongo kwenda nje ya nchi kucheza soka la kulipwa na miongoni mwao ni Mbwana Samatta ambaye kwa mshahara wake peke yake umezua gumzo mtaani,
Sasa taarifa kutoka TFF ambayo ame-amplify Ofisa habari wa TFF Boniface Wambura unaambiwa Wachezaji watatu kutoka Tanzania ambao ni wachezaji wa mpira wa miguu tayari wameombewa hati ya uhamisho wa Kimataifa[ITC] ili wakacheze katika nchi za Thailand na Ujerumani.
Miongoni mwao ni mchezaji Khamis Mroki Jamal ambaye timu yake ilikua Daraja la Kwanza ya Polisi Dar es Salaam yeye ameombewa ITC na Chama cha Mpira wa Miguu Thailand (FAT) ili akajiunge na Kabinburi ya nchini humo.
Wengine ni Said Ali Nassor aliyekuwa akichezea FC Turkey ya Zanzibar na Samuel Chuonyo hao wote wameombewa na ITC na Chama cha Mpira wa Miguu Ujerumani (DFB) kwa ajili ya kujiunga na klabu ya VfB Eichstatt.
Kwa sasa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linafanyia kazi maombi hayo na mara taratibu zote zitakapokamilika ikiwemo ridhaa ya klabu zao za hapa Tanzania TFF itatoa ITC hizo na jamaa kwenda kujiunga na timu hizo.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

TCIB: WAGOMBEA UCHAGUZI WAPIMWE AFYA


kibamba_9c593.jpg
Mkurugenzi Mtendaji wa TCIB, Deus Kibamba.PICHA|MAKTABA
Dar es Salaam. Kituo cha Taarifa kwa Wananchi (TCIB), kimeitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kubadilisha mfumo wa uendeshaji Uchaguzi Mkuu ikiwamo kuweka kipengele kitakachowalazimisha wagombea wa nafasi za uongozi kupima afya zao ili kuepuka kuchaguliwa viongozi wenye maradhi yatakayowafanya washindwe kumudu majukumu yao ya kazi.
Pia kimeitaka NEC kuweka zuio la kufanyika kwa uchaguzi na kutoza faini kali kwa mgombea anapotangaza kujitoa katika hatua za mwisho kabla ya kufanyika uchaguzi wenyewe.
Hayo yalisemwa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa TCIB, Deus Kibamba wakati akitoa tathimini ya uchaguzi mdogo wa udiwani uliofanyika katika Kata 27 na funzo kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa na ule wa Ubunge katika Jimbo la Kalenga mwezi ujao.
Alisema, Novemba 2012 kulifanyika uchaguzi kujaza nafasi 29 za udiwani wakati Juni 2013 kulifanyika tena uchaguzi katika kata 22 na mwezi huu umefanyika uchaguzi katika kata 27, huku baadhi ya kata zikiwa tayari zimekwisharudia chaguzi zaidi ya mara moja ndani ya kipindi cha miaka mitatu.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...