Wednesday, February 19, 2014

TCIB: WAGOMBEA UCHAGUZI WAPIMWE AFYA


kibamba_9c593.jpg
Mkurugenzi Mtendaji wa TCIB, Deus Kibamba.PICHA|MAKTABA
Dar es Salaam. Kituo cha Taarifa kwa Wananchi (TCIB), kimeitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kubadilisha mfumo wa uendeshaji Uchaguzi Mkuu ikiwamo kuweka kipengele kitakachowalazimisha wagombea wa nafasi za uongozi kupima afya zao ili kuepuka kuchaguliwa viongozi wenye maradhi yatakayowafanya washindwe kumudu majukumu yao ya kazi.
Pia kimeitaka NEC kuweka zuio la kufanyika kwa uchaguzi na kutoza faini kali kwa mgombea anapotangaza kujitoa katika hatua za mwisho kabla ya kufanyika uchaguzi wenyewe.
Hayo yalisemwa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa TCIB, Deus Kibamba wakati akitoa tathimini ya uchaguzi mdogo wa udiwani uliofanyika katika Kata 27 na funzo kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa na ule wa Ubunge katika Jimbo la Kalenga mwezi ujao.
Alisema, Novemba 2012 kulifanyika uchaguzi kujaza nafasi 29 za udiwani wakati Juni 2013 kulifanyika tena uchaguzi katika kata 22 na mwezi huu umefanyika uchaguzi katika kata 27, huku baadhi ya kata zikiwa tayari zimekwisharudia chaguzi zaidi ya mara moja ndani ya kipindi cha miaka mitatu.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 
"Tangu mwaka 2010 ulipofanyika uchaguzi mkuu, kumefanyika chaguzi tatu za madiwani nafasi hizo kuwa wazi zilitokana na vifo hivyo kuna haja ya viongozi wetu kuwapima afya zao hata magonjwa ya kisasa ili kuepusha kufanya chaguzi za mara kwa mara zenye gharama kubwa fedha zinazoweza kusaidia katika miradi mingine ya maendeleo," alisema Kibamba.
Aliongeza: "Unakuta mtu anachaguliwa na anapewa nafasi nyeti serikalini lakini afya yake hairidhishi na mwisho wa siku anafariki yote haya ni kutokuwapima afya zao."
Kibamba akizungumzia hatua ya kuchukua na kurejesha fomu alisema kulitokea dosari kadhaa, ambazo zimekuwa zikijirudia mara kwa mara mfano, mgombea kushindwa kurejesha fomu kwa wakati katika Kata ya Nduli mkaoni Iringa na kutekwa kwa mgombea katika kata ya Mtae mkoani Tanga wakati akirejesha fomu.
Alisema matukio kama hayo yanatakiwa kuangaliwa kwa jicho la tatu na NEC kuzuia kufanyika kwa uchaguzi ili kutoa nafasi kwa walioshindwa kuwasilisha fomu kutafutiwa ufumbuzi.
"Hapa kuna dalili za rushwa, mtu huwezi kuomba kugombea harafu ukajitoa hatua za mwisho, hivyo NEC iweke adhabu kali kwa watakaokuwa wakijitoa na wanaovamiwa," alisema Kibamba
Akizungumzia kauli tata ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa katika Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Mjini Dodoma mwishoni mwa wiki kuwa unyonge kwa wanachama wake sasa basi na ile ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliyoitoa Bungeni mwaka jana ya kuwapiga wanaokaidi amari ya vyombo vya dola alisema ni kauli za kichochezi zinazotakiwa kutafutiwa ufumbuzi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 
chanzo MWANANCHI

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...