Sunday, April 21, 2013

WASOMI:::SPIKA ANAVURUGA BUNGE

Baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda kutoa mwongozo na kuunga mkono uamuzi wa Naibu wake, Job Ndugai kuwasimamisha wabunge sita wa Chadema, wasomi, wanasiasa na wanaharakati wamesema Kiti cha Spika ndiyo chanzo cha mvutano bungeni kwa kuwa kinapendelea wabunge wa chama tawala (CCM).
Wamesema licha ya Bunge kuongozwa na kanuni, wakati mwingine viongozi hao wa Bunge wanatumia kanuni hizo kuwapendelea wabunge wa CCM, huku wakieleza kuwa licha ya wabunge wa chama hicho kutukana, hawakupewa adhabu yoyote.
Jumatano ya wiki hii, Ndugai aliwasimamisha Tundu Lissu (Singida Mashariki), Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini), Mchungaji Peter Msigwa (Iringa Mjini), Highness Kiwia (Ilemela), Ezekiah Wenje (Nyamagana) na Godbless Lema wa Arusha Mjini kutohudhuria Bunge kwa siku tano kutokana na alichokiita kufanya vurugu ndani ya Bunge.
Uamuzi huo wa Spika Makinda ulikuja baada ya Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kumtaka Ndugai aeleze alitumia kanuni gani kuwasimamisha wabunge hao.

DAWA ZA KUONGEZA AKILI ZATUA NCHINI

Mtindo wa maisha, ulaji na msongo wa mawazo, vimewasababishia Watanzani wengi maradhi lukuki hata vifo.Hata hivyo, wataalamu wa afya kutoka Afrika Kusini wamekuja na dawa maalumu, zilizo na uwezo wa kurudisha kumbukumbu, kuongeza upeo darasani, kuondoa sumu mwilini na kumfanya mzee kuonekana kijana.

 Dawa hizo zinazotumia vitamini zilizomo kwenye vyakula vya kila siku, zina uwezo wa kuongeza kiwango cha uelewa kwa mwanafunzi au mfanyakazi.
Kiwango hicho cha uelewa kitaalamu unatambulika kama ‘IQ’.
Mratibu wa dawa hizo hapa nchini, John Haule anasema kuwa dawa hizo zina uwezo wa kufanya kazi kwa haraka.
“Virutubisho hivi ni vizuri kwa wale wanaokwenda katika
mitihani au wanataka kufanya kazi inayohitaji umakini wa hali ya juu,” anasema Haule na kuongeza: “Zimetengenezwa kwa vyakula tunavyotumia na siyo kemikali.”
Haule ambaye ni mtaalamu wa tiba asili na mimea anasema kwamba mtindo wa maisha na vyakula vinavyoliwa na watu mara kwa mara kwa sasa huufanya mwili kuhifadhi sumu nyingi mwilini.

MUME WA MTU ATIWA MBARONI KWA KOSA LA KUFANYA MAPENZI NA MBUZI MWENYE MIMBA NA KUHARIBU MIMBA YA MBUZI HUYO

Marcel ambaye ni mume wa mtu, alifunguliwa kesi namba 29/2013 katika Mahakama ya Mwanzo ya Bashneti mkoani Babati kwa kosa la kuiingilia kimwili mifugo, kinyume na kifungu cha 325 kanuni ya adhabu, sura ya 16 na kesi hiyo ilisomwa hivi karibuni.
Mshitakiwa aliwekewa dhamana lakini siku chache baadaye kesi ilipotakiwa kuendelea, hakuonekana na imebainika mahakamani hapo kuwa ametoroka.

Kesi hiyo ipo mbele ya Hakimu Julius Dagharo wa mahakama hiyo na aliyethibitisha mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa ametoroka ni Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Bashneti, Omari Mwanditi.
Akizungumza mwishoni mwa wiki iliyopita, mmiliki wa mbuzi anayedaiwa kuingiliwa,  Clementina Masay alidai kuwa mtuhumiwa huyo amemsababishia hasara kwani mbuzi wake alikuwa na mimba lakini baada ya kitendo hicho, imeharibika.
Jamii ya wafugaji wa Kiiraq wa eneo hilo wamesikitishwa na kitendo cha mtuhumiwa kudaiwa kuiingilia mifugo yao kimwili mara kwa mara na wameahidi kumsaka hadi wamkamate.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Babati, ACP Akili Mpwapwa amekiri kutokea kwa tukio hilo na ametoa wito kwa wananchi kutoa taarifa wakimuona mtuhumiwa huyo ili afikishwe mahakamani.

AMA kweli dunia imekwisha kwani mtu mmoja, Daniel Marcel (27), mkazi wa Kijiji cha Madunga, wilayani Babati, Manyara, amekamatwa na kufikishwa mahakamani kwa madai ya kufanya mapenzi.

WAREMBO WA XTRA BONGO WAZITWANGA NGUMI, KISA BUZI LA KIZUNGU.


Otilia Boniface kulia na Janeth Tingisha

Wanenguaji wa Bendi ya Extra Bongo, Otilia Boniface na Janeth Tingisha mwishoni mwa wiki iliyopita walitoa kali ya mwaka baada ya kutaka kutwangana makonde wakigombea kutoa namba zao za simu kwa buzi la Kizungu.

Tukio hilo lilitokea ndani ya Ukumbi wa Meeda uliopo Sinza jijini Dar ambapo awali Mzungu huyo alivutiwa na wadada hao hivyo kuwafuata na kuomba namba ya simu ya mmoja wao.

Kufuatia ombi la Mtasha huyo, kila mmoja alitaka apate nafasi hiyo ndipo wanenguaji hao waliposukumana na kufikia hatua ya Janeth kuchukua simu ya Otilia na kuipiga chini ila kwa busara za Mzungu huyo alichukua namba za wote.

JUMA NATURE ATIMULIWA EATV BAADA YA KUINGIA AKIWA AMEVAA KANDAMBILI.....

Msanii mkongwe na maarufu nchini, Juma Kassin Kiroboto, aka Nature, ameonyesha kukerwa na kitendo  cha  kutimuliwa  jana usiku katika kipindi cha burudani cha televishen inayotizamwa africa ya mashariki alipokuwa akifanya nao interview. 
Nature alionekana akiwa amevaa kawosh na ndala na mara baada ya mahojiano mafupi ya mwanzo  mtangazaji alisema watarejea baada ya mapumziko mafupi  na ndipo Nature hakuonekana tena.
  Kilichotokea kwa mujibu wa Nature mwenyewe, ni wakati wa mapumziko hayo, mtangazaji wa kipindi hicho alimfuata na kumuambia kuwa hataendelea na interview tena kwasababu ya mavazi aliyokuwa kavaa ambayo ni ndala na kawosh. kuonyesha kukerwa kwake na ishu hiyo Nature aliamua kuandika yafuatayo  kupitia ukurasa wake wa facebook....

"hivi kwa mfano angekuwepo mzungu pale na kavaa ndala wangesitisha mahojiano na kuvaa kaoshi ni tatizo....

kunywa nimekunywa bt kuna baya nimeliongea na hivi kama kweri we nimuandishi wa habari unaruhusiwa kuvaa vile kisheria kama yule mtangazaji nimeboreka kinoma na ikiwezekana nasitisha kuanzia ssa kupeleka ngoma zangu pale siitaji interview"

WABUNGE WATAKA JUMBA LA MCHUNGAJI LWAKATARE LIVUNJWE.........!!!

'Hekalu' linalomilikiwa na Mchungaji Getrude Lwakatare.
Wabunge wamemtaka Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira Terezya Huvisa kuzivunja nyumba mbili zilizopo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam zilizojengwa katika fukwe ya bahari ya Hindi ikiwemo ya mbunge licha ya kwamba kuna zuio la mahakama.

Bila kutaja majina ya wamiliki hao, wabunge hao walitaka hatua hizo zichukuliwe kwa haraka kwa nyumba hizo zilizojengwa kwenye fukwe kinyume cha sheria zivunjwe kwa maelezo kuwa hazina ofa wala hati.
 
Sambamba na hilo wametaka watendaji wa serikali waliohusika kutoa vibali kuruhusu ujenzi huo kwa maelezo kuwa walichukua rushwa wachukuliwe hatua.

SHY- ROSE BHANJI APATA AIBU YA KARNE TOKA KWA ANNA KIBIRA

Aliyekuwa mjumbe baadae katibu mkuu wa CHANETA Anna Kibira amechaguliwa tena kuwa mwenyekiti wa chama cha mpira wa pete chaneta Katika uchaguzi uliofanyika jioni ya leo hii Mkoani Dodoma , huku msimazi wa uchaguzi huo akiwa mkuu wa wilaya ya bahi na aliyekuwa Mtangazaji wa zamani wa itv Betty Mkwasa .
Anna Kibira amemshinda mpinzani wake Shy-Rose Bhanji kwa tofauti ya la kura arobaini katika nafasi ya uenyekiti Anna Kibira amepata kura 61 dhidi ya mpinzani wake Shy-Rose Bhanji ambaye amepata kura arobaini na moja .
Aidha kulikuwa na nafasi mbalimbali ambazo zilikuwa zikigombewa katika chama hicho cha mpira wa pete ambapo kulikuwa na wajumbe wa kamati ya utendaji ambao walikuwa wagombea tisa lakini wamepataikana wagombea sita tu.

Grace Khatib ambaye alikuwa hana mpinzani katika nafasi ya mweka hazina alipata kura za ndio 66 na kura za hapana 16 kati ya kura 82 zilizopigwa.
Katika nafasi ya makamu mwenyekiti kulikuwa na wagombea wawili Zainab Mbiro na Agnes Madasila katika nafasi hiyo Zainabu Mbiro alipata kura hamsini saba wakati mpinzani wake amepata kura 27
Kwa maana hii CHANETA imepata safu mpya kabisa ya uongozi baada ya ile ya mwanzo ile kuamua kuachia ngazi na wagombea wengine kuamua kutokugombea kabisa uongozi katika chama hicho cha mchezo wa pete kwani safu mpya inatakiwa kufanya kazi ya ziada kufikia malengo ya kuinua mchezo wa mpira wa pete kwani uongozi uliopita uliiwezesha CHANETA kuifikisha timu ya taifa ya mchezo huo katika mashindano ya dunia.
Chama kiliweza kuaandaa michuano ya mataifa ya afrika ni wazi kabisa wanachangamoto kubwa ya kufanya japokuwa mara baada ya ushindi kibira amesema kuwa anataka kuupeleka mchezo huo mikoani na kwenda kuuimarisha zaidi vijijini .

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRIL 21 2013

.

.
.
.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...