Friday, February 22, 2013

BREAKING NEWSZZZZZZZZ .... BABA MZAZI WA RAIS MSEVEN AFARIKI DUNIA

Baba wa Rais Museveni afariki dunia.

Mzee Amos Kaguta baba mzazi wa Rais Yoweri Museveni wa Uganda amefariki dunia leo asubuhi huko jijini Kampala Uganda.

Mzee Amos Kaguta amefariki akiwa na umri wa miaka 96 na inasemekena alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya tumbo pia kichwa.East Africa Radio kwa habari zaidi.

LOWASSA ATOA OMBI KWA RAIS KIKWETE



Waziri mkuu aliejiuzulu Mh. Edward Lowassa, amemtaka rais Kikwete aunde tume kuchunguza kilichopelekea matokeo mabaya ya form IV mwaka huu. Amesema tume itasaidia kubaini ni nini chanzo cha tatizo.

Wakati huo huo Mh. Lowassa amemsifu kijana aliyemchora Messi na kusema kijana huyo ni intelligent. Amesifu uwezo wa kijana huyo kufanya hivyo!


Vilevile Mh. Lowassa, ameitaka serikali kuongeza uwekezaji katika elimu kwani amesema tofauti na nchi nyingine za Afrika Mashariki, Tanzania ndio ya mwisho kwa uwekezaji kwani inawekeza asilimia moja point something ya GDP katika elimu wakati Kenya ni asilimia tano na Rwanda kama sikosei amesema inawekeza mpaka asilimia 7 ya GDP katika elimu na hivyo ametoa wito kwa serikali kuongeza uwekezaji katika elimu.


Mh. Lowassa pia amemsifu Rais Kikwete kwa kufanikiwa katika maeneo mengine kama ujenzi wa barabara, hospitali, zahanati na kwenye maeneo mengine na kumtaka ajielekeze zaidi katika elimu. Mh. Lowassa amerudia kauli yake na kusisitiza kuwa msimamo wake utabaki kuwa ni elimu kwanza na sio kitu kingine.


Miongoni mwa viongozi waliohojiwa ni pamoja na Zitto Kabwe ambaye mbali na kushauri mambo mbalimbali pia amewataka waziri wa elimu na naibu wake pamoja na katibu mkuu wa wizara ya elimu kujiuzulu.


Source: Clouds FM mchana wa leo/jamiiforum

ASKOFU MDEGELA AFICHUA SIRI NZITO YA MAUAJI ZANZIBAR.


Askofu Dkt Mdegela
 

ASKOFU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi
yaIringa, Dk. Odernbarg Mdegela, ametoboa siri nzito kuhusu
uhalifu unaoendelea nchini, yakiwemo mauaji ya viongozi wa kidini na
uharibifu wa nyumba za ibada, kwamba upo nyuma ya vikundi kadhaa
vilivyopatiwamafunzo maalumu nje ya nchi kwa ajili ya utekelezaji wa
mpango huo.

Ingawa hakuvitaja moja kwa moja vikundi hivyo vinavyofadhiliwa
ilikutekeleza mkakati huo, Askofu Mdegela amedai kwamba vikundi
hivyo,vimepata mafunzo hayo na kwamba lengo ni kukamilisha mkakati
huo.

Mh. Membe kufungua Mkutano wa kwanza wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Oman (Joint Permanent Cooperation), tarehe 24 hadi 25 Februari, 2013


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb), (Pichani) anatarajiwa kufungua Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Oman (Joint Permanent Cooperation), tarehe 24 Februari, 2013 katika Hoteli ya Hyatt Regency (Kilimanjaro) iliyopo Dar es Salaam.
Mkutano huo pia utahudhuriwa na Waziri anayeshughulikia Masuala ya Mambo ya Nje wa Oman, Mhe. Yousuf bin Alawi bin Abdullah anayetarajiwa kuwasili nchini Jumamosi tarehe 23 Februari, 2013 saa 11 kamili jioni kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere uliopo mjini Dar es Salaam.
Mkutano huo unatokana na Makubaliano yaliyosainiwa tarehe 14 Oktoba 2009 kati ya nchi hizo mbili mjini Muscat, Oman.
Pamoja na mambo mengine, Mkutano huo utajadili masuala ya ushirikiano baina ya Tanzania na Oman katika Sekta za Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Nishati na Madini, Viwanda na Biashara, Elimu, Afya, Uwekezaji, Utamaduni na Habari.
Imetolewa na:
KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI,
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA,
DAR ES SALAAM.

RAIS MWAI KIBAKI WA KENYA AHITIMISHA ZIARA YAKE YA KISERIKALI NCHINI


 Rais Emilio Mwai Kibaki wa Kenya anayehitimisha leo Februari 21, 2013 ziara yake ya Kiserikali nchini akiagana na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali aliye pamoja na Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda pamoja na viongozi wengine katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wake Rais Emilio Mwai Kibaki wa Kenya anayehitimisha leo Februari 21, 2013 ziara yake ya Kiserikali nchini, wakisiliza taarifa ya pamoja ikisomwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wake Rais Emilio Mwai Kibaki wa Kenya anayehitimisha leo Februari 21, 2013 ziara yake ya Kiserikali nchini wakisimama kupokea heshima wakati nyimbo za taifa zikipigwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam.
 Vikundi mbalimbali vya ngoma vikitumbuiza wakati Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsindikiza mgeni wake Rais Emilio Mwai Kibaki wa Kenya anayehitimisha leo Februari 21, 2013 ziara yake ya Kiserikali nchini katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsindikiza mgeni wake Rais Emilio Mwai Kibaki wa Kenya anayehitimisha leo Februari 21, 2013 ziara yake ya Kiserikali nchini katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam.Picha na IKULU

MONTAGE CHARITY BALL KUFANYIKA LEO NDANI YA SERENA HOTELI

 Mkurugenzi wa Kampuni ya Montage Limited Teddy Mapunda akiongea na waandishi wa habari leo katika hoteli ya Serena iliyopo jijini Dar Es Salaam
Teddy Mapunda Akifafanunua Jambo Mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo Picha) leo katika Mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika hoteli ya Serena Kulia ni Msanii kutoka Nchini Kenya Kidumu atakaye fanya makamuzi pamoja na Peter Msechu na Barnaba
Mkurugenzi wa Kampuni ya Montage Limited Teddy Mapunda(katikati) Akiteta Jambo Na Msanii Kutoka Nchini Kenya Kidumu (kulia) wakati wa Mkutano na Wahandishi wa Habari uliofanyika katika Hoteli ya Serena Leo na Kushoto ni Msanii wa Bongo Fleva Peter Msechu
Mkurugenzi wa Montage Limited Teddy Mapunda akiongea na Waandishi wa habari (hawapo Pichani) wakati akiongelea Juu ya Tafrija ya Hisani ijulikanayo Kama Montage Charity Ball itakayofanyika Leo katika Hoteli ya Serena Kulia Kwa Teddy Mapunda Ni Peter Msechu na Kutoka Kushoto ni Msanii Barnaba na Kidumu kutoka Nchini Kenya
Pichani ni baadhi ya Wasanii  watakao tumbuiza kwenye tafrija ya Montage Charity Ball itakayofanyika jioni ya leo ndani ya Serena Hotel,jijini Dar.Kutoka kushoto ni Peter Msechu,Kidumu kutoka Kenya,Barnaba pamoja na Deo Mwanambilimbi ambaye ni kiongozi wa Kulunde Band.
Pichani shoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Montage,Teddy Mapunda (katikati) akizungumza na Waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akielezea kufanyika kwa tafrija maalum ya harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia wanawake wenye matatizo ya afya hapa nchini kupitia mfuko wa Montage Charity Ball,itakayofanyika jioni ya leo, Februari 22 kwenye Hoteli ya Serena,jijini Dar es Salaam

Aidha Teddy ameeleza kuwa malengo hasa ni kukusanya kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 100 kwa ajili ya kusaidia matibabu ya Wanawake wenye matatizo mbali mbali.Mgeni rasmi katika Tafrija hiyo anatarajiwa kuwa Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA),Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.Kulia kwake ni baadhi ya Wasanii watakaotumbuiza kwenye tafrija hiyo ambao ni Kidumu kutoka Kenya,Barnaba pamoja na Deo Mwanambilimbi ambaye ni kiongozi wa Kulunde Band na Peter Msechu ambaye hayupo pichani.

Maofisa wa FIFA wawasili Tanzania kukagua miradi ya maendeleo ya soka

Ashford Mamelodi. 
Ofisa Maendeleo wa Kusini mwa Afrika wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Ashford Mamelodi amewasili leo kwa ajili ya kufuatilia shughuli za maendeleo ya mpira wa miguu nchini.
Mamelodi, ambaye amekuwa msaada mkubwa kwa shughuli za maendeleo nchini Tanzania tangu alipoteuliwa kushika nafasi hiyo, pia amekuja kumtambulisha msaidizi wake, Patrick Onyango aliyeteuliwa kushika nafasi hiyo hivi karibuni.
Wakiwa nchini, wawili hao wanatarajiwa kupata taarifa ya maendeleo ya mradi wa kuweka nyasi bandia kwenye Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza, baada ya FIFA kuipa Tanzania mradi wa nne (GOAL Project 4) wa kuweka miundombinu kusaidia maendeleo ya mpira wa miguu.
Mwanza ilipata mradi huo baada ya Halmashauri ya Jiji hilo kukubali masharti ya mradi huo ya kulipia nakisi ya fedha zinazolipwa na FIFA, ambazo ni sh. milioni 700. Mradi huo wa kuweka nyasi bandia Nyamagana utagharimu sh. milioni 900, hivyo nakisi y ash. milioni 200 italipiwa na Jiji la Mwanza.
Pia Mamelodi na Onyango watapata taarifa ya maendeleo ya Uwanja wa Gombani uliowekwa nyasi za bandia kwa msaada wa FIFA katika mradi wa GOAL Project 3; na pia kupata mikakati ya maendeleo ya TFF kwa mwaka 2013, ikiwa ni pamoja na kozi na semina mbalimbali zitakazofanyika nchini mwaka huu.
Mamelodi na Onyango pia watapata taarifa ya maendeleo ya uboreshaji wa mashindano ya Copa Coca-Cola baada ya FIFA kuingia rasmi kwenye mashindano hayo mwaka jana kwa kuendesha kozi kwa walimu wa timu za kombaini ya mikoa na waamuzi.
Kwa sasa mashindano hayo yanashirikisha vijana wenye umri chini ya miaka 17, lakini FIFA inataka yahusishe umri mdogo zaidi ili kuendeleza soka ya vijana na kushirikisha kikamilifu shule. Maofisa hao wataondoka nchini Jumatatu asubuhi.

TANZANIA YATINGA KWENYE KUMI BORA NDANI YA LONDON FASHION WEEK

=

 Wabunifu mitindo Jackline Kibacha na Anna Lukindo wakisindikizwa na Mama Balozi Joyce Kallanghe na Mama Rose Kiondo
 Nje ya Jumba la Somerset
 Wanamitindo wa Kitanzania kwenye London Fashion Week 2013. Anna Lukindo, Christine Mhando, Jacquline Kibacha
 Anna, Jack na Duane kutoka Jamaica
 Anna Luks
Mama Rose Kiondo, Samson Soboye, Mama Joyce Kallaghe, Anna Lukindo, Christine Mhando, Jacquline Kibacha
 Barabara ya The Strand copy
London Fashion Week 2013.Picha zote za Urban Pulse
Imeandikwa na Urban Pulse na Freddy Macha

Jumapili mchana  wilaya ya Westminster jijini  London ilikuwa na mashindano ya ubunifu na urembo katika maonyesho  ya kimataifa ya London Fashion Week. Mashindano haya yalifanyika jumba la Somerset lililosimama imara  kwenye upembe wa  kaskazi ya mto Thames.
Maonyesho ya London Fashion Week, bado yanaendelea jumba hili  la Somerset toka tarehe 14 hadi tarehe 28. Wiki hizi mbili nzima zitakutanisha kila mtu anaye husika na biashara ya mavazi na urembo. Magwiji na mapapa wa mitindo, wabunifu, walimbwende, watafuta vipaji, wafanya biashara, wazalishaji mali ghafi na wamiliki viwanda.  Wote hukutana katika maonyesho haya. Hapa si vipaji tu vinavyojionyesha, bali pia watu wa biashara.
Siku hii Tanzania ilikuwa moja ya nchi mbili tu za Kiafrika zilizochaguliwa na British Council na LFW kushiriki kwenye mashindano  ya kutafuta vipaji chipukizi kwenye tasnia ya ubunifu wa mavazi na urembo.  Watanzania Anna Lukindo, Jacqueline Kibacha na  Christine Mhando ndio wasanii waliobeba bendera ya taifa letu na kutuwakilisha katika mashindano haya ya kimataifa yanayofanyika kila mwaka kwa zaidi ya miaka 27 sasa.
Katika kuunga mkono maendeleo ya Tanzania na Watanzania,  Ubalozi wetu  Uingereza na Bodi ya Utalii Tanzania, nao pia walichukua nafasi hii kuwasaidia wananchi hawa kufanikisha mahitaji yao ya ushindani. Ubalozi umetoa Ukumbi wa Nyumba Ya Tanzania ulioko Bond Street ili wasanii hao waweze kuonyesha nguo na sanaa zao kwa juma zima kama sheria za London Fashion Week zinavyoamuru. Vile vile Bodi ya Utalii ya Tanzania imesaidia katika mchango  wa mali ghafi zilizotumika katika shughuli hizi  ili kuiuza Tanzania kimataifa.
Mshindi wa tukio alikua Estonia. Ingawa  Tanzania haikuwa mshindi wa mwanzo- ilichaguliwa kati ya Kumi Bora jambo ambalo limetikisa nyoyo na vichwa vya  waandaaji, wabunifu,wafanya biashara na watafuta vipaji vya kimataifa. Hii ni mara ya kwanza kwa taifa letu kushiriki katika shughuli na  wote wameguswa na kupumbazwa na usanii wa hali ya juu ulioonyeshwa na wasanii  watatu wa Kitanzania.   Lukindo, Mhando na Kibacha wamechukua nafasi waliyopewa kwa mikono miwili na wote wameisogeza Tanzania hatua moja zaidi ndani ya ulingo wa kimataifa na katika biashara hii ya mavazi na urembo ambayo inasemekana ina thamani ya  Pauni Billioni 10  ama  shilingi Trillion 25 za Tanzania.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...