Friday, September 26, 2014

BAWACHA YAPANGA KUMUONA RAIS KIKWETE KWA MAANDAMANO...!!!


Mwenyekiti wa Baraza la wanawake Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bawacha), Halima Mdee akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusu mandamano ya kupinga kuendelea kwa vikao vya Bunge la katiba. Kulia ni Makamu Mwenyekiti Bara, Hawa Mwaifunga.

Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) limetangaza maandamano kwenda Ikulu kumuomba Rais Jakaya Kikwete asikubali kutia saini Rasimu ya Katiba inayopendekezwa iwapo itapitishwa na Bunge.

Mwenyekiti wa Bawacha, Halima Mdee alisema jana kwamba maandamano hayo yatafanyika mwishoni mwa wiki ijayo, baada ya maandalizi yatakayofanyika kwa siku saba kuanzia jana kukamilika.

Mdee ambaye pia ni mbunge wa Kawe, alisema baraza hilo limeamua kuitisha maandamano hayo ili kuwakilisha kilio cha wanawake ambao ndiyo waathirika wa kwanza pale nchi inapokuwa katika mfumo usio wa haki.

Alivitaka vyombo vya dola hasa polisi kujitokeza kuwasindikiza na kuandamana nao kwa kuwa nao ni miongoni mwa Watanzania ambao wataathiriwa na uamuzi usiolenga kujenga umoja wa kitaifa.

Hata hivyo, Polisi imetahadharisha kuwa itaendelea kuwachukulia hatua za kisheria wanachama wa Chadema watakaojiingiza katika maandamano yaliyopigwa marufuku nchini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA WATISHIWA MAISHA


Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, wakiwa katika vikao vya Bunge hilo Dodoma jana. Picha ya Maktaba

Siku tatu kabla ya Bunge la Katiba kuanza kupigia kura Rasimu ya Katiba inayopendekezwa, watu wasiojulikana wameanza kusambaza vitisho vya kuwatia hofu wajumbe wa Bunge hilo.

Watu hao wamesambaza vipeperushi katika maeneo mbalimbali ya mji wa Dodoma usiku wa kuamkia jana, wakiwataka wajumbe kutoingia bungeni vinginevyo yatakayowapata watajuta, huku wajumbe kutoka Zanzibar wakitishiwa kwa ujumbe wa simu kupitia mtandao wa WhatsApp.

Tayari, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd ametoa kauli kuhusu vitisho hivyo akisema Serikali itachukua kila hatua kuhakikisha wajumbe kutoka visiwani humo ambao wamekuwa wakipokea vitisho wanakuwa salama.

Mbali na kusambazwa kwa karatasi hizo, maandishi mekundu yamechorwa katika kuta za jengo la Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma yakisomeka, “No Katiba. No ufisadi.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 26, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ZAIDI YA RAIA 3, 000 WA ULAYA NI WAFUASI WA I.S


Inakisiwa kuwa zaidi ya raia 3000 kutoka Ulaya ni wafuasi wa Islamic State
Idadi ya raiya kutoka Uropa wanaojiunga na kundi la wapiganaji wa Kiislamu nchini Syria na Iraqi imeongezeka hadi zaidi ya 3,000 kulingana na mkuu wa kitengo cha kupambana na ugaidi bara la ulaya.
Gilles de Kerchove ameonya kuwa mashambulizi ya hewa yanayofanywa na nchi za Magharibi yataongezea hatari ya mashambulizi ya kulipiza kisasi katika bara la Ulaya.
Vikosi vikiongozwa na Marekani vimetekeleza mashambulizi ya hewa mia mbili dhidi ya wanamgambo wa Islamic state wa Iraqi tangu Agosti na Jumatatu iliyopita wakaanza kulenga wale walioko Syria.
Bunge la Uingereza litapiga kura kwa mashambulizi ya hewa dhidi ya Iraqi siku ya Ijumaa.
Kundi la IS wameteka sehemu kubwa za Syria na Iraqi katika miezi ya hivi karibuni.
CIA inakisia kuwa kundi la IS linaweza kuwa na wapiganaji mpaka 31,000 huko Iraq na Syria, mara tatu zaidi ya wale waliohofiwa.
Mashambulizi haya yaliotekelezwa siku ya Alhamisi na ndege za Marekani, Saudi na UAE zilikuwa zinalenga mitambo 12 ya kusafisha mafuta nchini Syria .
Msemaji wa Pentagon Rear Admiral John Kirby alisema kuwa kusudi la mashambulizi haya ya hewa halikuwa kuwaua wanamgambo hao lakini ilikuwa kuharibu maeneo ambayo yalikuwa yakiletea kundi hilo fedha kupitia soko nyeusi.
Baadaye, siku ya Ijumaa, wabunge wa Uiungereza wataulizwa kuunga mkono mashabulizi dhidi ya wanamgambo wa IS Iraqi lakini sio Syria. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TALIBAN YATEKA MJI WA GHAZNI AFGHANISTAN


Afisa wa usalama akishika doria katika mji wa Ghazni
Maafisa huko mashariki mwa Afghanistan wanasema kuwa wapiganaji wa Taliban wamechukua udhibiti wa baadhi ya Wilaya katika jimbo la Ghazni.
Watu zaidi ya 70 wanahofiwa kufariki katika Wilaya ya Ajrestan katika mapambano hayo ya kuteka vijiji vyao hapo jana jioni.
Ripoti zinasema Kuna makabiliano makali ya risasi huku walinda usalama wakifanya kila wawezalo kujaribu kutwaa tena wilaya hizo zilizotekwa.
Ghazni ni mji muhimu umnaochukuliwa kama mlango unaounganisha mji mkuu Kabul na eneo la kusini mashariki mwa nchi hiyo.
Wadadisi wa hali ya usalama nchini humo wanasema kuwa kutekwa kwa mji huo ni ilani kwa miji iliyoko karibu na
Ghazni huenda pia zikatekwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

AZAM YAZIPIGA BAO SIMBA NA YANGA


Klabu ya Azam FC ndiyo inayoongoza kwa kulipa posho kubwa wachezaji wake kati ya timu zote 14 zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa wachezaji wa Azam ndiyo vinara wa kupata posho zilizoshiba wakizizidi Yanga na Simba ambao kwa kauli yao wamekubali matokeo.

Mgawanyo huo unaonyesha kwamba Azam kila inaposhinda mechi moja ya ligi inavuna kiasi cha Sh 4milioni, ambapo kila mchezaji anapewa Sh130,000 kiwango ambacho ni kikubwa kwa Simba na Yanga

Kitu kibaya kwa Azam ni pale inapotoa sare au kufungwa, ambapo hakuna chochote watakaochopata ingawa Simba na Yanga huambulia kitu zikitoka sare.

Hata hivyo, kiutaratibu unaonekana utaratibu unaotumiwa na Simba ndiyo mzuri kwani wachezaji wake hupata 40 % ya pato la mlangoni endapo timu hiyo inaibuka na ushindi huku ikiambulia 20% inapopata sare katika michezo yao.

Yanga, ambayo hivi karibuni wachezaji wake waliwasilisha maombi maalumu juu ya kutaka kubadilishiwa viwango vya posho, mpaka sasa wanaambulia kiasi cha Sh70,000 kila mchezaji kwa mechi wanayoshinda na hupata Sh 30,000 wanapopata sare.

“Hatuwezi kushindana na Azam, unajua Azam hata kama haupo katika orodha ya wachezaji wanaocheza mechi, Sh130,000 ipo palepale, lakini Simba na Yanga haipo hivyo, mchezaji anayecheza mechi anapata zaidi ya yule aliyekosa mechi,” alisema mmoja wa mabosi wa Simba ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TFF YAZIKINGIA KIFUA SIMBA NA YANGA


Wachezaji wa kimataifa wa Yanga, Gelinson Santos ‘Jaja’ (kushoto) na Andrey Coutinho. Picha na maktaba.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limezikingia ‘kifua’  Simba na Yanga na kueleza kuwa haliwezi kwa sasa kuzinyang’anya pointi kwa kuchezesha wachezaji wasio na vibali vya kufanya kazi  nchini.

Katibu Mkuu wa TFF, Celestine Mwisigwa alisema jana  kuwa suala hilo lipo kisheria zaidi.

“Kama kweli Simba, Yanga wamechezesha wachezaji wasio na vibali vya kufanya kazi nchini ni kosa na Serikali, inaweza kuwachukulia hatua klabu na wachezaji wao,” alisema Mwesigwa.

Hata hivyo, alisema kuwa adhabu ya kunyang’anywa pointi haielezi moja kwa moja na hadi sasa hakuna timu iliyokwenda TFF kulalamikia suala hilo.

“Hatuwezi sisi kuzinyang’anya pointi kama hakuna timu iliyokuja kwetu kulalamika, isitoshe Simba nimezungumza nao leo (jana) baada ya gazeti  kuripoti habari hiyo wakasema tayari wamewaombea vibali wachezaji na kocha wao, hivyo siwezi kujua nani mkweli, Simba na Uhamiaji,” alisema .

Juzi, Idara ya Uhamiaji ilitoa tamko kuhusu baadhi ya wachezaji na makocha wa kigeni wa timu hizo kutokuwa na vibali  vya  kufanya kazi nchini na kueleza kuwa tayari imeanza msako wa kuwakamata watakapoonekana wakijihusisha na mazoezi au mechi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...