Friday, September 26, 2014

TFF YAZIKINGIA KIFUA SIMBA NA YANGA


Wachezaji wa kimataifa wa Yanga, Gelinson Santos ‘Jaja’ (kushoto) na Andrey Coutinho. Picha na maktaba.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limezikingia ‘kifua’  Simba na Yanga na kueleza kuwa haliwezi kwa sasa kuzinyang’anya pointi kwa kuchezesha wachezaji wasio na vibali vya kufanya kazi  nchini.

Katibu Mkuu wa TFF, Celestine Mwisigwa alisema jana  kuwa suala hilo lipo kisheria zaidi.

“Kama kweli Simba, Yanga wamechezesha wachezaji wasio na vibali vya kufanya kazi nchini ni kosa na Serikali, inaweza kuwachukulia hatua klabu na wachezaji wao,” alisema Mwesigwa.

Hata hivyo, alisema kuwa adhabu ya kunyang’anywa pointi haielezi moja kwa moja na hadi sasa hakuna timu iliyokwenda TFF kulalamikia suala hilo.

“Hatuwezi sisi kuzinyang’anya pointi kama hakuna timu iliyokuja kwetu kulalamika, isitoshe Simba nimezungumza nao leo (jana) baada ya gazeti  kuripoti habari hiyo wakasema tayari wamewaombea vibali wachezaji na kocha wao, hivyo siwezi kujua nani mkweli, Simba na Uhamiaji,” alisema .

Juzi, Idara ya Uhamiaji ilitoa tamko kuhusu baadhi ya wachezaji na makocha wa kigeni wa timu hizo kutokuwa na vibali  vya  kufanya kazi nchini na kueleza kuwa tayari imeanza msako wa kuwakamata watakapoonekana wakijihusisha na mazoezi au mechi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Abbas Irovya alisema makocha wa Yanga,  Leonardo Neiva na Marcio Maximo na wachezaji Genilson Santos ‘Jaja’ na Andrey Coutinho bado hawajapata vibali, ingawa tayari uongozi wa klabu hiyo umewasilisha maombi yao.

Alisema wachezaji wote wa kigeni wa Simba  pamoja na kocha mkuu, Patrick Phiri hawana vibali vya kufanya kazi nchini na hadi juzi jioni  idara hiyo haikuwa imepokea maombi yoyote ya klabu hiyo kuwaombea vibali hivyo waajiriwa wake hao.

Yanga ilimtumia Jaja kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii hivi karibu  dhidi ya Azam, sambamba na kocha Maximo, lakini pia iliwatumia wachezaji hao kwenye mechi yao ya kwanza ya Ligi Kuu dhidi ya Mtibwa ambayo walifungwa 2-0.

Simba pia iliwatumia wachezaji wake wa kigeni kwenye mechi dhidi ya Coastal Union ambao hawana vibali hivyo.

Emmanuel Okwi ana kibali cha Yanga ambacho kwa mujibu wa Irovya kinaonyesha kuwa mwajiri wake ni Yanga na wala si Simba anakocheza  sasa.

Rais wa Simba, Evance Aveva alipotafutwa na gazeti hili jana  kutoa ufafanuzi wa suala hilo aligoma kuzungumza na kutaka atafutwe saa 11.00 jioni na alipotafutwa muda huo hakupokea simu.

“Siko katika ‘mudi’ ya kukujibu swali lako, nitafute baadaye nitakujibu,” alisema Aveva na kukata simu huku makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ akikataa kulizungumzia suala hilo.
Wakati huo huo, Uhamiaji pia imeanza msako kwenye klabu za Kagera Sugar, Azam, Yanga na Coastal Union ambazo pia zinao wachezaji wa kigeni. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Kamishna  Irovya, alisema oparesheni hiyo itafanyika kwenye klabu hizo zenye wachezaji na makocha wa kigeni.
“Tunachokita ni sheria kuchukua mkondo wake, tayari tumewasiliana na Uhamiaji Kagera ili kutupa taarifa juu ya kocha wa Kagera Sugar kufanya kazi hapa nchini na wakati wowote kuanzia sasa tutakuwa tumepata majibu ya hilo, mbali na Kagera kuna hii timu ya Coastal Union wao waliomba vibari vya muda mfupi kwa wachezaji wao wa kigeni ambavyo vinakwisha Desemba 16 mwaka huu.
Ligi Kuu Bara itaendelea wikiendi hii katika viwanja mbalimbali.

Na Mwananchi

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...