Monday, June 24, 2013

MSHTAKIWA WA EPA ASIMULIA JINSI WAJANJA WALIVYOMZIDI ‘KETE’ KWENYE AKAUNTI YAKE

Godfrey Mosha 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Principal Ltd, Godfrey Mosha amesimulia jinsi Benki ya Akiba Commercial (DCB), tawi la Kariakoo, ilivyoidhinisha malipo ya fedha kwa mtu mwingine kutoka akaunti yake ndani bila yeye kujua.
Mosha ni mmoja wa washtakiwa katika kesi ya  wizi wa fedha kwenye  Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Pamoja na wenzake, Bahati  Mahenge, Manase Makale, Davis Kamungu na Eda Makale, wanakabiliwa na kesi ya wizi wa Sh1.86 bilioni za EPA, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kuipitia Kampuni ya Changanyikeni Residential Complex.
Katika kesi hiyo dhidi ya DCB, inayosikilizwa na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Warialwande Lema, Mosha anaidai benki hiyo Sh46.8 milioni, zilizolipwa kwa mtu asiyemfahamu kwa kutumia hundi nne tofauti na tarehe tofautitofauti.
Katika ushahidi wake Ijumaa  iliyopita, akiongozwa na Wakili wake, Michael Ngalo, Mosha alidai  alibaini uhamisho huo wa fedha  kutoka  akaunti yake namba 0400438671, Novemba 15, 2011 alipochukua taarifa ya benki.

SOGGY DOGGY NAE ATANGAZA KUGOMBEA UBUNGE 2015

 
Nguli wa muziki wa kizazi kipya Soggy Doggy Anter aka Anselm Tryphone Ngaiza leo ametangaza nia ya kugombea Ubunge wa jimbo la Segerea, Dar es Salaam kupitia tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, MWAKA 2015.
Msanii huyo ametiririka katika ukurasa wake wa facebook, na hapa nanukuu "Shikamoo Mbunge wa Segerea, Makongoro Mahanga, imetosha sasa nadhani ni zamu yangu kuwatumikia wana-segerea 2015 kupitia CHADEMA" mwisho wa kunukuu. Pia kwenye ukurasa wake wa twitter imesomeka ivyo ivyo.
 
Nilipoongea na Msanii huyu aliniambia ameamua kufanya ivi ili kuwasaidia na kuwaletea maendeleo wana-segerea na watanzania kiujumla.
Pia aliniambia ameamua kugombea kupitia CHADEMA, kwasababu ndo chama kinachoweza kufanya mabadiliko kwenye jamii kwasasa.
Nikamuuliza je amemfuata rafiki yake Joseph Mbilinyi aka "SUGU" katika chama icho, akasema hapana, hawajawahi kupewa ushawishi wowote wa kisiasa na Nguli huyo wa muziki wa Hip Hop.
Wana-Segerea kazi kwenu kijana ameamua na amedhamiria.

SIKU 17 KABURINI... FAMILIA YASHANGAA RIPOTI KIFO CHA NGWEA.


ZIKIWA zimekatika siku 17 tangu aliyekuwa mkali wa Hip Hipo Bongo, Albert Kenneth Mangweha ‘Ngwea’ alale kaburini, familia imeshangaa kupelekewa vitu vingine bila ripoti ya kifo chake.

Kwa mujibu wa mtu wa ndani wa familia hiyo, Millard Ayo wa Clouds FM ndiye aliyepewa majukumu ya kushughulikia kila kitu baada ya kifo tata cha Ngwea kilichotokea Johannesburg, Afrika Kusini Mei 28, mwaka huu.
 
Chanzo hicho kilieleza kuwa mara baada ya mwili wa marehemu Ngwea kuletwa Bongo, familia ilitarajia kukabidhiwa kila kitu ikiwemo ripoti ya nini kilimuua Ngwea.
 
“Hakuna swali tunaloulizwa kama ripoti ya kifo cha Albert (Ngwea). Kila mtu anataka kujua nini hasa kilitokea hadi akafa kwa sababu maneno ni mengi sana.
“Ripoti ndiyo ingeweza kumaliza maneno na kuwafunga watu midomo,” kilisema chanzo chetu mjini hapa.

Kiliendelea kunyetisha kuwa mwili ulipofika ilibidi familia ‘idili’ na maziko kwanza ambapo Millard aliahidi kuipeleka baada ya msiba.

“Kweli Millard alikuja tena juzikati, alichokabidhi ni cheti cha kifo (death certificate) na hati ya kusafiria ya marehemu Ngwea,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
“Familia nzima ilishangaa kwani ilikuwa ni tofauti na tulichotarajia lakini tulipomuuliza kuhusu ripoti ya kifo cha Ngwea, alikabidhi barua iliyoelezea kuwa chanzo cha kifo bado kinachunguzwa huko Afrika Kusini ambapo wanafanya critical investigation (uchunguzi wa kina) na tutajulishwa mara tu uchunguzi huo utakapokamilika.”

Baada ya kudakishwa habari hizo, Ijumaa Wikienda lilizungumza na mama wa marehemu Ngwea, Denisia Mangweha ambaye alikiri kupokea vitu hivyo na kwamba ni kweli familia ilijiandaa kupokea ripoti ya kifo lakini haikuwa hivyo.
Credit: GLP

SUMAYE AMPONDA LOWASSA KANISANI...!!!

WAZIRI Mkuu mstaafu Frederick Sumaye amesema anashangazwa na baadhi ya viongozi wa dini kutoa sifa nzuri kwa watu wanaochanga fedha na si kuzingatia uadilifu na wema walionao.



Kiongozi huyo alitoa kauli hiyo jana katika sherehe za kutimiza miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), zilizofanyika katika Chuo Kikuu cha Makumira mkoani Arusha.


Sumaye alihoji kuwa inakuwaje wema wa baadhi ya watu unajitokeza zaidi wakati nchi ikielekea kwenye uchaguzi unaotegemewa kufanyika mwaka 2015.


Sherehe hizo za kutimiza miaka 50 zilifanyika katika Chuo Kikuu cha Makumira na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa KKKT kutoka sehemu mbalimbali duniani pamoja na maaskofu wote wa dayosisi 20 zilizopo nchini.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNI 2, 2013 YA HABARI,UDAKU NA MICHEZO

DSC 0030 53cf9
DSC 0033 4b8a4

BAADA YAKUPIGWA MAKOPO DODOMA, HICHI NDICHO ALICHOKIONGEA OMMY DIMPOZ

 
 

MH. SUGU AMUOMBA RADHI WAZIRI MKUU

Mhe Sugu
Waziri Mkuu, Mhe. Pinda
BAADA ya kauli yake iliyoibua mjadala mkubwa nchini dhidi ya Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda kufuatia majibu yake aliyoyatoa wiki iliyopita Bungeni kwa kutaka Polisi kuendelea kuwapiga raia, Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe Joseph Mbilinyi 'Sugu', aomba radhi.
Sugu amemuomba radhi mhe Pinda na watanzania kwa ujumla kwa lugha aliyotumia katika kuonyesha hisia zake juu ya kauli aliyoitoa mhe Pinda bungeni.

Kupitia akaunti yake ya Facebook, Mbunge huyo machachari amenukuliwa akiwaomba radhi Watanzania waliokerwa na kauli yake iliyodai kwamba Tanzania haijawahi kuwapata Waziri Mkuu kama Mhe. Pinda kwa kusema;
"Ndugu watanzania, naombeni radhi kwa tusi nililolitoa kwa mhe Pinda, kwani nilikua nimeghafirika, halikuwa kusudio langu kumtukana mmoja wa viongozi wa nchi."

ANGALIA PICHA ZA MAZISHI YA MAMA MZAZI WA BARNABA (BI MARIAMUARUBETH)

Mama Diamond

Siku ya leo jumapili ndio ilikuwa siku husika kabisa katika kutoa heshima za mwisho kwa Bi Mariamu 
Arubeth aliezaliwa 4/12/1967 na kufariki tarehe 22/6/2013.


Zifuatazo ni picha za Mazishi Ya Mama mzazi wa Barnaba kuanzia nyumbani hadi makaburini....

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...