Wednesday, June 07, 2017

SHILOLE: WATOTO WANGU HAWATAIGA MAISHA YANGU


MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, amesema kwamba watoto wake hawataiga maisha wala mavazi anayovaa kwenye shoo zake wala maisha ya sanaa anayoishi kwa kuwa wanatambua yupo kazini kwa ajili yao.

Shilole akiongea na mwandishi wa habari hii alisema kwamba, malezi anayowalea watoto wake ni tofauti na maisha anayoishi yeye na watoto hao wanatambua kwamba mama yao ni msanii hivyo hawataiga anachofanya.

 “Watoto wangu nawalea katika maadili kama mama, siwezi kuwalea maisha ya kistaa kama ninavyoishi mimi na wanatambua kwamba mama yao nipo kazini kwa ajili yao na pia hawana ndoto za kuishi maisha yangu ya kisanii,” alieleza Shilole.

Shilole aliongeza kwamba licha ya kulea watoto wake kwa maadili ya dini, lakini hataacha kuendelea kuwapa elimu, mafunzo ya maisha na biashara.

HUDDAH: SITAKI KUOLEWA

MWANAMITINDO maarufu nchini Kenya, Huddah Monroe, amefunguka na kusema kwamba hana mpango wa kuolewa katika maisha yake.

Mrembo huyo ambaye hakauki mitandaoni, amekuwa akihusishwa kutoka na nyota wa soka wa timu ya Taifa ya Kenya na klabu ya Tottenham ya nchini England, Victor Wanyama, lakini amekuwa akikana taarifa hizo na sasa ametangaza kwamba hana mpango wa kuolewa kwenye maisha yake.

“Kila mtu ana mipango yake, hivyo kwa upande wangu sina mpango wowote wa kuolewa. Hata hivyo, kama itakuja kutokea nikaolewa hatakuwa mwanamume wa Nigeria.

“Maana kuna taarifa kwamba natoka na Wizkid, sikushangaa sana kwa kuwa niliwahi kuposti picha nikiwa na msanii huyo nilipokutana naye nchini Marekani, picha hizo zikaleta maneno mengi nina uhusiano naye wa kimapenzi hakuna ukweli na sitaolewa na mwanamume wa Nigeria,” alisema Huddah.

ACT WAZARENDO WAMVUA CHEO MAMA MGHWIRA

Chama cha ACT Wazalendo kimmevua uongozi aliyekuwa mwenyekiti wake, Anna Mgwhira ambaye ameteuliwa na Rais John Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Chama hicho kimefikia hatua hiyo kwa kuzingatia ibara ya 17 ya katiba yake ambayo inatamka kuwa kiongozi wa chama atakoma kuendelea na madaraka yake iwapo atashindwa kutekeleza majukumu yake.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano, Kaimu Kiongozi wa ACT, Samson Mwingamba alisema kamati ya uongozi wa ACT ulikutana leo lengo kuu ni kutafakari lililotokea kuona namna gani Mgwhira anaweza kutimiza majukumu yake kama Mwenyekiti na Mkuu wa Mkoa.

“Kama chama baada ya kutafakari kwa kina na baada ya mashauriano baina yake na viongozi kutumia katiba ya chama anakoma kuwa kiongozi kwa kuwa kutakuwa na mgongano wa majukumu, maslahi hivyo anakoma kuwa mwenyekiti,” alisema Mwigamba.

Mwigamba alisema kamati ya chama imemchagua Yeremia Maganja kuwa  Kaimu Mwenyekiti na kamati ilimpongeza Rais Magufuli kwa kumteua Mgwhira.

Hata hivyo, Mwigamba alisema Mghwira bado ataendelea kuwa mwanachama halali wa chama hicho.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...