Friday, May 31, 2013

DIAMOND AMPIGIA MAGOTI JOKATE NA KUMUOMBA MSAMAHA

MKALI wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, ameibuka na kuelezea kuhusu uhusiano wake na mpenzi wake zilipendwa, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ ambaye ni mwigizaji na modo moto wa kuotea mbali Tanzania.


Nasibu Abdul ‘Diamond’ akiwa na Jokate Mwegelo ‘Kidoti’.

Akizungumza kwa uhakika kabisa, Diamond alisema inampasa amuombe radhi Jokate kwa sababu katika uhusiano wao, Jokate hakuwahi kumkosea ila yeye ndiye tatizo na chanzo cha kuachana kwao.
Diamond alisema hayo kwenye mahojiano na Mtangazaji Zamaradi Mketema katika Runinga ya Clouds kwenye Kipindi cha Take One, kilichorushwa juzi Jumanne usiku kituoni hapo.

DIAMOND ANAFAFANUA
“Inanipasa nimuombe radhi Jokate. Ni kweli nilimtenda vibaya wakati wa mapenzi yetu. Hakukosea sana maana hakuwahi kufanya jambo lolote kinyume. Sijui niseme nini lakini nataka kueleza wazi kuwa mimi ndiyo sababu ya kuachana kwetu na ilitokea tu.


Diamond na Jokate wakicheza.

“Naamini hilo jambo lilimuuma sana, maana nakumbuka wakati ule, baada ya mimi kurudi kwa Wema (Sepetu), watu walimwandama sana kwa maneno na alionekana msaliti lakini ukweli ni kwamba nilimpenda sana lakini ndiyo hivyo, siwezi kufafanua zaidi.
“Kutoka moyoni mwangu, namuomba msamaha Jokate, kama hatanisamehe nitaendelea kumuomba mpaka naingia kaburini. Sina raha kabisa kutokana na jambo hilo. Lazima niwe mkweli.”

JACQUELINE WOLPER
Diamond alikwenda mbali zaidi na kuwazungumzia baadhi ya wasichana aliowahi kutoka nao kimapenzi akiwemo mwigizaji Jacqueline  Wolper ambaye alisema ni mwanamke aliyempenda sana, ndiyo maana alimtungia wimbo wa Mawazo.

PENNY SASA
Kwa upande wa mpenzi aliye naye sasa, Mtangazaji wa Runinga ya DTV, Penieli Mungilwa ‘Penny’ alisema ni mwanamke mtulivu na sahihi kwake kwa sababu anatambua majukumu yake kwake, pia anamheshimu.

“Huyu kwa kweli ana karibu sifa zote alizonazo Wema ila uzuri wa Penny ananiheshimu sana. Hafanyi mambo yake hadharani. Unajua wakati nikiwa na Wema hata kama akifanya mambo yake siku mbili au tatu baadaye nayaona kwenye magazeti, tofauti na Penny ambaye kwangu mimi naona ananiheshimu, hata kama anafanya mambo yake ni kwa siri.”

BREAKING NEWZZZZZZZZZZZ...!!! NECTA YATANGAZA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA (ACSEE 2013)


Matokeo ya kidato cha 6 yametangazwa. Ufaulu umeongezeka mara dufu zaidi ya wanafunzi 90% wamefaulu. Shule zilizoongoza ni
    1. Marian Girls
    2. Mzumbe

f Matokeo ya kidato cha sita (ACSEE) 2013 - Link 1

f Matokeo ya kidato cha sita (ACSEE) 2013 - Link 2

TANGAZO MUHIMU KWA UMMA KUTOKA BENKI KUU YA TANZANIA

 
 Benki Kuu inapenda kuutahadharisha umma kuwa katika siku za karibuni kumekuwepo
na mtandao wa matapeli unaotumia TOVUTI ifuatayo www.jakayafoundation.wapka.mobi/index.html

Mtandao huo unajidai kuwa ni Taasisi ya Fedha ijulikanayo kwa jina la Jakaya foundation ambayoinamilikiwa na Benki Kuu chini ya utawala wa bodi kuu ya mikopo inayotolewa na serikali kupitia sekretariat ya Utumishi wa umma ofisi ya Rais. 


Matapeli hao wanaeleza kwamba Taasisi hiyo inatoa mikopo ndani ya masaa 24 kwa Mtanzania yeyotemwenye umri kuanzia miaka 18 endapo atajiunga kwa kulip a ada ya shilingi 37,000/=.BENKI KUU INAUARIFU UMMA KUWA HAIITAMBUI NA WALA HAIHUSIANI KWA NAMNA YOYOTE ILE NA TAASISI INAYOELEZWA KWENYE TOVUTI HIYO.


Kwa taarifa hii, Benki Kuu inatoa tahadhari kwa Wananchi kutojihusisha na Taasisi hiyo ya kitapeli kwa ajili ya kupata huduma za mikopo kama ambavyo inadai.
 

IMETOLEWA NA
IDARA YA UHUSIANO NA ITIFAKI
BENKI KUU
YA TANZANIA
DAR ES SALAAM.
29/5/2013

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MAY 31, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS HAYA HAPA

14 b3187

1 1c845

HAWA NDIO WADADA WALIO FUNGA NDOA YA JINSIA MOJA

Mashoga hao wakifungishwa ndoa kwenye ofisi ya msajili nchini Uingereza.
Wanawake wawili raia wa Pakistan wameweka historia kama Waislamu wa kwanza wa jinsia moja kufunga ndoa nchini Uingereza.

Rehana Kausar, miaka 34, na Sobia Kamar, miaka 29,wameweka historia pale walipofunga pingu za maisha katika sherehe iliyofanyika kwenye ofisi ya msajili, kisha haraka wakaomba hifadhi ya kisiasa baada ya kuwa wamefunga ndoa, wakidai kwamba maisha yao yatakuwa hatarini kama wakirejea kwenye nchi yao ya asili.
Wakishuhudiwa na wasimamizi wao na marafiki wawili, wanandoa hao walivalia mavazi meupe asilia ya ndoa pale walipofunga ndoa mjini Leeds, West Yorkshire.
Wawili hao, kutoka mikoa ya Lahore na Mirpur ya Pakistan, walisema walipokea vitisho vya kuuawa kutoka kwa wapinzani nchini Pakistan - ambako mahusiano ya jinsia moja ni kinyume cha sheria na kuchukuliwa ni kusaliti Uislamu.
Na tangu habari za ndoa yao mapema mwezi huu kuzagaa, wanandoa hao walidai kupokea vitisho vya kuuawa hata kutoka nchini Uingereza 
Kabla ya zoezi hilo, hata msajili aliwashauri wawili hao kufikiria kwa makini kuhusu uamuzi wao wa kufunga ndoa sababu ya mtazamo wa baadhi ya Waislamu kuhusu mahusiano ya jinsia moja.

Thursday, May 30, 2013

Wema Afunguka na Kusema: "Sikuwahi kumsaliti Diamond na tulikuwa tunapendana sana"

 
Miss Tanzania mwaka 2006 na muigizaji wa filamu Wema Sepetu amefunguka kupitia jarida jipya la Mzuka kuwa katika uhusiano wake wote na Diamond hakuwahi kumsaliti.

Wema ambaye yupo kwenye cover la jarida hilo linalotolewa na  Bongo5,amefunguka kwa kusema kuwa yeye na Diamond walikuwa wakipendana sana.


“Maisha yangu yote tangia nimeanza mapenzi na Naseeb naweza kusema kuwa sikuwahi kuwa unfaithful. I used to be very faithful to him na tulikuwa tunapendana sana. With Naseeb nilikuwa nimesharidhika na maisha ambayo niko nayo,” amefunguka Wema.

Wema amefunguka pia kuhusu jinsi Diamond alivyomcheat na Jokate kwa kusema, “nadhani pia inacost mwanaume akishajua kwamba anakutawala in one way or another so labda ni shetani au ni ibilisi alimuingilia baada ya kutaka kuanza kushoot video ya Mawazo ndo rumors zilianza, nikawa siamini kwanza.”

Katika jarida hilo ambalo linauzwa kwa shilingi 1,500 tu, Wema amesimulia mengi tangia alipokutana na Diamond, jinsi alivyoumizwa na kitendo chake cha kumrekodi na kusambaza sauti kwenye radio, mapenzi yake na Kanumba, utajiri wake, jinsi anavyowapenda mbwa wake na mambo mengine exclusive.

HII NDIO RIPOTI YA KUTEKWA, KUUMIZWA KIBANDA



TAARIFA YA UCHUGUZI JUU YA KUTEKWA NA KUUMIZWA KWA ABSALOM KIBANDA IMEWASILISHWA NYUMBANI HOTEL - TANGA MEI 30, 2013


UTANGULIZI: 

Usiku wa Jumanne ya Machi 5 kuamkia Machi 6, 2013, Mhariri Mtendaji wa New Habari (2006) Ltd, ambaye pia Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda alivamiwa na kujeruhiwa vibaya akiwa nje ya lango la kuingilia nyumbani kwake Mbezi Juu, Dar es Salaam.Tukio hilo liliishtua na kutikisa taifa kwa kiwango kikubwa si tu katika tasnia ya habari nchini, bali pia jamii kwa ujumla hasa baada ya aina ya utekaji, utesaji na usiri uliotumika katika kufanikisha uhalifu huu kufanana kwa karibu na tukio lilomkuta Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madkatari Tanzania, Dk. Stephen Ulimboka lililotokea karibu miezi tisa kabla ya tukio la Kibanda yaani, usiku wa Juni 26, 2012.Ukiacha matukio hayo, miezi sita kabla ya Kibanda kutekwa na kuteswa Mwandishi Daudi Mwangosi, aliuawa akiwa mikononi mwa vyombo vya dola Septemba 2, 2012 huko Nyololo, Iringa akiwa kazini.Tukio la Kibanda limekuwa na sura ya mwendelezo wa mauaji au utesaji wa wanahabari, hasa ikitiliwa maanani kuwa Mwandishi Issa Ngumba (45) wa Radio Kwizera aliyekuwa anafanyia kazi zake katika Wilaya ya Kakonko, Kigoma, Januari mwaka huu, alipigwa risasi na kuuawa katika mazingira ya kutatanisha.Kama hiyo haitoshi, tukio la kutekwa na kudhuriwa kwa Kibanda limetokea mwezi mmoja tu baada ya Mwandishi wa Gazeti la Tanzania Daima, Shaaban Matutu kupigwa risasi na polisi akiwa nyumbani kwake Dar es Salaam kwa maelezo kuwa kimakosa polisi walidhani Matutu ni jambazi.

BREAKING NEWZZZZZZZ....!!! MATOKEO YA KIDATO CHA NNE HAYA HAPA







HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI MHE. EZEKIAH DIBOGO WENJE (MB) ILIYOSABABISHA BUNGE KUHAIRISHWA LEO

HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI MHE. EZEKIAH DIBOGO WENJE (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA KWA MWAKA WA FEDHA 2013/2014

1.0 UTANGULIZI

Mheshimiwa Spika, katika hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni katika bajeti ya wizara hii mwaka 2012/13, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inayoongozwa na CHADEMA ilibaini mapungufu mengi ya kiutendaji na kiuwajibikaji katika wizara hii, na hivyo kuitaka Serikali kufanya mambo yafuatayo ili kuboresha utendaji na ufanisi:

1. Kuziwezesha balozi zetu nje kwa kuzitengea fedha za kutosha ili ziweze kufanya kazi kwa ufanisi
2. Kutoa idadi ya majengo ya balozi zetu nje (nyumba za mabalozi, nyumba za maafisa wa balozi na ofisi za balozi) kwa mchanganuo wa idadi ya nyumba katika nchi na kama nyumba hizo zina hati miliki au la.
3. Kutoa taarifa ya namna kila ubalozi ulivyotekeleza sera ya Diplomasia ya uchumi kwa kuzingatia kwamba balozi nyingi ziko hoi kifedha kiasi cha kwamba waambata wa kiuchumi wanakosa fedha za kusafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa ajili ya upelelezi wa masuala ya kiuchumi.
4. Kulikarabati jengo la ubalozi wa Tanzania huko Msumbiji lililokuwa limechakaa kwa kutofanyiwa ukarabati tangu 1975 ingawa jengo hilo tulipewa bure na Serikali ya Msumbiji chini ya FRELIMO.

PICHA ZA MWAKILISHI WETU KATIKA BBA ALIVYOJIACHIA BAFUNI NA DILISH.

Dillish na Nando wakioga
Jana (May 29) ilikuwa ni usiku wa tatu katika jumba la big brother Afrika huko Afrika Kusini mengi yanazidi kuonekana na sasa washiriki wengi wanaanza kuonesha side B ya mioyo yao na kujaribu kupata muda wa kuwa romantic na kuonesha upendo (Romantic time). 
 Wakati washiriki wengine wakiendelea na mambo yao mtanzania Ammy Nando alijiachia kwenye bafu moja na na kuoga na mrembo Dillish kutoka na Namibia ambae ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu akisomea Saikolojia.
Huenda huu ukawa mwanzo wa mahusiano yao humo ndani kwa sababu moyo hauna pazia na uruzi wa Dillish unaweza kumvuta to the limit model huyo wa kitanzania.
Dillish
Kwa upande mwingine the boss lady toka Kenya Huddah Monroe alipata nafasi ya kushare na  Denzel mawili matatu hasa kuhusu mahusiano, wakati Denzel akiwa ameonesha tangu mwanzo kudata kwa Huddah. Jana Huddah alifunguka na kumwambia kuwa anahitaji mwanamme mwenye pesa na kwamba she is a gold digger. Lakini second kadhaa baadae akafuta kauli yake na kumwambia kuwa alikuwa anatania. Really?!

Wiki hii Benzel, Betty, Huddah, Selly na Natasha wako katika nafasi kukumbwa na Eviction.

MSANII K-LYN AFUNGUKA KUHUSU BABA WA WATOTO WAKE MAPACHA NI BOSS WA MEDIA KUBWA BONGO

Am just a messenger!

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE YAZIDI KUZUA UTATA

Matokeo ya kidato cha nne yanayotarajiwa kutangazwa leo, yamezidi kuzua mapya baada ya Baraza la Mitihani nchini (Necta) kulazimika kutumia kanuni iliyofanya ufaulu upande kwa asilimia tisa kutoka 34 wa awali, lengo likiwa ni kuepusha watahiniwa waliokuwa wamefaulu mwanzo kufeli.

Kanuni iliyokuwa imetumika mwanzo, ilifanya matokeo hayo yapande kwa asilimia kati ya 20 na 23, kiwango ambacho Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete aliwaeleza wabunge wa chama chake Mei 19, mwaka huu mjini Dodoma.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari kutoka ndani ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, wiki iliyopita maofisa wa wizara na taasisi zake wakiongozwa na Waziri Dk Shukuru Kawambwa, walijadili matokeo hayo.


                       Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Dk Shukuru Kawambwa.
“Wakati yakijadili, ufaulu bado ulikuwa kulekule kwenye zaidi ya asilimia 54, kutokana na kanuni hiyo wanafunzi kama 2,500 waliokuwa wamefaulu kwa madaraja ya juu walikuwa washuke,” kilisema.

Kutokana na hali hiyo, kwa sasa ufaulu ni asilimia 43 jambo linalofanya matokeo hayo yawe chini ikilinganishwa na mwaka 2011.
Chanzo chetu kilieleza kuwa, katika kikao hicho, kulikuwa na mvutano kuhusu kanuni ipi itumike ili kuwaokoa wanafunzi hao alama zao zisishuke.
Baada ya kumalizika kwa kikao hicho, Necta ilienda tena kuyafanyia kazi matokeo hayo ambapo sasa ufaulu umeshuka kwa asilimia zaidi ya 20 hadi kufikia  asilimia tisa.

“Kwa sasa hakuna mtu ambaye matokeo yake yameshuka, ila bwana kazi ipo siyo kama ambavyo watu wanaona kuna vurugu kweli,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:
“Ukijaribu kuangalia, Necta wanasimamia kanuni, lakini wakati mwingine inabidi mtu uangalie hali ilivyo, kwa sasa watu wanaangalia zaidi mwitikio wa wananchi utakavyokuwa haya matokeo yakitangazwa badala ya kuangalia vitu vya msingi,” kilisema chanzo hicho.

Producer Mswaki Aimba kama Ngwear Kumuenzi-Sikiliza Wimbo Huo Hapa...!!

Huu Wimbo Ameimba Producer wa mziki anayejulikana kwa jina la Mswaki Kutoka Studio ya Black Curtains....Ameimba kama Marehemu Ngwear Akiimba baada ya Kifo chake...Sikiliza Hapa chini: Big up Sana Mswaki 

>>>>>  Click Hapa

ANGALIA WALICHOCHAT WEMA SEPETU NA NGWAIR SIKU CHACHE KABLA YA KIFO, NI KUUSU KAJALA KUONEKANA KATIKA VIDEO MPYA YA MAREHEMU NGWAIR

 
Katika upekuzi wetu leo hii tuliweza kupata moja ya chat za mwisho mwisho ya marehemu Albert Mangwea akiwa afrika ya kusini na mwanadada wa bongo movies Wema sepetu. Katika maongezi hayo Ngwea alikuwa anapanga Kumtumia mwadadada mwingine wa bongo movies Kajala Masanja kwenye video yake mpya aliyokuwa anajiandaa kuifanya. Maongezi yao yalikuwa hivi.

Mangwea : kuku bandani..
Mangwea : Nataka Kajala…
Mangwea : Sikiza nyimbo then utanipa idea..
Mangwea : Nataka tukipiga hela kwa bro…
Mangwea : Tulipe na hela ya ticket ya Jux aje toka China tumalize huku kusini
Mangwea : #hugs
Wema Sepetu : Upo api?
Mangwea: Me nipo Pretoria now momo…
(Angalia screen shot ya maongezi hayo pichani)
Dah, inasikitisha sana. Maisha ya Msanii huyu yaliyokatika mapema. Mungu ailaze roho marehemu mahali pema peponi.

TCRA.... "SIMU ZISIZOSAJILIWA MWISHO KESHO"

TCRA: Simu Zisizosajiliwa Mwisho KeshokutwaMamlaka ya Mawasilino Tanzania, TCRA, imesema watumiaji wa simu ambazo hazikusajiliwa, watakatiwa mawasiliano ifikapo Juni Mosi mwaka huu.
Tamko hilo lilitolewa jijiji Mbeya na Mkurugenzi wa Sheria na Leseni wa mamlaka hiyo, Elizabeth Nziga wakati wa semina kuhusu utekelezaji wa sheria mpya ya mawasiliano ya elektroniki na posta ya mwaka 2010 kwa wadau mbalimbali.
Hiyo ni awamu nyingine katika mipango ya TCRA, kwani awali ilikuwa na kampeni za kuzima mitambo ya analogia nchi nzima na kuwataka wananchi kuingia katika mfumo wa dijitali ulioanzia katika Mkoa wa Dar es Salaam Desemba 31, mwaka jana.
Mikoa mingine iliyoingia kwenye mfumo wa dijitali ni Arusha, Tanga, Dodoma, Mbeya na Mwanza. Nziga alisema mamlaka hiyo inasisitiza kuwa hatua hiyo ni utekelezaji wa makubaliano kati yake na watoa huduma za mawasilino ya simu na kufikia usiku wa Juni Mosi, namba za simu ambazo hazikusajiliwa zitakoma. Mmiliki wake hataweza kuitumia kupiga wala kupokea siku.
Alisema kuwa ni muda mrefu umepita ambao ulitolewa kwa ajili ya kusajili namba za simu lakini watu wengi hawakuweza kufanya hivyo kwa wakati na badala yake wamekuwa wakitumia simu vibaya ikiwa ni pamoja na kufanya uhalifu na kutoa lugha chafu.
Katika hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,
Abbas Kandoro, ilisema vyombo vya mawasiliano vimesaidia kukua kwa sekta mbalimbali

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MEI 30, 2013


3 a8154


1 847ab

Wednesday, May 29, 2013

Justin Bieber matatani tena,majirani wamtuhumu kuvuta bangi mbele ya watoto na kupiga kelele ovyo usiku wa manane


Siku chache baada ya kuondoa stress za mahusiano ya mapenzi juu ya Selena Gomez ‘The Beauty and beat singer’ Justin Bieber amekumbana na matatizo mengine ambayo yanaweza kuwa makubwa zaidi ya stress alizokuwa nazo, baada ya kuwa kero kwa majirani zake ambao wanajuta kukaa karibu na staa huyo kwa kuwa tabia zake zimeuharibu utulivu uliokuwepo katika ujirani huo huko Los Angeles.

Majirani hao wameiambia TMZ kuwa Bieber na marafiki zake wamekuwa wakisababisha kelele nyingi usiku wa manane wanaporudi kutoka viwanja na kuendesha gari lake aina ya Ferrari kwa fujo na wakati mwingine pikipiki yake, lakini pia hata wakifikika nyumbani huendeleza party huku wakiachia sauti juu na kuwanyima usingizi majirani hao.

Majirani hao walisema mida ya mchana Bieber hupita na gari lake taratibu mbele ya watoto wadogo huku akivuta marijuana a.k.a bangi waziwazi, na kwamba siku moja mwimbaji huyo alikuwa anaendesha akiwa na rafiki yake ambae pia alikuwa anavuta bangi.

Walisema hata bodi ya mmiliki wa nyumba hizo imewaambia majirani hao kuwa amepanga kuripoti polisi suala hilo kwa kuwa ni swala la kiharifu na linalovunja haki za msingi za majirani hao. Majirani hao pia wamesharipoti polisi tayari na polisi wamepanga kuzuia uendeshaji magari mida ya usiku sana katika maeneo hayo ili kuondoa kero hizo.

Mkasa huu uliompata wa kuchukiwa na majirani zake unaweza kufanana kidogo na ule wa Chris Brown kushtakiwa na majirani zake kwa kuwa alichora michoro iliyosemekana kuwatishia watoto wao. Lakini hii ya Bieber kuvuta marijuana mbele ya watoto wao itakuwa imetisha zaidi.

DAKTARI ATHIBITISHA KUWA MANGWEA KAFARIKI KWA KUJIOVERDOSE HEROIN NA CRACK

 
 
The Medical report from Helen Joseph hospital,Dr Shirley Radcliffe  confirming that albert Mangwairdied from “alcohol toxicity” after drinking toomuch,Over-exhaustion and drugs overdose....The inquest heard that Albert 28, collapsed in the his friends home had been more thanfive-times the legal S.A drink-drive limit with 416mgof alcohol per 100 millilitres of blood in hissystem....
Radcliffe described thereasons for ICU admission included hypoxemia and one of his friend found “two empty vodka bottles[found] on the Car” and he hadbeen suffering from the eating disorder Bulimiafor several months before his death and endless partying session with little or no resting...sample taken from his stomach showed poly-drug cocktail and he overdosed Heroin,Cocaine 'crack' and cannabis 0.08gms was also found in his blood...and his death was caused by massive heart attack and respiratory failure followed by sudden Heart stop...and end up dead within seconds! R.I.P Mangwear!

HISTORIA YA MAREHEMU NGWAIR ALIYOISEMA MWENYEWE KWENYE INTERVIEW YAKE YA MWISHO

 
JINA LAKE HALISI NI ALBERT KENETH MANGWAIR,NI MTU WA RUVUMA MNGONI...,,,,MNGONI,LAKINI ALIZALIWA MBEYA TAREHE 16 NOVEMBER,MWAKA 1982.YEYE NI MTOTO WA MWISHO KWAO,KWA BABA AKIWA MTOTO WA 10,KWA MAMA AKIWA MTOTO WA 6.
NGWAIR ASILI YAKE NI RUVUMA,YAANI MNGONI, ALIZALIWA MBEYA,A KIWA MIAKA 5 WALIHAMIA MOROGORO AKASOMA SHULE YA MSINGI BUNGO HADI DARASA LA 5,BABA YAKE AKAPATA UHAMISHO AKAHAMIA DODOMA,SO AKAHAMA NA BABA YAKE AKAENDA AKAMALIZA SHULE YA MSINGI MLIMWA DODOMA.BAAADAE MAZENGO SEC,THEN CHUO CHA UFUNDI MAZENGO

WIMBO WA CHID BENZ UNAITWA R.I.P NGWAIR. USIKILIZE NA KUDOWNLOAD



Click hapa>>>>>>       Chid Benz - Albert Mangwea

(News) Staki kusikia nyimbo zote za marehemu ALBERT MANGWEAR alizorekodi BONGO REC zikipigwa CLOUDS FM kuanzia sasa.

 Muda mfupi uliopita nilipokea simu kutoka kwa Producer mkongwe hapa bongo anajulikana kwa jina la P Funk Majani na kuniomba nipokee msg hii hapa chini na kuwaomba watanzania walijue hili na baadae atatoa barua rasmi.

TAARIFA YA KIFAMILIA KUHUSU MAZISHI YA NGWEA NA JINSI MWILI HUO UTAKAVYOLETWA TANZANIA

 
Baba Mdogo wa Marehemu Mzee Mangweha ambaye yuko Mbinga Songea kikazi, amesema kuwa wamekubaliana na kaka yake mkubwa yaani baba mkubwa wa Ngwair, David Mangweha ambaye naye yuko Songea kuwa watu watakutanika Mbezi kwa msiba na pia mapokezi yatafanyika hapa Dar es salaam Mbezi Beach. 
Ingawa bado kikao cha familia nzima hakijafanyika lakini baba huyo mdogo amesema wanaweza kulazimika kuzika Morogoro sehemu ambayo baba yake alizikwa.
Baba huyo mdogo alisema kuwa kesho ndo watarudi Dar es Salaam pamoja na kaka yake yaani baba mkubwa wa marehemu. 

Kuhusu mwili kuletwa hapa Tanzania kutoka Afrika Kusini baba mdogo amesema kuwa mpaka sasa hawajajua jinsi gani mwili huo utafika hapa lakini kuna ndugu zao ambao tayari washaanza kufanya taratibu za kuwasiliana na ubalozi wa Afrika Kusini ili kujua ni jinsi gani mwili huo utafika hapa.

Kama kutakuwa na mabadiliko yeyote watakapowasili kesho baba mdogo na baba mkubwa baada ya kikao cha familia watatoa taarifa.

MAAJABU AGNESS JERALD ‘MASOGANGE’ ANASUMBULIWA NA TATIZO LA KUOTA NDOTO MBAYA USIKU NA KUAMKA KISHA KUTOKA NJE NA KUTIMUA MBIO.


VIDEO Queen wa Bongo Fleva, Agness Jerald ‘Masogange’ anasumbuliwa na tatizo la kuota ndoto mbaya usiku na kuamka kisha kutoka nje na kutimua mbio, jambo ambalo kwa wengi linaweza kuonekana kuwa ni maajabu.
 
                                                        Agness Jerald ‘Masogange’.
Habari kutoka kwa sosi wetu, zinasema kuwa katikati ya wiki iliyopita, Masogange akiwa ndotoni, aliamka na kufungua milango na geti la nje kisha kutimua mbio umbali mrefu akiwa na nguo za kulalia na miguuni hana  viatu.

“Bahati nzuri ni kwamba, wakati anahangaika kufungua geti, rafiki yake aliyekuwa amelala naye alishtuka na kushangaa kukuta milango iko wazi. Alipotoka nje, akakuta Masogange ndiyo anamalizia kufungua geti kubwa na kuanza kukimbia hivyo akamkimbiza,” kilieleza chanzo chetu.
Akaongeza: “Lakini pia aliwapigia simu marafiki zake wengine na kuwajulisha juu ya tukio hilo, maana mwenyewe ilikuwa mara ya kwanza kumuona katika hali hiyo.”

MASOGANGE ANASEMAJE?
Risasi Mchanganyiko kama ilivyo kawaida yake ya kutokukurupuka, lilimsaka Masogange kwa simu na kufanikiwa ambapo alithibitisha tukio hilo na kufafanua kwamba liliwahi kumtesa kwa muda mrefu huko nyuma, likaisha.

“Ilikuwa hatari sana lakini namshukuru rafiki yangu kwa kunisaidia. Unajua hili tatizo liliwahi kunitesa sana wakati nikiwa mdogo lakini nilikwenda Mbeya nikapewa dawa tatizo likapotea kabisa hadi juzi liliporudi tena,” alisema.
Habari na Global Publishers.

NGWAIR ALIKUA MUUMINI MZURI, NA MASAA MACHACHE KABLA YA KIFO ALIANDIKA MSTARI HUU KUTOKA KATIKA BIBLIA


MAGAZETI YA LEO JUMATANO MEI 29, 2013

7 02703  1 45fee

SIKILIZA NA DOWNLOAD NYIMBO YA MAOMBOLEZO KWAAJILI YA KIPENZI CHETU ALBERT MANGWEA...R.I.P BROTHER

SONG - R.I.P BROTHER NGWEA
ARTIST - MOZEH THOMAS & MIRROR RHYMES
OVERCLASSIC MUSIC/ EIZER
 SIKILIZA HAPO CHINI...

Click hapa >>>>>         R.I.P NGWEA

 

KAULI YA MAMA MZAZI WA NGWEA..... "MWANANGU ALINIAHIDI KUWA ATARUDI IJUMAA ILIYOPITA"

Marehemu Albert Mangwair enzi za uhai wake.

Akiongea kupitia kipindi cha Amplifire cha Clouds FM, kutoka mkoani Morogoro, mama mzazi wa msanii Albert Mangwair aliyefariki dunia leo akiwa nchini Afrika Kusini, amesema kuwa mara ya mwisho kuwasiliana na marehemu ilikuwa wiki mbili zilizopita ambapo Mangwair alimwambia kuwa mzima na anaendelea vizuri na kwamba angerejea nchini Ijumaa iliyopita. Aliongeza kuwa taarifa za kifo cha mwanaye amezipata jioni hii kwa masikitiko. Wakati Mangwair anaelekea Afrika Kusini hakumuaga mama yake japo akiwa huko alikuwa anawasiliana naye. Kuhusu taarifa za mazishi mama Mangwair amesema bado anasubiri shemeji zake wafike ili wapange. Mungu ampumzishe Mangwair mahali pema peponi. Amen!

MWANA FA NA KALAPINA WAAHIRISHA SHOW ZAO ZA MWISHO WA WIKI KUTOKANA NA KIFO CHA MSANII MANGWEA...

Kutokana na habari za kufariki kwa mwanamuziki Albert Mangwair, msanii ambaye ni mmoja kati ya wana Hip Hop maarufu nchini, Mwanamuziki mwingine pia wa Hip Hop Hamis Mwin'jumah, a.k.a MwanaFA(Pichani)nametangaza kuahirisha show yake ya The Finest iliyokuwa ifanyike Ijumaa hii May 31, 2013.

 
MwanaFA ameiambia Mdimuz Blog kwamba kuguswa kwake na taarifa hizi kumesababisha ajisikie kuomboleza kwanza, kabla maisha mengine hayajaendelea, kwa hiyo amewaomba radhi mashabiki, hasa wale waliokuwa wameshanunua tiketi, na kuwaomba wawe na subira, tarehe y

SIRI YA MAFANIKIO YA MUONEKANO MPYA WA VICENT KIGOSI

Kwa Kipindi kirefu amekuwa akionekana kuwa mwenye mwili nadhifu na
mengine yakizushwa
kwa kila aina ya usemi....Lakini Blog yako ya This is Diamond imeweza
Kujua Lililo nyuma ya pazia...
The Prezdah wa Bongo Movie Vicent Kigosi almaarfu kama
Ray the Greatest, ameamua kueka kando mambo yote ya starehe
na hivi sasa yuko gym kutengeneza
 mwili wake na Afya kwa ujumla ili kulitumikia vyema Taifa lake la
 Tanzania kupitia tasnia ya Film..

Zifuatazo ni Picha kadhaa tu Star Huyo wa BongoMovie akiwa
Gym akitengeneza mwili kiujumla...


Hakika Ray the Greatest  Huu ni mfano wa kuigwa kwa wewe
 mwananchi kwa kufanya mazoezi
kutengeneza afya yako kwa ujumla......

This is Diamond inakutakia Baraka tele na Amani katika kazi
 yako ya sanaa na mipango
Lukuki kwenye jamii....

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...