Tuesday, December 24, 2013

SOMA TAARIFA KUHUSU BEI MPYA ZA UMEME ZITAKAZOANZA KUTUMIKA TAREHE 1 JANUARI 2014

tanesco
Tarehe 11 Oktoba 2013, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) liliwasilisha maombi ya kurekebisha bei ya umeme kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA). TANESCO ilipendekeza kuongeza bei kwa asilimia 67.87 kuanzia tarehe 1 Oktoba 2013, asilimia 12.74 kuanzia tarehe 1 Januari 2014 na asilimia 9.17 kuanzia tarehe 1 Januari 2015.
Vilevile TANESCO waliomba kuidhinishwa kwa kanuni ya kurekebisha bei ya umeme kulingana na mabadiliko ya bei za mafuta, mfumuko wa bei na mabadiliko ya thamani ya shilingi ya kitanzania. Aidha, TANESCO iliomba kuidhinishwa viwango vya gharama za kuunganisha umeme vinavyozingatia ruzuku inaliyotolewa na Serikali, na kuidhinishwa tozo mbalimbali kwa huduma zitolewazo na TANESCO.
Kwa mujibu wa TANESCO, kupitishwa kwa maombi haya kutaliwezesha Shirika (a) kupata fedha za uendeshaji na uwekezaji wa miundombinu, (b) kulifanya Shirika liweze kukopesheka na hivyo kuwezesha kupata mikopo yenye masharti nafuu, (c) kuliwezesha Shirika kukabiliana na ongezeko la mahitaji ya umeme kwenye Gridi ya Taifa, na (d) kuongeza uwezo wa
kufanya matengenezo ya mara kwa mara ya miundombinu iliyopo ili kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa huduma za umeme wa uhakika kwa wateja.


Itakumbukwa kwamba bei za umeme zinazotumika hivi sasa ziliidhinishwa mwezi Januari 2012. Bei hizo zilipanda kwa asilimia 40.29 ikilinganishwa na maombi ya TANESCO ambapo ilipendekeza bei zipande kwa wastani wa asilimia 155. Sababu ilikuwa ni kuongezeka kwa gharama za uendeshaji kulikosababishwa na hali ya ukame katika maeneo yanayotiririsha maji katika mabwawa ya kuzalishia umeme, toka mwaka 2011. 
Hali hiyo ilipelekea TANESCO kulazimika kununua umeme kwa gharama kutoka kwa wazalishaji wa dharura (Emergency Power Producers). Hali ya maji katika mabwawa ya kuzalishia umeme bado sio nzuri na hivyo TANESCO itaendelea kununua umeme kutoka kwa wazalishaji wa dharura (Emergency Power Producers).

HII HAPA TAARIFA RASMI YA KUFUKUZWA KOCHA WA YANGA ERNST BRANDTS


Uongozi wa klabu ya Young Africans SC umempatia taarifa (Notice) ya siku ya thelathini (30) kocha mkuu mholanzi Ernie Brandts juu ya kusitisha mkataba wake kuanzia jana Disemba 22 mwaka huu.
Maamuzi hayo yanafuatia muenendo wa matokeo mabaya katika michezo iliyopita ya Ligi Kuu, kirafiki na bonanza la Nani Mtani Jembe dhidi ya Simba SC mwishoni mwa wiki.
Hatua ya Young Africans SC kusitisha huduma na Brandts isichukuliwe kama chuki bali ni moja ya sehemu ya kuhakikisha tunaboresha benchi la ufundi ili tuweze kupata matokeo mazuri katika Mashindano yanayotukabili.
Ukitazama uwezo wa mchezaji mmoja mmoja wa Yanga SC na wapinzani wetu, na soka tulilocheza kwenye mchezo wa mwishoni mwa wiki kwa kweli ni dhahiri mwalimu amefikia mwisho kimbinu na hana njia mbadala.
Young Africans SC imekua ikicheza chini ya kiwango katika michezo ya Ligi Kuu hali iliyoplekea kupata ushindi kwa tabu na wakati mwingine timu kupoteza pointi.
Kufuatia kupewa taarifa ya siku 30, Brandts ataamua mwenyewe kama ataendelea kusimamia mazoezi ya timu au kuondoka moja kwa moja kabla ya muda huo ukiwa haujakamilika.

WANAMUZIKI WA KUNDI LA PUSSY RIOT WAACHIWA HURU

Wanamuziki wote wa kundi la muziki wa Punk la Pussy Riot la nchini Russia wameachiliwa huru kutoka gerezani chini ya sheria ya msamaha.
Nadezhda Tolokonnikova aliachiwa huru kutoka hospitali moja ya gereza lililopo Siberia, wakati mwenzake Maria Alyokhina aliachiliwa huru Jumatatu huko Nizhny Novgorod.
Wote wameuita msamaha huo kuwa ni sawa na sarakasi za serikali za kujisafisha kabla ya kufanyika kwa michezo ya olimpiki ya majira ya joto itakayofanyika Russia Februari mwakani.
Wanawake hao wanamuziki walifungwa Agosti 2012 baada ya kuimba nyimbo inayokejeli katika kanisa kuu jijini Moscow.
Kitendo chao kilitafsiriwa kama kumkufuru mungu na wananchi wengi wa Russia lakini kutiwa kwao hatiani kwa kosa la utukutu ukichochewa na chuki dhidi ya dini ulishutumiwa na vikundi vya kutetea haki za binadamu, wanaharakati wanaompinga Rais Vladmir Putin na mataifa ya nje.
Watu wengi wanaotumikia vifungo wanauona msamaha huo kama jaribio la Rais Putin la kusafisha taswira yake katika nchi za magharibi na kuiboresha rekodi yake ya haki za binadamu kabla ya kufanyika kwa michezo ya Olimpiki huko Sochi Februari 2014.
Siku mbili baada ya sheria hiyo ya msamaha kuanza kutumika, Rais Putin alimsamehe Mikhail Khodorkovsky, ambaye siku za nyuma alikuwa ni mtu anayeongoza kwa utajiri nchini Russia na mkosoaji binafsi wa sera za serikali, hatua ambayo pia ilitafsiriwa kama kuyaridhisha mataifa ya magharibi.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE DESEMBA 24, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.

MSIMAMO WA LIGI KUU YA UINGEREZA

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...