Friday, July 05, 2013

MAHAKAMA YAELEKEZA MAZISHI YA MANDELA, YAAMURU MIILI YA WANAWE IFUKULIWE IKAZIKWE ATAKAPOZIKWA




Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela


HATIMAYE vita iliyokuwa ikipiganwa ndani ya familia ya Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, kuhusu mahali panapostahili kuwa eneo la kuzikia miili ya wanafamilia hiyo imefikia mwisho, baada ya Mahakama Kuu ya Mthatha iliyoko Jimbo la Eastern Cape, kutoa hukumu inayoelekeza yawe katika makazi ya Mandela yaliyoko kijijini Qunu.



Hukumu hiyo ilitolewa juzi na Jaji Lusindiso Pakade wa Mahakama Kuu ya Eastern Cape, aliyekuwa akisikiliza shauri lililofunguliwa mahakamani hapo na mtoto mkubwa wa kike wa Mandela, Makaziwe, aliyekuwa akipinga hatua ya Mandla ambaye alichukua uamuzi wa kufukua miili ya watoto watatu wa Mandela akiwamo baba yake mzazi, kutoka katika makaburi ya familia yaliyoko Qunu na kwenda kuizika katika makazi yake ya kichifu yaliyoko Mzove.



Jaji Pakade katika hukumu yake ya juzi, alikiita kitendo cha Mandla kufukua miili hiyo kutoka kaburini na kwenda kuizika upya bila ridhaa ya wanafamilia, kuwa hakikubaliki hivyo miili hiyo ifukuliwe na kurudishwa ilipozikwa awali.

UHUSUIANO WA IRAN NA ZIMBABWE WAPONGEZWA

 
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Ali Akbar Salehi amekutana na Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe mjini Harare ambapo wamefanya mazungumzo kuhusu njia za kustawisha uhusiano wa pande mbili. Katika mkutano huo, Salehi amemkabidhi Mugabe salamu za Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Iran na rais-mteule Hassan Rohani. Kwa upande wake Rais Mugabe ameashiria safari zake nchini Iran na kusema Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu pia aliwahi kutembelea Zimbabwe wakati akiwa rais. Mapema Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran alikutana na kufanya mazungumzo na mwenzake wa Zimbabwe Simbarashe Mumbengegwi ampabo wawili hao wamepongeza uhusiano baina ya nchi zao.
  Katika mkutano huo Salehi alisema Iran na Zimbabwe ziko katika mashinikizo na vikwazo haramu na hivyo nchi hizi mbili zinapaswa kuwa na ubunifu katika kukabiliana na mzingoro wa maadui. Naye Mumbengegwi alisema Iran, kama mwenyekiti wa mzunguko wa Harakati ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote NAM imeinua itibari ya harakati hiyo. Aidha amepongeza misimamo imara ya Iran na Zimbabwe pamoja na kuwepo mashinikizo ya kila aina dhidi yao.

RAIS WA MPITO AAPISHWA NCHINI MISRI

 
Sherehe zilijaa kote Misri baada ya Morsi kuondolewa mamlakani
Jaji mkuu wa mahakama ya juu zaidi ya kikatiba ameapishwa nchini Misri kuwa rais wa muda baada ya jeshi kumng'oa mamlakani rais aliyechaguliwa na raia kwa njia ya kidemokrasia na kushinda kwa wingi wa kura, Mohammed Morsi.
Viongozi duniani wamepokea kwa tahadhari matukio yanayojiri huko Misri. Waziri wa mashauri ya kigeni wa Ujerumani, Guido Westerwelle, amewaambia waandishi kwamba anaangalia kwa umakini hatua iliyochukuliwa na jeshi la Misri.
Waziri wa mashauri ya kigeni wa Uingereza , William Hague, amesema Uingereza haiungi mkono uvamizi huo wa kijeshi lakini haina budi kuitambua hatua hiyo na kusogea mbele. Hata hivyo alikataa kulishutumu jeshi kwa kumpindua Morsi akisema ni uvamizi ulioungwa mkono na watu wengi.
Mfalme Abdalla wa Saudia ametuma ujumbe wa hongera kwa kaimu rais wa Misri akisema kwamba uteuzi wake unajiri katika wakati muhimu.
Mkuu wa jeshi Generali Abdul Fattah al-Sisi alitoa tangaza hilo kupitia televisheini Jumatano jioni, katika kile Morsi, alisema ni mapinduzi ya kijeshi.
Generali Sisi alisema kuwa Morsi,ambaye ni rais wa kwanza kuchaguliwa amekosa kutimiza mahitaji ya watu.
 
Ishara ya mapenzi iliyochorwa angani kwa kutumia ndege za kijeshi kuwataka wananchi kupatana
Hatua hiyo inakuja baada ya siku nyingi ya maandamano, dhidi ya rais Morsi wa chama cha Musolim Brotherhood.
Waandamanaji walimtuhumu yeye na chama chake kwa kusukuma ajenda ya kiisilamu kwa taifa hilo na kukosa kusuluhisha matatizo ya kiuchumi yanayokumba taifa hilo.
Chama cha Muslim Brotherhood kimesema kuwa bwana Morsi pamoja na washauri wake wako chini ya kifungo cha nyumbani na hawana mawasiliano ya nje.
Hapo awali mkuu wa majeshi alisema kuwa katiba ya nchi hiyo imeahirishwa na kwamba jaji mkuu wa taifa hilo atachukuwa mamlaka ya rais.
Maelfu ya waandamanaji wanaompinga bwana Morsi mjini Cairo walisherehekea kwa shangwe na vifijo kufuatia taarifa hiyo ya jeshi lakini wale wanaomuunga bwana Morsi wanasemekana kubaki kimya huku wakisubiri matukio yatakayofwata.
Rais Obama amesema kuwa ana wasiwasi mkubwa kuhusiana na matukio yaliyopo nchini Misri huku katibu mkuu wa umoja wa mataifa Banki Moon akitaka kuwe na utulivu.

RCC MBEYA YAPENDEKEZA WILAYA YA CHUNYA KUWA MAKAO MAKUU YA MKOA MPYA WA SONGWE


   
Mbunge wa Jimbo la Songwe mkoani Mbeya ambaye pia ni Naibu Waziri Elimu na Mafunzo ya Ufundi Philip Mulugo akifurahia jambo.
Na Gordon Kalulunga
WILAYA ya Chunya mkoani Mbeya ambayo kwa sasa imepitishwa na kikao maalum cha kamati ya ushauri ya mkoa(RCC) kuwa iwe makao makuu ya mkoa mpya wa Songwe, ina historia ndefu na inastahili kuwa makao makuu ya mkoa. Historia inaonesha kuwa wilaya hiyo ndiyo wilaya kubwa kuliko zote nchini Tanzania.
Wilaya hiyo ina kilomita za mraba zipatazo 29,219 tarafa 4, kata 30 vijiji 73 na idadi ndogo ya watu wapatao 290,478.
Chunya ilianzishwa kwenye miaka ya 1948 na wakati huo ikiwa kama makao makuu ya wilaya ya Mbeya.

Wilaya hiyo ni moja kati ya wilaya za zamani au za mwanzo na zenye historia kubwa na ya pekee nchini.
 
Upekee wake unaazia kuwa ni wilaya ambayo imesahaulika kimaendeleo.
Enzi za ukoloni wakati nchi ikijulikana kwa jina la Tanganyika, waingereza walichagua wilaya ya Chunya kuwa makao makuu ya jeshi la polisi katika eneo la mgodi wa Saza(mine).
George Chanda anasema kuwa, sababu kubwa ya kuchagua eneo la mgodi wa Saza au Saza Mine kuwa makao makuu ya polisi katika koloni la Tanganyika ni kilinda maslahi ya dhahabu.
 

MAGAZETI YA LEO TAREHE JULAI 05, 2013




Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...