Saturday, May 24, 2014

MBUNGE NA BIBI HARUSI MTARAJIWA VICY KAMATA AUGUA GHAFLA SAA 36 KABLA YA HARUSI...!!!

Mbunge Vicky Kamata akiwa amelazwa Hospitali ya Tabata General, Dar es Salaam jana. Picha na Florence Majani 

Dodoma/Dar es Salaam. Ni matukio nadra kutokea katika maisha, lakini haya ndiyo yaliyomkuta Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Vicky Kamata, baada ya kuugua ghafla saa 36 kabla ya harusi yake.
Kuugua kwa bibi harusi huyo mtarajiwa, kumezua gumzo katika Viwanja vya Bunge mjini Dodoma na maeneo mengine nchini, kutokana na kile kilichoelezwa kwamba harusi hiyo ilipangwa kuwa ya kifahari ikitarajiwa kutumia Sh96 milioni.
Kamata ilikuwa afunge ndoa leo katika Kanisa Katoliki Parokia ya Bikira Maria Mama wa Mkombozi, Sinza Dar es Salaam na tayari kadi za mialiko zilishasambazwa kwa watu mbalimbali wakiwamo wabunge.
Habari za kuugua ghafla kwa mbunge huyo ambaye pia ni msanii wa muziki aliyetamba na kibao chake cha ‘Wanawake na Maendeleo’ zilianza kuzagaa kwa kasi juzi jioni nchini. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

LIGI YA MABINGWA: SAMATA, ULIMWENGU KUIONGOZA TP MAZEMBE DHIDI YA MAHASIMU WAO AS VITA MJINI LUBUMBASHI


1
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
WASHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samata na Thomas Emmanuel Ulimwengu kesho jumapili wanatarajia kuiongoza TP Mazembe katika mchezo wa hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya wapinzani wao wakubwa, AS Vita mjini Lubumbashi.
Timu hizi hasimu zitakutana katika mchezo wa kesho zikiwa na kumbukumbu ya kusababisha maafa ya vifo vya watu zaidi ya 15 katika mchezo wao wa ligi kuu ya DR Congo wiki za karibuni.
Tukio hilo baya lilitokea mjini Kinshasa baada ya mashabiki wa AS Vita kutoridhishwa na kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa wapinzania wao TP Mazembe.
Mchezo wa kesho umevuta hisia za mashabiki wengi wa soka, kwani timu hizi zinapokutana, upinzani unakuwabmkubwa mno nje ya uwanja na ndani ya uwanja.
TP Mazembe wataingia katika mchezo wa kesho wakiwa na kumbukumbu mbaya ya kupigwa bao 1-0 kwenye mchezo wao wa kwanza wa kundi A na Al Hilal ya Sudan mnao mei 17 mwaka huu.
Mei 18 mwaka huu, AS Vita walitumia vyema uwanja wao wa nyumbani baada ya kuilaza Zamalek ya Misri mabao 2-1, hivyo wataingia katika mchezo huo wa kundi A wakiwa na morali kubwa ya kusaka ushindi wa pili.
Mechi nyingine ya kesho jumapili itakuwa ya Kundi B kati ya wenyeji ES Setif ya Algeria dhidi ya SC Sfaxine ya Tunia.
Mei 18 mwaka huu SC Sfaxine waliifumua Al Ahly Benghazi ya Libya mabao 3-1, wakati mei 17, 2014, ES Setif waliifunga mabao 2-1 Esperance ya Tunisia.
Mbali na mechi hizo za kesho, leo hii mitanange mingine inaendelea ambapo kundi A, wenyeji Zamalek watawakaribisha Al Hilal kutoka nchini Sudan.
Huu utakuwa mchezo muhimu kwa Mafarao waliopoteza mechi iliyopita. Al Hilal wao watakuwa wanahitaji ushindi wa pili katika michuano hiyo.
Mechi ya kundi B leo hii, wenyeji Al Ahly Benghazi ya Libya waliopoteza mechi ya kwanza kwa mabao 3-1 watakabiliana na miamba ya soka la Tunisia, Esperance ambao nao mechi ya kwanza walilala kwa mabao 2-1. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

CECAFA NILE BASIN CUP, MBEYA CITY FC KUTUPA KARATA YAO YA KWANZA LEO

IMG_1150 
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano mipya ya CECAFA Nile Basin Cup inayoendelea nchini Sudan , Mbeya City fc wanaanza kutupa karata yao ya kwanza leo hii majira ya 11:30 jioni kwa saa za Sudan dhidi ya Academie Tchite ya Burundi. Kuelekea katika mechi hii itakayopigwa uwanja wa Al-Merreikh mjini Khartoum, ushinidi ni muhimu kwa Mbeya City fc ili kupata morali ya mashindano haya yaliyoanza jana kwa mechi tatu kupigwa viwanja viwili tofauti. Kocha Juma Mwabusi ameuambia mtandao huu kwa njia ya simu kutoka nchini Sudan kuwa kikosi chake kipo salama na kipo tayari kwa ajili ya mechi ya leo jioni. “Tumewasili salama mjini Khartoum. Tulichelewa kufika huku ili angalau kuzoa hali ya hewa. Lakini haimaanishi hatuwezi kushindana. Sisi tumejiandaa vizuri na tulikaa Dar kwenye joto ingawa hailingani na Sudan”. “Mashabiki wetu wawe na imani na timu yao. Tunaiwakilisha nchi na tutapambana kwa nguvu zote. Wachezaji wana morali ya kufanya vizuri”. Alisema Mwambusi. Mbali na mchezo huo wa jioni, mechi nyingine ya usiku itakuwa baina ya AFC Leopard ya Kenya dhidi ya Enticelles ya Rwanda. Katika mechi zilizopigwa jana, kwa mujibu wa msemaji wa CECAFA Rodgers Mulindwa, Victoria University ya Kenya iliilaza Malakia FC ya Sudan kusini bao 1-0. Wenyeji Al-Merreikh waliibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Polisi ya visiwani Zanzibar. Nao Al-Shandi waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Dkhill ya Djibouti. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

CCM: "HATUWEZI KUWAVUMILIA WATENDAJI WA SERIKALI WANAOKWAMISHA UTEKELEZWAJI WA ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI"

Katibu wa CCM wilaya ya kilolo Bw. Raphel Mahumba mwenye pama, akimuagiza Diwani wa kata ya ukumbi afuatilie nani anaye kwamisha ujenzi wa zahanati ya kitowo na hatua zichukuliwe haraka, aliye vaa skafu ni katibu mwenezi wa chama.
Wananchi waliongozana na katibu wa CCm wilaya ya Kilolo kuangalia ujenzi wa zahanati ya Kotowo ambayo imesimama bila sababu za msingi. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

ZIJUE KANUNI ZA SAYANSI ZA KUSAIDIA MTU KUISHI MAISHA MAREFU


Nyama nyekundu inaelezwa kuwa ni moja ya vyakula vinavyopunguza urefu wa maisha. 

Na Clifford Majani, Mwananchi


Kwa miaka mingi sana binadamu wa karne zote wamekuwa wakitafuta siri za maisha marefu, kuzuia uzee na hata kuzuia kifo. Lakini pamoja na jitihada nyingi mambo haya yameendelea kuwa changamoto kubwa kwenye maisha ya mwanadamu katika nchi mbalimbali duniani.  Kwa Tanzania, inakadiriwa kuwa umri wa kuishi kwa wanaume ni takriban miaka 58.2 na kwa wanawake ni miaka 60.5.
Muda huu wa kuishi ni mfupi sana ikilinganishwa na wenzetu katika nchi zilizoendelea kama vile Marekani ambako wastani wa kuishi ni unakadiriwa kuwa ni miaka 78.2. Wanasayansi wamekuwa na nadharia nyingi kuhusu sababu zinazosababisha binadamu azeeke na kufa mapema. Ila wengi hufikiri kuwa tunazeeka mapema kutokana na sababu za maumbile na vinasaba tunavyorithi kwa wazazi wetu.
Wengine husema kuwa tunazeeka haraka kutokana na kuwa na mtindo usiofaa wa maisha. Mtaalamu wa Afya, Dk Mark Stibich  anasema kwamba kuzeeka haraka na kuishi maishi mafupi ni suala mtambuka na linahusisha mambo kama vile vinasaba, kemia, fiziolojia ya mwili pamoja na tabia zetu kwa mujibu wa makala yake ya Mei 10, 2014 liyowekwa kwenye tovuti ya longevity.about.com.
Mtaalamu wa maabara nchini Ujerumani, Dk James Vaupel anadai kuwa vinasaba huchangia kasi ya kuzeeka kwa asilimia tatu pekee na sehemu kubwa ya visababishi vya kuzeeka haraka hutokana na mtindo wa maisha usiofaa pamoja na lishe duni. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI MEI 24, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

ALIYEZAA MTOTO WA AJABU HANDENI ALONGA


Mwajuma Seif (50). PICHA|MAKTABA 



Tangu mwaka 2012 zaidi ya watoto 154 wamezaliwa na wanawake walio juu ya umri wa miaka 50. Miongoni mwao, wamo waliotokana na teknolojia ya upandikizaji. Pamoja na madaktari kuonya kuwa kuzaa katika umri mkubwa kunahatarisha maisha ya mama na mtoto, wanawake hasa matajiri wamekuwa wakizaa katika umri mkubwa. Wilayani Handeni Mkoa wa Tanga, Mwajuma Seif (50) aliweka rekodi ya kujifungua watoto mapacha katika umri huo.

Lakini Mwajuma ana kingine cha ziada tofauti na wanawake wengi wanaozaa katika umri huo; alizaa kwa njia ya kawaida na si kwa teknolojia ya upandikizaji. Tofauti nyingine ya mwanamke huyo si kwamba alizaa katika umri huo kwa kuwa hakuwa na mtoto; ujauzito huo ulikuwa ni wa 13. Daktari anayemwangalia Mwajuma, Elinisa Mushi anasimulia mkasa wa mwanamke huyo akisema pamoja na umri, kingine kilichomshangaza ni mtoto wa ajabu aliyemzaa .

Anaeleza kuwa walimpokea Mwajuma, ambaye ni mkazi wa Kata ya Sindeni zaidi ya mwezi mmoja uliopita akiwa na ujauzito, lakini walishangazwa na tumbo la mama huyo kwani lilikuwa kubwa sana kiasi cha kuhisi kulikuwa na tatizo fulani. Ndipo walipoamua kuanza kumfanyia uchunguzi. Baada ya kupima ujauzito huo kwa kutumia mashine ya ultra sound (kamera ya mionzi), waliona ni kweli tumboni kuna watoto wenye maumbo yasiyoeleweka hivyo walitaka kumsafirisha kumpeleka Hospitali ya Mkoa wa Tanga, Bombo lakini walishindwa kutokana na hali yake. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

UN: VATICAN INAPUUZA HAKI ZA WATOTO

Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis
Kamati ya Umoja wa Mataifa dhidi mateso imelaumu vikali kanisa Catholiki kwa kutoshughulikia ipasavyo suala la unyanyasaji wa ngono ndani ya kanisa hilo.
Katika ripoti iliyochapishwa hivi karibuni na Umoja huo mjini Geneva , Kamati hiyo imeushutumu utawala wa Vatican kwa kuwahamisha watawa kutoka parokia moja hadi nyingine kuwaepusha kushtakiwa, na kupuuza haki za waathiriwa za kupokea fidia .
Utawala wa Vatican uliithinisha mkataba dhidi ya unyanyasaji , ukatili na matendo yaliyo kinyume na utu.
Uchunguzi uliofanywa na kamati ya Umoja wa Mataifa dhidi ya Vatcan ni sehemu ya uchunguzi wa mara kwa mara wa kamati hiyo dhidi ya nchi wanachama ili kuhakikisha mikataba inatekelezwa. Kamati hiyo ya Umoja wa Mataifa ina hofu kuwa wakati utawala wa Vatcan umeelezea kutokubali kamwe kuwepo kwa unyanyasaji ndani ya kanisa, maneno hayaendani na vitendo.
Kamati hiyo imekasirishwa zaidi na kwamba Utawala wa Vatcan unasisitiza kuwa unahusika zaidi na wahudumu wanaofanyika kazi ndani ya Vatcan kwenyewe , kuliko makasisi wake wanaofanyika kazi kwingineko duniani.
Mwezi Januari mwaka huu utawala wa Vatican ulichunguzwa upya na kamati ya Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watoto, baada ya kupokea ukosoaji kama huo kwamba ulishindwa kuwalinda watoto waliokuwa chini ya uangalizi wake. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Chanzo: BBC

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...