Saturday, May 24, 2014

ALIYEZAA MTOTO WA AJABU HANDENI ALONGA


Mwajuma Seif (50). PICHA|MAKTABA 



Tangu mwaka 2012 zaidi ya watoto 154 wamezaliwa na wanawake walio juu ya umri wa miaka 50. Miongoni mwao, wamo waliotokana na teknolojia ya upandikizaji. Pamoja na madaktari kuonya kuwa kuzaa katika umri mkubwa kunahatarisha maisha ya mama na mtoto, wanawake hasa matajiri wamekuwa wakizaa katika umri mkubwa. Wilayani Handeni Mkoa wa Tanga, Mwajuma Seif (50) aliweka rekodi ya kujifungua watoto mapacha katika umri huo.

Lakini Mwajuma ana kingine cha ziada tofauti na wanawake wengi wanaozaa katika umri huo; alizaa kwa njia ya kawaida na si kwa teknolojia ya upandikizaji. Tofauti nyingine ya mwanamke huyo si kwamba alizaa katika umri huo kwa kuwa hakuwa na mtoto; ujauzito huo ulikuwa ni wa 13. Daktari anayemwangalia Mwajuma, Elinisa Mushi anasimulia mkasa wa mwanamke huyo akisema pamoja na umri, kingine kilichomshangaza ni mtoto wa ajabu aliyemzaa .

Anaeleza kuwa walimpokea Mwajuma, ambaye ni mkazi wa Kata ya Sindeni zaidi ya mwezi mmoja uliopita akiwa na ujauzito, lakini walishangazwa na tumbo la mama huyo kwani lilikuwa kubwa sana kiasi cha kuhisi kulikuwa na tatizo fulani. Ndipo walipoamua kuanza kumfanyia uchunguzi. Baada ya kupima ujauzito huo kwa kutumia mashine ya ultra sound (kamera ya mionzi), waliona ni kweli tumboni kuna watoto wenye maumbo yasiyoeleweka hivyo walitaka kumsafirisha kumpeleka Hospitali ya Mkoa wa Tanga, Bombo lakini walishindwa kutokana na hali yake. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Anasema baada ya kugundua kuwa hawataweza kumsafirisha kutokana na hali yake, ilibidi wamuweke katika ulisimamizi maalumu hadi siku ya kujifungua. Alijifungua kwa njia ya upasuaji. Katika upasuaji, madaktari walimtoa mtoto wa kwanza mwenye umbo la ajabu akiwa na kilo sita na wa pili akiwa na kilo 1.5. Anafafanua kuwa mtoto alipotolewa tumboni ingawa hakuwa wa kawaida, alikuwa anapumua. Baada ya muda alianza kutoka maji na saa moja baadaye alifariki dunia. Mtoto mwingine aliishi kwa siku moja na akafariki.

“Alikuwa na kilo sita pia alikuwa amevimba sana. Huu ni uzito mkubwa sana kwa mtoto. Baada ya muda mfupi alianza kutoka maji hadi mwili ukapungua kiasi na baadaye alifariki. Mwenzie aliendelea kuishi kwa saa 24,” anasema Dk Mushi. Mtoto huyo alizaliwa akiwa na miguu yote miwili, lakini iliyoungana na kichwa chenye mdomo na masikio yanayoonekana kwa mbali. Hana kiuno wala mikono.

Dk Mushi anasema kuwa zipo sababu nyingi za kitaalamu ambazo zinaweza kusababisha hali hiyo kutokea na kusema kuwa miongoni mwa sababu hizi ni umri mkubwa wa mwanamke. Anasema mama mwenye umri wa miaka kuanzia 45-50 anashauriwa kupumzika kuzaa, kumeza dawa kali bila ushauri wa daktari miezi mitatu baada ya mimba kutunga na sababu nyingine ni mama mjamzito kuwa ameshajifungua watoto wengine wengi au ameshabeba mimba zaidi ya saba.
Anasema mama huyo tayari alishabeba mimba zaidi ya 10 na baadhi ziliharibika. Hiyo ni dalili ya kutosha kuwa alipaswa kuacha na ikiwezekana kufunga kabisa kizazi ili kuepukana na madhara zaidi ya uzazi.
Dk Mushi anaeleza kuwa kitu kingine ni uelewa mdogo wa jamii kuhusu masuala ya uzazi, kwani wapo baadhi ya wanandoa hawafahamu umuhimu wa kupanga uzazi na badala yake wamekuwa wakipanga uzazi kwa njia za kawaida bila ya ushauri wa daktari.
Kaimu mganga mkuu na mganga mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Handeni, Dk Bakari Mdoe alisema kuwa katika miaka 20 ya kazi ya udaktari, hiyo ni mara ya pili kukutana na kiumbe kama huyo, lakini anasema huyo alizidi kwa kuwa maumbile yake hata hayawezi kuelezeka. Dk Bakari anasema haieleweki mtoto huyo aliathirika na nini hadi akazaliwa akiwa na umbile hilo.
Mwajuma aelezea kisa kizima
Alipohojiwa kuhusu suala hilo, mwanamke huyo alisema mara ya kwanza aliona kuwa amebeba mimba ya kawaida na hakukukwa na tatizo lolote lakini muda ulipokuwa unasonga mbele alishangaa kuona ujauzito ule unakuwa mzito sana. Anasema hali hiyo ilimtisha naye akaamua kukimbilia hospitalini hapo kujua hatima yake, lakini hakupewa jibu la uhakika badala yake aliambiwa abakie hospitalini.
Anasema kuwa mpaka siku ya kujifungua alijua ni watoto wa kawaida na aliposhindwa kujifungua kwa njia ya kawaida na kupelekwa chumba cha upasuaji, ndio akapewa taarifa kuwa kati ya watoto wake wawili, mmoja si wa kawaida, jambo ambalo lilimpa mshituko kidogo lakini ilibidi akubali baadaye kuwa hiyo ni kazi ya Mungu na hakuhusisha na ushirikina.
Anasema hakuwahi kutumia dawa zozote kali na alikuwa anahudhuria kliniki kama kawaida na kufuata masharti yote ya ujauzito. Kwa sasa mama huyo amekubali ushauri wa kufunga kizazi kabisa kwani historia ya uzazi wake inaonyesha hajapata mtoto tangu ashike ujauzito wa 10.
Mama huyo, ambae pamoja na mumewe wanajishuhulisha na kilimo, anasema alifanikwa kupata watoto nane, wakiwemo watano wa kiume na watatu wa kike. Alibahatika kupata mapacha katika mimba yake ya nne. “Nimeamua kukubali kufunga kizazi kwa kuwa nimechoka. Tangu mimba ya 10 hadi hii ya juzi sifanikiwi kupata mtoto zaidi ya matatizo, hivyo ngoja nipumzike hawa ambao Mungu amenijalia wanatosha sasa,” alisema. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Hata hivyo, anaeleza kuwa katika kipindi chote cha uzazi wake, hajawahi kukutana na elimu yoyote ya uzazi wa mpango na kwamba endapo kama angeipata, labda asingepata matatizo hayo. Aidha anasema katika mimba zote 13 ni mbili tu ndio alibahatika kujifungulia hospitalini, na zilizobaki 11 alijifungulia nyumbani kwa uangalizi wa wakunga wa jadi.
Daktari ashauri
Dk Mdoe anatoa ushauri kwa wakina mama na waume zao kujenga tabia ya kwenda kliniki kujifunza uzazi wa mpango. Anasema kuwa ni vema kujenga tabia hizo mapema kwani zinaweza kuwasaidia kwa kufuatilia maendeleo ya mtoto tumboni, kuliko kukaa nyumbani kwani mama mjamzito anaweza kupata matatizo makubwa bila kama ambayo yamekuwa yakimtokea mwanamke huyu.

Aliyevunja Rekodi
Raia wa India, Rajo Devi ndiye mwanamke aliyevunja rekodi mwaka juzi ya kuzaa akiwa na umri mkubwa kuliko wengine duniani. Mwanamke huyo alishika ujauzito akiwa na umri wa miaka 69. Ujauzito huo uliweka rehani uhai wake kwani isingekuwa uangalizi mzuri wa madaktari, mwanamke huyo angepoteza maisha. Kama ilivyo kwa wanawake wengi, mwanamke huyo alishika ujauzito baada ya kufanyiwa upandikizaji wa mayai (IVF).
Pamoja na kuwa madaktari walitabiri mwanamke huyo angekufa mapema kwasababu ya zoezi zima la kumpatia ujauzito kumgharimu nguvu nyingi, mwanamke huyo yupo hai mpaka sasa na binti aliyemzaa, Naveen ameanza shule. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
 Na Rajabu Athuman, Mwananchi

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...