Thursday, October 24, 2013

MAMA KANUMBA "HUYU MCHUNGAJI KAIRUKI ANANITAFUTA KWA KUDAI KANUMBA YUPO HAI"

Baada ya hivi karibuni kuibuka tena kwa yule nabii na Mchungaji George Kaiuruki na kudai kuwa Marehemue Steven Kanumba bado yu hai, FROLA Mtegoa - mama mzazi wa aliyekuwa mwigizaji nyota filamu wa Bongo marehemu Steven Kanumba amesikitishwa na tabia ya mtu anayejiita Nabii George Kairuki kwa kutumia jina na kifo cha marehemu mwanaye kama njia ya kujitengenezea fedha na umaarufu, mama Kanumba anasema kuwa awali Kairuki alitumia msiba wa mwanaye katika kuongelea vitu ambavyo hata familia haivijui isipo kuwa yeye pekee yake.

Mama Kanumba anadai kuwa hivi karibuni Kairuki alijitokeza kwa kudai kuwa Kanumba hajafa na amemtumia fedha katika simu yake, na kusema kuwa karibu atamrudisha duniani na kuendelea na maisha yake jambo ambalo mama wa marehemu anapingana nalo kwa kusema kuwa yeye kwa imani yake anaamini kuwa mwanaye amefariki na hakuna miujiza mingine.

“Huyu mtu anayeitwa Nabii George Kairuki sijui anatafuta nini katika familia yangu, Kanumba alikuwa ni kipenzi cha watu na sisi sote tumeshuhudia hilo kama kweli yeye ana uwezo wa kumfufua amfufue watu wote watafurahi kipenzi chao kurudi kama anavyosema yeye, mimi simjui hata sura zaidi ya kumuona katika picha,”anasema mama Kanumba

Mama Kanumba anasema kuwa iwapo Kairuki ataendelea na tabia hiyo itabidi afanye utaratibu wa kumfungulia mashitaka na hata ikibidi kumfungulia mashitaka na kumfunga endapo ataendelea na tabia ya kutumia sana jina la Kanumba katika kujitafutia fedha na kutangaza maneno ya ajabu ajabu.

VATICAN YAMSIMAMISHA ASKOFU KWA KUPENDA RAHA


Page_12_0_47c17.jpg
Kumekuwa na kelele za waumini nchini Ujerumani wakishinikiza askofu huyo afukuzwe kwa kukiuka taratibu.
Vatican City. Makao Makuu ya Kanisa Katoliki Duniani (Vatican) yamemsimamisha kazi Askofu wa Jimbo la Limburg, Ujerumani Franz-Peter Tebartz-van Elst anayekabiliwa na kashfa ya matumizi mabaya ya fedha kwa shughuli za kifahari.
Vatican ilieleza jana kuwa uamuzi huo umechukuliwa baada ya kuridhika kuwa Askofu van Elst amekiuka maadili yaliyowekwa na Papa Francis kwa viongozi walioko chini yake akiwataka waishi maisha ya uchaji, umaskini.
Hadi sasa, kumekuwa na kelele nyingi miongoni mwa waumini nchini Ujerumani wakitaka askofu huyo afukuzwe kazi.
Miongoni mwa matumizi yake makubwa ni ujenzi wa makazi yake binafsi yaliyogharimu Euro 2.9 milioni (Dola 3.9 milioni), ukumbi wa chakula wenye mita za mraba 63 ambao ni pamoja na mesi na bafu yenye thamani ya Euro 15,000.

M23 WAIVURUGA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

m3 8b114
KUNDI la waasi wa M23, linalopambana na Jeshi la Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), limetajwa kuwa chanzo cha kuisambaratisha Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Kauli hiyo imetolewa juzi na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, katika mahojiano yake na kituo cha redio cha Clouds.


Membe amesema kinachosababisha Tanzania itengwe na baadhi ya nchi wanachama wa jumuiya ya EAC, ni hatua yake ya kupeleka majeshi katika mji wa Goma ulio Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kwa ajili ya kupambana na waasi wanaoipinga Serikali ya Rais Joseph Kabila.
Amesema hatua hiyo ya Tanzania ilizikera baadhi ya nchi wanachama wa EAC, zenye maslahi ya moja kwa moja na kundi hilo na kusisitiza kuwa hata kama itatengwa, kamwe haitaondoa vikosi vyake DRC na badala yake vitaendelea kupambana.

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS OKTOBA 24, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.

.
.

AJALI MBAYA YATOKEA IRINGA JANA




k_fe241.jpg
Daladala aina ya Coster yenye namba za usajiri T.960 AQY inayofanya safari zake za Kibwabwa mjini Iringa mara baada ya kugongana na gari aina ya Isuzu Tipa, lenye namba SM 3363 katika Mlima wa Ipogolo eneo la Kisima cha Bibi.
l_dd9a2.jpg
m_74746.jpg
Taxi ambayo nayo ilisababishiwa ajari ikiwa katika eneo la tukio, huku askari polisi wakilinda usalama wa mali za abiria na baadhi ya vitu katika eneo la tukio.

n_7bc78.jpg
Wananchi wa mji wa Iringa wakitazama ajari hiyo katika mlima wa Ipogolo (Kisima cha Bibi).

MSAFARA WA RAIS KIKWETE WAKUMBWA NA BALAA LA MOTO MKALI

Moto mkubwa ukiteketeza msitu wa Sao Hill Mufindi



 Msafara  wa rais Jakaya  Kikwete ukiwa  umesimama kwa muda eneo la  msitu wa  taifa  wa Sao Hill Mufindi  katika barabara kuu ya Iringa- Mbeya  kufuatia  moto mkubwa kuwaka katika msitu huo jana mchana.


 Askari polisi akimamisha  msafara  wa rais Kikwete kutokana na moto  mkubwa  kutanda  eneo hilo la Changalawe katika  msitu wa Taifa  wa Sao Hill umbali wa mita  mbili kuelekea  barabara  ya Ikulu ndogo mjini Mafinga


 Askari  wa FFU  wakishuka katika gari lao kwenda  kuangalia  usalama  wa rais Kikwete na  kulia gari la kwanza ni naibu waziri wa ujenzi gari la pili la la tatu ni magari ya Ikulu yakiwa  yamesimama


 hapa  askari  wakishuka  kuingia katika moshi mzito  kuangalia  usalama  wa rais katika eneo hilo ambalo moshi mzito  ulitanda barabarani

ZIARA YA WAZIRI MKUU MHE. MIZENGO PINDA CHENGDU - CHINA

IMG_0119
Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda na mkewe Tunu wakipata maelezo kuhusu kiwanda cha kutengeneza maligafi za viwanda vya plastiki cha Hongda Chlor alkali Chemical Base cha Chengdu nchini China akiwa katika ziara ya kikazi Oktoba 22, 2013,. Kushoto ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Abdallah Kigoda. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) IMG_0427
Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda akizungumza na viongozi wa kampuni ya Dalian International ya China kwenye hoteli ya Shangri-la, Chengdu akiwa ktika ziara nchini China. Oktoba 22, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
IMG_0496
Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda akikagua eneo la Mradi wa umwagiliaji la Dujiangyan lililopo Chengdu nchini China akiwa kaika ziara nchini humo Oktoba 22,2013.(Picha naOfisi yaWairi Mkuu)
 IMG_0573
Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda akitia saini kitabu cha wageni baada ya kutembelea mradi wa umwagiliaji wa Dujiangyan uliopo Chengdu nchini China akiwa katika ziara ya kikazi nchini humo   Oktoba 22, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...