Monday, January 20, 2014

AJALI YATOKEA MBALIZI MBEYA, MAGARI ZAIDI YA MATANO YAGONGWA

 Magari yakiwa yamegongwa Mbalizi Mbeya

MWANAJESHI FEKI AKAMATWA TANGA AKIMTAPELI DC

'Koplo' feki wa JWTZ akiwa ofisini kwa mkuu wa wilya.


 'Koplo' feki akijiandaa kupanda  kwenye gari kupelekwa kituo cha polisi kwa mahojiano zaidi

SOMA SABABU YA MAWAZIRI MIZIGO KUACHWA KWENYE BARAZA LA MAWAZIRI...!!!


RAIS JAKAYA KIKWETE.

SERIKALI imetoa kauli kuhusu tuhuma zilizokuwa zikiwakabili baadhi ya mawaziri, waliobatizwa jina la ‘Mawaziri Mizigo’, na hatua ambazo zimekuwa zikichukuliwa kukabiliana na kero zilizosababisha wapewe jina hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Ikulu Dar es Salaam, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Safue, alisema mawaziri hao walituhumiwa kutokana na changamoto zilizopo katika wizara zao; na si upungufu wao binafsi kama viongozi.

Mawaziri hao saba walitajwa katika ziara ya mikoani ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na baadae walihojiwa katika kikao cha Kamati Kuu cha chama hicho.

Baada ya kuhojiwa, Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alisema Kamati Kuu ilimuachia Rais Kikwete jukumu la kuamua kuwafukuza kazi, kuwahamisha au kuwataka kutekeleza majukumu yao kikamilifu.

Miongoni mwa mawaziri waliohojiwa ni aliyekuwa Naibu Waziri wa Fedha, Saada Mkuya, ambaye sasa ameteuliwa kuwa Waziri wa Fedha.

HII NDIO THAMANI YA JINO MOJA LA NDOVU NA JINSI BIASHARA INAVYOFANYWA

  2013-04-28-TimphotobyCarlSafina.JPG
Yafuatayo ni kuhusu biashara ya meno ya tembo

Kwanza: Matumizi yake; meno ya tembo hutumika kutengeneza vitu vya urembo kama vile hereni , mikufu, mapambo kama vile sanamu na hata keys za keyboards za vinanda.
Vifaa vilivyotengenezwa kwa meno ya tembo hutumika nchini China kama sehemu ya kuonyesha ufahari, kwa mujibu wa Wikipedia.


Pili: Bei ya meno ya tembo

Bei inategemea na soko , hata hivyo kwa mujibu wa answers.com , jino moja la tembo huweza kuuzwa kwa dola za kimarekani mia saba (700).

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...