Tuesday, September 03, 2013

WIMBO MPYA WA DIAMOND - NUMBER ONE


MWANAMKE ANASWA NA SARE ZA JWTZ....!!!


JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limemkamata Saida Mohamed (30), mkazi wa Mwasonga Kigamboni, akiwa na sare za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ). 
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleimani Kova, alisema mtuhumiwa huyo alikamatwa Agosti 31, mwaka huu, katika eneo la Mwasonga, Kigamboni.

Alisema Saida alikamatwa na suruali saba, mashati saba ya kombati, kofia 10, shati mbili nyepesi, fulana mbili na kofia moja aina ya bareti, vyote vikiwa mali ya JWTZ.

Alisema mtuhumiwa huyo, alikuwa na begi moja la kuwekea nguo za jeshi, cheo kimoja cha Koplo na mikanda miwili ya kijeshi.

Alisema uchunguzi unaendelea juu ya mwanamke huyo ili kubaini sababu za kumiliki sare za jeshi, kabla ya kufikishwa mahakamani.

Katika tukio jingine, polisi wamemkamata Husein Mkondoa (25), mkazi wa Gongolamboto Mzambarauni, akiwa anaendesha pikipiki huku akiwa amevaa nguo za kiraia na kofia ngumu ya kijani yenye nembo ya Polisi.

VIDEO MPYA YA GK - BARAKA AU LAANA


MAGAZETI YA LEO JUMANNE SEPTEMBA 3, 2013

DSC 0008 e4878
DSC 0009 047f4

RWANDA YAONGEZA USHURU KWA MIZIGO IPITAYO BADARI YA DAR TU

paul kagame 2d247
NI dhahiri sasa biashara ya kupitisha mizigo katika Bandari ya Dar es Salaam, imekuwa moto, baada ya Serikali ya Rwanda kupandisha tozo ya ushuru kutoka dola za Marekani 152 hadi 500 ambazo ni sawa na Sh 800, 000 za Tanzania.
Hali hii inawezekana kwa namna moja au nyingine, imetokana na mzozo kati ya Rais Jakaya Kikwete na Rais Paul Kagame wa Rwanda, ambao umepelekea wafanyabiashara wa Rwanda na Uganda kutishia kuacha kupitisha mizigo yao katika Bandari ya Dar es Salaam.


Itakumbukwa mzozo huo, umekuja baada ya Rais Kikwete kumshauri Rais Kagame akubali kukutana na waasi wanaoendelea na vita mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), lakini ushauri huo unaonekana kupokelewa tofauti na Rais Kagame.
Siri ya kupandishwa kwa gharama hizo, imefichuka jana baada ya malori mengi ya wafanyabiashara wa Tanzania kukwama katika mpaka wa Rusumo mkoani Kagera.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...