Wednesday, October 16, 2013

WAZIRI MKUU MH. MIZENGO PINDA AWASILI CHINA NA KUPOKEA TAARIFA, ASIKITISHWA NA USAFIRISHAJI WA DAWA ZA KULEVYA



IMG_0072
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
*Asikitishwa na idadi kubwa ya wasafirishaji wa dawa za kulevya

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amewasili Beijing, China saa 10 leo jioni (Jumatano, Oktoba 16, 2013) na kuanza vikao ikiwa ni sehemu ya ziara ya kikazi yake ya siku tisa kwa mwaliko wa Serikali ya nchi hiyo.
Mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Beijing, Waziri Mkuu alielekea kwenye nyumba ya wageni ya Serikali ya Diaoyatui ambako alipokea taarifa fupi kuhusu hali ya kisiasa na kiuchumi nchini China.
Akiwasilisha taarifa hiyo mbele ya Waziri Mkuu, Balozi wa Tanzania nchini China, Luteni Jenerali (Mst.), Abdulrahman Shimbo alisema sehemu kubwa ya utekelezaji wa miradi kati ya Tanzania na China iko chini ya mwamvuli wa FOCAC (Forum on Africa China Cooperation) ambayo inagawanyika katika maeneo sita.
 Alyataja maeneo hayo kuwa ni misaada (grants), mikopo ya masharti nafuu (preferential loans), mikopo ya kibiashara (preferential buyers credit), uwekezaji, ushirikiano maalum na ushirkianao wa kihistoria.

RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN ASISITIZA AMANI BARAZA LA IDD ZANZIBAR

DSC_0112
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein wapili kushoto akiomba Dua pamoja na viongozi wengine wa Kitaifa katika Swala ya Idi –El-Hjji ilioswaliwa Kitaifa huko katika kitongoji cha Marumbi Mkoa wa Kusini Wilaya ya Kati Unguja.kulia kwake ni Kadhi Mkuu wa Zanzibar Khamis Haji Khamis na kushoto yake ni Katibu mtendaji wa Wakfu na Mali ya Amana Sheikh Abdalla Twalib,Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanizbar Maalim Seif Sharif Hamadi na wamwisho ni Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Mahmod Mussa Wadi. DSC_0230
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein akitoa hotuba katika baraza la Idi -El-Hajji lililofanyika huko Tunguu Mkoa wa Kusini Wilaya ya Kati Unguja DSC_0206
Baadhi ya Viongozi na Wananchi waliohudhuria katika Baraza la Idi-El-Hajji lililofanyika huko Tunguu Mkoa wa Kusini Wilaya ya Kati Unguja
PICHA ZOTE NA YUSSUF SIMAI ALI-HABARI MAELEZO ZANZIBAR

MUME AMKATA MKEWE MGUU HUKO TARIME MKOANI MARA

Na Waitara Meng’anyi, Tarime


 Ghati Chacha (21) mkazi wa kijiji cha Nyanitira kata ya Nyansincha Wilayani Tarime amesababishiwa kilema cha maisha kwa kukatwa mguu wake wa kulia na Mume wake baada ya kuchelewa kumfungua mlangao nyakati za usiku.

Akisimulua mkasa huo hivi karibuni akiwa wodi namba sita alikolazwa akiuuguza vidonda na majeraha,Ghati alisema, mume wake  aliye mtaja kwa majina ya Chacha Mwita(23) alifika nyumbani saa mbili usiku akiwa amelewa.

ANGALIA VIDEO YA RAIS KIKWETE ALIPOKUTANA NA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA


JAMBO TZ INAWATAKIA EID MUBARAK NYOTE!


KUMBE SHOW ZA MAJUU SIO KAMA ZA BONGO! - OMMY DIMPOZ


Ommy alikuwa akiongea na kipindi cha Ampilifaya jana baada ya kurejea kutoka nchini Marekani alikokuwa kwenye ziara ya wiki tatu.

“Naweza kusema hapa nyumbani tunalipwa hela nyingi kuliko tunavyopata nje kwa msanii yeyote kwa asilimia kubwa. Inategemea pia unaenda kufanya tamasha sehemu gani. Kwahiyo asilimia kubwa hela unatengeneza zaidi nyumbani,”alisema Ommy.

Alisema hiyo ni kwasababu show za Tanzania huhudhuriwa na watu wengi zaidi kuliko inavyokuwa nchi za nje ambako ni watu wachache sana huingia japo kiingilio ni kikubwa na wengi wanaohudhuria ni watu waliotoka Afrika Mashariki zaidi.
Katika hatua nyingine, leo Ommy Dimpoz kupitia Instagram, ameandika maneno ya shukrani kwa wote walioifanikisha show yake.

“AssaLaam ALeykum Ndugu zangu, Eid MubaraQ Ndugu, jamaa, Marafiki, and all my Fans all over the world…Namshukuru Mungu Alhamdulilah nimerudi nyumbani Salama Kuendelea na Majukumu mengine baada ya Tour ya Takriban Mwezi Mmoja…Ningependa kuchukua Nafasi hii kuwashukuru @Dmkglobal promotion na J&P kwa kufanikisha tour yangu ambayo imeweza kuwa na Mafanikio makubwa Na kufanikisha baadhi ya malengo ambayo mengine sikuyatarajia.Pia ningependa kuwashukuru watu wote ambao walionyesha support kipindi chote cha tour yangu hususan Watanzania wenzangu na Watu wa Africa Mashariki na Kati ambao walionyesha Ushirikiano na support ya kutosha tangia mwanzo mpaka mwisho wa tour yangu…Nachoweza kuwaahidi ni kuwa mengi mazuri Yanakuja na Naimani sitawaangusha.Nawatakia mapumziko na sherehe njema za sikukuu ya Idd…. Mimi na team nzima ya pozkwapoz tutakuwa DARLIVE tukitoa Huduma Karibuni sana.LOVE U ALL.” na Vijimambo Blog

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASHIRIKI SWALA YA EID EL HAJ MSIKITI WA ANWAAR MSASANI, DAR ES SALAAM

 Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na waumini wa dini ya Kiislamu baada ya kushiriki nao katika Swala ya Sikukuu ya Idd El Haj, iliyofanyika katika Msikiti wa Anwaar uliopo Msasani, jijini Dar es Salaam leo. Picha zote na Ofisi ya Makamu wa Rais
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na waumini kushiriki Swala ya Sikukuu ya Idd El Haj na Waumini wa dini ya Kiislam katika Msikiti wa Anwaar, uliopo Msasani jijini Dar es Salaam, leo asubuhi.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO OKTOBA 16, 2013

DSC 0137 46fbc
DSC 0138 47cac

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...