Thursday, October 27, 2016

SERIKALI YATANGAZA MATOKEO YA DARASA LA SABA 2016

Serikali imetangaza matokeo ya mtihani wa darasa la 7 kwa mwaka 2016 ambapo ufaulu umeongezeka kwa asilimia 2.52 na shule iliyoongoza kitaifa ni shule ya Msingi Kwema ya mkoani Shinyanga. 

Mtihani huu ulifanyika tarehe 7 na 8 mwezi Septemba mwaka huu. Kutazama matokeo hayo bofya hapa.

Wednesday, October 26, 2016

MAGAZETI YA LEO JUMATANO OCTOBA 26, 2016 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

20161026_041718
20161026_041734
20161026_041746

Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

MPIGIE KURA RAIS MAGUFULI ASHINDE TUZO ZA MTU MASHUHURI ZA FORBES

Rais John Magufuli ni miongoni mwa watu mashuhuri barani Africa waliopendekezwa kuwania tuzo ya FORBES AFRICA PERSON OF THE YEAR 2016.

Mpaka sasa rais Magufuli anaongoza kwa 80% ya kura zote zilizopigwa. Unaweza kumpigia kura yako hapa.

Share na wenzio.

Tuesday, October 25, 2016

MABUSHA TATIZO LA WENGI JIJINI DAR

UTAFITI uliofanywa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii unaonyesha kuwa wakazi wa Mkoa wa Dar es salam 6800 tayari wamepata athari ya matende na mabusha. 

 Akizungumza katika zoezi hilo Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dk Grace Magembe alisema mpaka sasa tayari watu 104 kwa Mkoa wa Dar es Salaam wameshafanyiwa upasuaji wa mabusha. 

Alisema kutokana na idadi kubwa ya wagonjwa wa mabusha Jijini Dar es Salaam wanatarajia kuwafanyia upasuaji wagonjwa 1000. 

Akizungumza wakati wa ugawaji wa dawa za kinga tiba ya Matende, Minyoo na Mabusha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, alisema kuwa kiwango hicho ni kikubwa sana kwa wakazi wa dar es salaam kwani mpaka sasa watanzania milioni 2.7 wameathirika na magonjwa yasiyopewa kipaumbele ikiwemo ngiri maji pamoja na matende hususani vijijini. 

Alisema zoezi la utoaji wa dawa za kinga tiba litatolewa bure ambapo zaidi ya watanzania milioni 4.5 wanatarajiwa kupata kinga tiba hizo. 

 “Kinga tiba imeanza kutolewa Oktoba 25 hadi 29 kwa watu wenye umri kuanzia miaka 5 na kuendelea kwa kumeza dawa za Mectizan na Albendazole za kukinga na kutibu magonjwa ya minyoo tumbo,mabusha na matende,” alisema Makonda.

FORBES: RAIS MAGUFULI KUWANIA TUZO YA FORBES YA MTU MASHUHURI

Ikiwa ni mwaka mmoja tangu kufanyika kwa uchaguzi mkuu,Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli ameteuliwa kuwania tuzo la Forbes la mtu mashuhuri wa mwaka.

 Jarida hilo la biashara limemtambua rais Magufuli kwa umuhimu wake katika kuimarisha uchumi wa taifa. Wengine walioteuliwa kuwania tuzo hiyo ni pamoja na Benki ya Capitec nchini Afrika Kusini, Rais wa Mauritania, Mtetezi wa haki za umma nchini Afrika Kusini na raia wa Rwanda. 
Mwaka uliopita tuzo hilo lilichukuliwa na mfanyibiashara wa Tanzania Mohammed Dewiji.

Chanzo: BBC Swahili

Sunday, October 02, 2016

MSANII WA JAMAICA ALIYEJICHORA TATTOO YA MAGUFULI....!!!

Las Laciano

Mwanamziki wa Jamaica Las Laciano aliyewahi kutamba na nyimbo kadhaa, ikiwemo "its me against jah" amejichora tatoo ya rais kutokea Africa anayemkubali, ambaye ni rais wa Tanzania Mh. Dr. John Magufuli. 

Sababu ni kuwa ndo rais muwajibikaji, anayeona mbele hatishiwi na matatizo ya mpito ila anatishiwa na matatizo ya muda mrefu kama rushwa, urasimu na uzembe kazini. Mheshimiwa Magufuli ameendelea kugonga kimataifa na anazidi kukubalika.

Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz.
https://m.facebook.com/jambotz/

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...