Sunday, September 22, 2013

"SERIKALI KURUDISHA O’LEVEL KATIKA SHULE KONGWE" PINDA


Pinda1 WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema Serikali imeanza kushughulikia utaratibu wa kurejesha utoaji wa elimu ya kidato cha kwanza hadi kidato cha nne katika baadhi ya shule kongwe ili kurudisha ufaulu uliokuwepo na kuimarisha malezi ya watoto kuanzia elimu ya chini.

Amesema uamuzi huo unafuatia kaulimbiu ya kutaka kuwajengea wanafunzi maadili mema katika mazingira ya shule za sekondari tangu wanapoingia kidato cha kwanza badala ya mfumo wa sasa ambapo wanakuja kupata mafunzo hayo kidato cha tano na cha sita lakini wanakuwa hawajapata msingi imara tangu wakiwa wadogo.

Ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumamosi, Septemba 21, 2013) wakati akizungumza na mamia ya wanajumuiya waliohitimu katika shule hiyo (Alumnae), wanafunzi waliopo pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria sherehe za Jubilei ya miaka 50 ya Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Weruweru.

Waziri Mkuu ambaye alikuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo, alikuwa akijibu maombi yaliyotolewa na Dk. Maria Kamm ambaye aliongoza shule hiyo kwa miaka 22 kuanzia mwaka 1970 hadi 1992, pamoja na wazungumzaji wengine katika sherehe hizo.

Alisema Serikali ilikwishatoa maelekezo kwa Makatibu Tawala wa Mikoa kwa ajili ya shule tano ambazo ziliondolewa madarasa ya kidato cha kwanza hadi cha nne na mojawapo ya shule hizo ni Sekondari ya Wasichana ya Weruweru.


PICHA MBALIMBALI ZA SHAMBULIO LA KIGAIDI JIJINI NAIROBI JANA AMBALO LIMEUWA ZAIDI YA WATU 60 NA WATU 100 WAMEJERUHIWA VIBAYA SANA








MATUKIO YALIYOJILI KATIKA MKUTANO WA KATIBA ULIOFANYIKA VIWANJA VYA JANGWANI JANA







 Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Azaveli Lwaitama.




 Askofu Zakaria Kakobe akihutubia katika Mkutano wa Katiba Viwanja vya Jangwani.




 Mbunge wa Ubungo Mh John Mnyika akihutubia katika Mkutano wa Katiba Ulioitishwa na Umoja wa Vyama vya siasa, Wanaharakati na Viongozi wa Dini.

SIMBA, MBEYA CITY ZAINGIZA MIL 123/-

Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Mbeya City iliyochezwa jana (Septemba 21 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 123,971,000.
Watazamaji 21,936 ndiyo waliokata tiketi kushuhudia mechi hiyo namba 32 ya VPL msimu wa 2013/2014 iliyomalizika kwa timu hizo kutoka sare ya mabao 2-2.
Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 30,064,741.95 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 18,910,830.51. 
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 15,287,156.92, tiketi sh. 3,145,790, gharama za mechi sh. 9,172,294.15, Kamati ya Ligi sh. 9,172,294.15, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 4,586,147.08 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 3,567,003.28.
Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI SEPTEMBA 22, 2013

DSC 0001 7a34a
DSC 0002 72785

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...