Saturday, May 17, 2014

MSANII NA MUONGOZAJI WA FILAMU 'ADAM KUAMBIANA' AMEFARIKI DUNIA GHAFLA ASUBUHI YA LEO...!!!

Adam Kuambiana enzi za uhai wake.
Mwili wa Marehemu Adam Kuambiana ukitolewa nje ya Hospitali  ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge jijini Dar es Salaam kupelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kuhifadhiwa leo mchana huu. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

HOMA YA DENGUE, MABASI 600 KUPULIZIWA DAWA

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki

Serikali imeiagiza Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), kuhakikisha mabasi yote 600 yanayofanya safari zake mikoani yanapulizia dawa ya kuondoa mazalia ya mbu wanaoeneza ugonjwa wa dengue.

Manispaa za Dar es Salaam zimetengewa Sh. milioni 218 kwa ajili ya kununua dawa na vifaa vya kupulizia mazalia ya mbu hao.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki alisema kuwa tayari serikali imefanya jitihada mbalimbali katika kuhakikisha ugonjwa huo unadhibitiwa ili usienee kwa wengine. Alisema mabasi yatakayokaidi agizo hilo yatafungiwa safari zake lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha ugonjwa huo hausambai katika mikoa mingine.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki alisema kuwa tayari serikali imefanya jitihada mbalimbali katika kuhakikisha ugonjwa huo unadhibitiwa ili usienee kwa wengine.

Alisema mabasi yote yanatakiwa kuhakikisha yanapulizia dawa ili yanapoanza safari zake ili yasiondoke na mbu hao katika mikoa mengine. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

FILAMU YA JOTI SANDUKU LA BABU KUINGIA SOKONI HIVI KARIBUNI

Msanii Lucas Mhavile 'Joti'baada ya kukaa kimya kwa mda sasa ameibuka na filamu yake ya Joti Sanduku la Babu ambayo amecheza katika husika tofauti tofauti.
Filamu hiyo itakuwa ikisambazwa na Kampuni yaproin promotions ya jinini Dar es salaam akizungumzia filamu hiyo Joti alisema kuwa amekuja kivingini kwani kitu alichofanya katika filamu hiyo haijawai kutokea wala kufanywa na mtu yoyote yule katika tasinia hii ya filamu nchini hivyo wapenzi wangu wakae mkao wa kula tu kwani wakati wowote kuanzia sasa itakuwa inaingia sokoni kwani filamu hii si yakukosa mana unambiwa uzee mwisho chalinze mjini kila mtu honey hivyo wapenzi wa filamu nawaomba wanunue nakala alisi ya filamu hiyo pindi itakapotoka ambapo nimelezea mambo mbalimbali ya ujana usichana pamoja na uzee mbali na hivyo filamu hiyo imebeba mambo matatu muhimu kwanza ina burudisha pia ina elimisha na kupata ujumbe muhimu kabisa katika jamii inayotuzunguka' filamu hiyo ya kwanza tangu joti aweke kando mambo ya filamu na kujingiza katika mambo ya uchekeshaji kupitia luninga sasa ameludi tena katika filamu yake mwenyewe inayokwenda kwa jina la Joti sanduku la babu. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI MEI 17, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

PROFESA LIPUMBA AWASHANGAA VIJANA WA IRINGA

Baadhi ya vijana waliohudhuria mkutano huo

Lipumba wa CUF akisisitiza jambo

Mchungaji Msigwa wa Chadema
Danda Juju wa NCCR-Mageuzi
 Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

ASKOFU DALLU KUSIMIKWA RASMI KESHO


dalu_1b119.jpg
Balozi wa Baba Mtakatifu nchini Tanzania Askofu Mkuu Fransisko Montecillo Padilla, anataraji kuongoza Misa Takatifu ya kusimikwa kwake Askofu Mpya wa Jimbo Kuu la Songea, Mhashamu Damian Dennis Dallu (Pichani).

Tukio hilo litafanyika katika Kanisa la Mtakatifu Mathias Mulumba Kalemba la Jimbo Kuu la Songea hapo kesho. Leo hii baadhi ya waumini wamesafiri mpaka katika mpaka wa Mkoa wa Ruvuma na Njombe kwa ajili ya kumpokea Askofu Dallu anayeingia Jimboni Songea na leo Jumamosi atafanyiwa Ibada ya kukabidhiwa Kanisa.

Tukio hilo linalotaraji kuhudhuriwa na Viongozi wengi wa Madhehebu ya dini, litahudhuriwa pia na Rais mstaafu wa awamu ya tatu Mheshimiwa Benjamin Wiliam Mkapa. (PERAMIHO PUBLICATIONS)
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

WATU 10 WAUAWA KATIKA MILIPUKO NAIROBI

Haijulikani na nani aliyesababisha milipuko ingawa washukiwa tayari wamekamatwa
Milipuko miwili ilitikisa Soko kubwa la nguo la Gikomba mjini Nairobi na kuwaua watu 10 huku zaidi ya hamsini wakijeruhiwa..
Soko hilo linapakana na mtaa wa Easleigh ambako wasomali wengi wanaishi na kufanya kazi.
Shirika la serikali la kushughulikia majanga linasema kuwa angalau watu 10 wamefariki na wengine zaidi ya hamsini kujeruhiwa.
Mlipuko wa kwanza ulitokea katika gari la abiria wakati la pili likitokea ndani ya soko.
Soko la Gikomba ni maarufu kwa nguo za mitumba
Milipuko hiyo ilitokea siku moja baada ya Uingereza kutoa onyo kwa raia wake wanaoishi nchini humo kurejea makwao kwa hofu ya usalama na pia baada ya tahadhari kutolewa ya kutokea kwa mashambulizi ya kigaidi nchini humo.
Gikombaa ni soko kubwa la kuuza nguo ambalo linapakana na mtaa wa Eastleigh ambako wasomali wengi wanaishi na kufanya kazi.
Kenya imekuwa ikikumbwa na mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kwa wawu wenye uhusiano na kundi la wanamgambo la kiisilamu nchini Somalia la Al Shabaab. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC Swahili

USALAMA WA NIGERIA KUANGAZIWA UFARANSA

Kiongozi wa kundi la Boko Haram Abubakr Shekau
Rais wa Ufaransa Francois Hollande anaanda mkutano hii leo mjini Paris kuangazia hali ya usalama nchini Nigeria.
Mkutano huo utawaleta pamoja viongozi kutoka nchi za Nigeria,Benin,Cameroon,Chad na Niger ili kutafuta njia za kukabiliana na kundi la wanamgambo wa kiislamu wa Boko haram.

Wawakilishi wa Marekani muungano wa Ulaya na Uingereza wataangazia kazi iliofanywa na wataalam wa Uingereza, Ufaransa na Marekani waliotumwa nchini humo ili kuisaidia mamlaka ya Nigeria kuwanusuru zaidi ya wasichana 200 waliotekwanyara na kundi hilo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Chanzo: BBC Swahili

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...