Wednesday, March 28, 2018

TANESCO KUTUMIA MFUMO MPYA WA MALIPO YA SERIKALI KUUZA UMEME WA LUKU

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema wateja wake wote wanaotumia mita za malipo ya kabla yaani (LUKU) kuwa, kuanzia April 2, mwaka huu shirika hilo itahamia rasmi katika mfumo wa malipo wa Serikali ujulikanao Government e-Payment Gateway (GePG).

Mfumo utaanza kutumika kutokana na matakwa ya sheria kwa taasisi za Serikali. Taarifa ya Ofisi ya Uhusiano ya TANESCO makao makuu imeeleza kuwa shirika hilo ni miongoni mwa Taasisi za Serikali, hivyo itaanza kutumia mfumo huu kwa kufanya mauzo ya LUKU kupitia ofisi zake kampuni za simu pamoja na benki zote zinazofanya mauzo ya LUKU kupitia huduma za kibenki. 

"Serikali kwa kushirikiana na wataalamu wa TANESCO itahakikisha kuwa mfumo huu unafanya kazi bila kuathiri manunuzi ya LUKU. Ifahamike TANESCO ni miongoni mwa Taasisi za Serikali zitakazotumia mfumo huu mpya na hadi hivi sasa taasisi nyingine za Serikali zimeshaanza kutumia kwa mafanikio.

DIAMOND, MWAKYEMBE, SHONZA WAMALIZA BIFU LAO

Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe jana Jumanne Machi 27, 2018 amekutana na mwanamuziki Nassibu Abdul 'Diamond Plutnumz' jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kaimu mkuu wa kitengo cha mawasiliano Serikalini, Lorietha Laulence imesema lengo la kukutana kwa wawili hao ni kulejesha maelewano kwenye tasnia ya muziki kufuatia hatua zinazochukuliwa na Wizara hiyo kufungia baadhi ya nyimbo zikiwemo mbili za mwanamuziki huyo.
Imeeleza kuwa katika kikao hicho kilichofanyika ofisi za Wizara hiyo na kuchukua zaidi ya saa tatu, kiliudhuriwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Juliana Shonza, katibu mtendaji wa Balaza la Sanaa la Taifa (BASATA) Godfrey Mwingereza.

VIWANJA VYA NDEGE 10 BORA HIVI HAPA

Tovuti ya utafiti wa anga ya Skytrax ya nchini Uingereza imetoa orodha ya viwanja vya ndege bora duniani ambapo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Singapore Changi umeshika nafasi ya kwanza.



Orodha ya viwanja 10 vinavyoongoza kwa ubora ni;
1. Singapore Changi Airport
2. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Incheon (Seoul, Korea Kusini)
3. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Tokyo Haneda)
4. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hong Kong
5. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hamad (Doha, Qatar)
6. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Munich (Ujerumani)
7. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Chubu Centrair Nagoya (Japan)
8. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa London Heathrow
9. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zurich (Switzerland)
10. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Frankfurt (Ujerumani)

JESUS AWAFUTA MACHOZI BRAZIL

Timu ya taifa ya Ujerumani walishindwa kwa mara ya kwanza katika mechi 23 baada ya mshambuliaji wa Manchester City Gabriel Jesus kuwafungia Brazil bao moja na kuwapa ushindi wa 1-0 jijini Berlin.

Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kwa mataifa hayo mawili kukutana uwanjani tangu Ujerumani walipowaaibisha Brazil 7-1 katika nusu fainali ya Kombe la Dunia mwaka 2014 mjini Belo Horizonte.
Jesus aliwaweka Brazil mbele kwa mpira wa kichwa dakika za mwishi mwisho kipindi cha kwanza, dakika ya 37.

ARGENTINA WACHEZEA KICHAPO KITAKATIFU TOKA KWA UHISPANIA

Katika mchezo uliochezwa jana Mjini Madrid, Isco alifunga mabao matatu na kuwasaidia Uhispania kupata ushindi mnono wa 6-1 dhidi ya Argentina ambao walifika fainali Kombe la Dunia 2014.

Uhispania waliongoza 2-0 baada ya Diego Costa kumbwaga Sergio Romero kisha Isco akafunga bao lake la kwanza.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...