Tuesday, August 19, 2014

WAPENZI WA JINSIA MOJA KENYA KUPIGWA MAWE HADI KUFA...!!!

Screen Shot 2014-08-19 at 8.03.13 AM
(Nje ya bunge la Kenya. Picha na Maktaba)
 
Bunge la taifa nchini Kenya linapanga kujadili sheria ya kipekee inayopendekezakupigwa mawe hadi kufa kwa raia wa kigeni atayeshiriki mapenzi ya jinsia moja huku wazawa wakikuhukumiwa kifungo cha maisha jela.

Mwandishi na mdhamini wa sheria hiyo Edward Onwong’a Nyakeriga anapendekeza kuharamishwa kwa ulawiti na kisha kuhukumiwa jela kwa wale wanaotenda kosa hilo huku akisisitiza kuwa upo umuhimu wa kuwalinda watoto na vijana ambao wanalengwa na dhulma ambazo kwa mda mrefu zinaepukwa kutokana na mabadiliko ya teknolojia na habari isiyo chujwa na watoto yatima kukosa mwakilishi pamoja na majaribio ya wanaoshiriki uhusiano wa jinsia moja kuwalea watoto ilihali wanaendeleza uhusiano wao’
 Screen Shot 2014-08-19 at 8.06.26 AM
Muswada huo wa chama cha Republican Liberty Party unaharamisha uhusiano wowote wa jinsia moja na tayari umeungwa mkono na wabunge zaidi ya 78 na wengine zaidi wanaendelea kushawishiwa. Pia spika wa Bunge Mh. Justin Muturi ameupokea na kuuwasilisha katika kamati ya sheria bungeni ambayo inatathmini kisha kutoa ripoti kwa bunge.
 Mmoja kati ya waaandishi wa vitabu maarufu nchini Kenya Binyavanga Wainaina amekua miongoni mwa waliojitokeza hadharani na kukiri kushiriki mapenzi ya jinsia moja na wakati huohuo Mashirika ya kutetea haki za wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja hivi karibuni yaliwasilisha pendekezo la kutaka Wabunge kuondoa sheria zote zinazowazuia kuishi maisha yao kama watu wengine. Muswada huo unatarajiwa kupata upinzani mkali kutoka kwa wanaotetea haki za binadamu.
Kwa upande wa Katiba ya Kenya ya mwaka 2010 imeharamisha ndoa ya jinsia moja japo haiharamishi moja kwa moja uhusiano wa mapenzi ya jinsia moja ambapo pia mwezi uliopita utafiti uliofanywa na kampuni ya Ipsos Synovate umeonyesha kwamba 64% ya Wakenya wanaamini kwamba hisia za kushiriki mapenzi na jinsia sawa ni jambo la kujifunza ilihali 14% kati yao wanaamini watu hao huzaliwa walivyo.

Chanzo: Millard Ayo

UAMUZI MGUMU CCM KATIKA KAMATI KUU LEO

Kamati Kuu (CC) ya Halmashauri Kuu ya CCM inakutana leo mchana mjini Dodoma chini ya mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete huku ikitarajiwa kufanya uamuzi mgumu wa mchakato wa Katiba.

Kikao hicho kinaketi mara ya pili katika muda mfupi, baada ya hivi karibuni kukaa jijini Dar es Salaam na kueleza kuridhishwa na mchakato huo.

Hata hivyo, safari hii kikao hicho kinaketi kukiwa na maswali lukuki ambayo hayajapata majibu: Je, Bunge la Katiba liendelee au livunjwe? Je, lisitishwe kwa muda kupisha maridhiano au la? Je, kuna umuhimu wa maridhiano? Kuna ulazima wa kuwapo Ukawa bungeni?

Akizungumzia kikao hicho, mtaalamu wa sayansi ya siasa na utawala katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Alexander Makulilo alisema jambo kubwa litakalojadiliwa katika kikao hicho ni kauli tofauti zilizotolewa na wananchi kuhusu mchakato wa kupata Katiba Mpya. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

"KAULI YA WEREMA NI YA KINAFIKI" MBATIA


Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia (kulia) akizungumza na waandishi jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Mosena Nyambabe.


Siku moja baada Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema kueleza kuwa hakuna mwenye mamlaka kisheria kuvunja au kusitiza Bunge la Katiba, mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi amesema kauli hiyo imejaa unafiki na kwamba upo uwezekano wa kuahirisha vikao kwa muda mpaka mwafaka wa kitaifa utakapopatikana.

Mwenyekiti huyo, James Mbatia amesema kuahirisha Bunge kunawezekana kama ambavyo iliwezekana kusitishwa vikao vya Bunge hilo Aprili mwaka huu kupisha Bunge la Bajeti na kubadilishwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba kinyemela kwa kuongeza idadi ya siku za Bunge la Katiba kutoka 70 hadi 90 mpaka kuwa muda wowote ambao utaonekana unafaa.

Wakati Mbatia akieleza hayo, jana waliibuka wazee wa Jiji la Dar es Salaam wakiwataka Watanzania kuyaombea makundi yanayovutana na moja likisusia vikao vya Bunge hilo vinavyoendelea mjini Dodoma, ili yakutane na yakubali kufikia mwafaka kwa pamoja.

Kauli ya Mbatia

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mbatia alisema kauli iliyotolewa juzi na Jaji Frederick Werema imejaa unafiki. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE AGOSTI 19, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SOMA ALICHOANDIKA MAULID KITENGE BAADA YA KUACHA KAZI ITV/ RADIO ONE

Screen Shot 2014-08-19 at 8.22.01 AM 
Maulid Kitenge yuko kwenye orodha ya Watangazaji wa muda mrefu wa michezo nchini Tanzania ambapo ujazo wa jina lake uliongezeka baada ya kuanza kufanya kazi na ITV/RadioOne zaidi ya miaka 10 iliyopita.
August 18 2014 Maulid aliandika yafuatayo kwenye page yake ya twitter >>> ‘Namshukuru sana Mungu leo nimemaliza miaka 14 ya kutumika kuwa kama mtangazaji wa michezo Radio one stereo na hakika naondoka rasmi
Mpaka asubuhi ya August 19 2014 Maulid alikua hajaandika tweet nyingine ya anakokwenda au atakachofanya baada ya kuondoka ITV/Radio One
Screen Shot 2014-08-19 at 8.16.51 AM

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WATU WEUSI WABAGULIWA KOREA KUSINI...!!!

Watu weusi wanyanyapaliwa Korea Kusini
Tangu kuanza kwa ugonjwa wa Ebola kumekuwapo na malalamiko ya watu wanaotoka Barani Afrika kutengwa kwa kutopewa huduma za kijamii nchini Korea ya kusini ikiwamo kutoruhusiwa kuingia katika Migahawa na usafiri wa umma kwa madai ya kuwa huenda wana virusi vya Ebola.

Aidha, baadhi yao wamedai watu weusi wanaposimamisha TAXI hazisimami kutokana na hofu ya virusi hivyo vya Ebola. Nimezungumza na Kijana RWEHUMBIZA KALANGALI,ambaye ni mwanafunzi anayesoma huko Korea Kusini, na hapa anaeleza hali ilivyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

OBAMA ASIFU MAJESHI YA IRAQ NA KURD

Rais wa Marekani, Barack Obama
Rais wa Marekani Barack Obama amesema majeshi ya Iraq na yale ya Kikurd yamepiga hatua kubwa kulitwaa tena bwawa muhimu la Mosul kutoka kwa wapiganaji wa kiislamu kaskazini mwa Iraq.
Amesema wamethibitisha kwamba wanauwezo wa kufanya kazi kwa pamoja na wataendelea kuungwa mkono na majeshi ya Marekani, ambayo tayari yamefanya mashambulio Zaidi ya anga katika eneo linalokaliwa na wapiganaji wa kiislamu.

Ripoti zinasema kuwa mapambano katika juhudi za kudhibiti maeneo yanayozunguka bwawa hilo yanaendelea. Katika hatua nyingine kundi la himaya ya kiislamu linalofanya mashambulizi dhidi ya Wakurd limekanusha kwamba wapiganaji wake wamepoteza udhibiti wa bwawa hilo.

Wakati huohuo kiongozi wa kanisa katoliki duniani papa Francis amesema jumuia ya kimataifa itakuwa na haki katika kuchukua hatua dhidi ya wanamgambo hao. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Papa Amesema ni halali kuzuia kile alichokiita dhuluma ya kichokozi. Lakini ametahadharisha kuwa hatua yoyote itakayochukuliwa lazima ifanyiwe tathmini. kusimamisha na kwamba hakusema. Mwandishi wa BBC MJINI Roma Italia anasema papa Fransis hajaonesha kuunga mkono mashambulio ya anga yanayofanywa hivi sasa na Marekani dhidi ya wapiganaji hao wa kiislamu.

Na BBC

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...